< Proverbs 6 >

1 My sonne, if thou be surety for thy neighbour, and hast striken hands with the stranger,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 Thou art snared with the wordes of thy mouth: thou art euen taken with the woordes of thine owne mouth.
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Doe this nowe, my sonne, and deliuer thy selfe: seeing thou art come into the hande of thy neighbour, goe, and humble thy selfe, and sollicite thy friends.
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 Giue no sleepe to thine eyes, nor slumber to thine eyelids.
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Deliuer thy selfe as a doe from the hande of the hunter, and as a birde from the hande of the fouler.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Goe to the pismire, O sluggarde: beholde her waies, and be wise.
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 For shee hauing no guide, gouernour, nor ruler,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 Prepareth her meat in the sommer, and gathereth her foode in haruest.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 Howe long wilt thou sleepe, O sluggarde? when wilt thou arise out of thy sleepe?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Yet a litle sleepe, a litle slumber, a litle folding of the hands to sleepe.
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 Therefore thy pouertie commeth as one that trauaileth by the way, and thy necessitie like an armed man.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 The vnthriftie man and the wicked man walketh with a froward mouth.
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 He maketh a signe with his eyes: he signifieth with his feete: he instructeth with his fingers.
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 Lewde things are in his heart: he imagineth euill at all times, and raiseth vp contentions.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Therefore shall his destruction come speedily: hee shall be destroyed suddenly without recouerie.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 These sixe things doeth the Lord hate: yea, his soule abhorreth seuen:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 The hautie eyes, a lying tongue, and the hands that shed innocent blood,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 An heart that imagineth wicked enterprises, feete that be swift in running to mischiefe,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 A false witnesse that speaketh lyes, and him that rayseth vp contentions among brethren.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 My sonne, keepe thy fathers commandement, and forsake not thy mothers instruction.
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Binde them alway vpon thine heart, and tye them about thy necke.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 It shall leade thee, when thou walkest: it shall watch for thee, when thou sleepest, and when thou wakest, it shall talke with thee.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 For the commandement is a lanterne, and instruction a light: and corrections for instruction are the way of life,
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 To keepe thee from the wicked woman, and from ye flatterie of ye tongue of a strange woman.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Desire not her beautie in thine heart, neither let her take thee with her eye lids.
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 For because of the whorish woman a man is brought to a morsell of bread, and a woman wil hunt for the precious life of a man.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Can a man take fire in his bosome, and his clothes not be burnt?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Or can a man go vpon coales, and his feete not be burnt?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 So he that goeth in to his neighbours wife, shall not be innocent, whosoeuer toucheth her.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 Men do not despise a thiefe, when he stealeth, to satisfie his soule, because he is hungrie.
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 But if he be founde, he shall restore seuen folde, or he shall giue all the substance of his house.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 But he that committeth adulterie with a woman, he is destitute of vnderstanding: he that doeth it, destroyeth his owne soule.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 He shall finde a wounde and dishonour, and his reproch shall neuer be put away.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 For ielousie is the rage of a man: therefore he will not spare in the day of vengeance.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 He cannot beare the sight of any raunsome: neither will he consent, though thou augment the giftes.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Proverbs 6 >