< Proverbs 9 >

1 Wisedome hath built her house, and hewen out her seuen pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 She hath killed her vitailes, drawen her wine, and prepared her table.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 She hath sent forth her maydens and cryeth vpon the highest places of the citie, saying,
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 Who so is simple, let him come hither, and to him that is destitute of wisedome, she sayth,
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 Come, and eate of my meate, and drinke of the wine that I haue drawen.
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Forsake your way, ye foolish, and ye shall liue: and walke in the way of vnderstanding.
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 He that reproueth a scorner, purchaseth to himselfe shame: and he that rebuketh the wicked, getteth himselfe a blot.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 Rebuke not a scorner, least he hate thee: but rebuke a wise man, and he will loue thee.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Giue admonition to the wise, and he will be the wiser: teache a righteous man, and he will increase in learning.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 The beginning of wisedome is the feare of the Lord, and the knowledge of holy things, is vnderstanding.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 For thy dayes shalbe multiplied by me, and the yeeres of thy life shalbe augmented.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 If thou be wise, thou shalt be wise for thy selfe, and if thou be a scorner, thou alone shalt suffer.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 A foolish woman is troublesome: she is ignorant, and knoweth nothing.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 But she sitteth at the doore of her house on a seate in the hie places of the citie,
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 To call them that passe by the way, that go right on their way, saying,
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 Who so is simple, let him come hither, and to him that is destitute of wisedome, shee sayth also,
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 Stollen waters are sweete, and hid bread is pleasant.
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 But he knoweth not, that ye dead are there, and that her ghestes are in the depth of hell. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >