< Numbers 33 >

1 These are the iourneyes of the children of Israel, which went out of the land of Egypt according to their bands vnder the hand of Moses and Aaron.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 And Moses wrote their going out by their iourneies according to ye commandement of the Lord: so these are ye iourneies of their going out.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Nowe they departed from Rameses the first moneth, euen the fifteenth day of the first moneth, on the morowe after the Passeouer: and the children of Israel went out with an hie hand in the sight of all the Egyptians.
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 (For the Egyptians buried all their first borne, which the Lord had smitten among them: vpon their gods also the Lord did execution.)
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 And the children of Israel remoued from Rameses, and pitched in Succoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 And they departed from Succoth, and pitched in Etham, which is in the edge of the wildernesse.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 And they remoued from Etham, and turned againe vnto Pi-hahiroth, which is before Baal-zephon, and pitched before Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 And they departed from before Hahiroth, and went through the middes of the Sea into the wildernesse, and went three dayes iourney in the wildernesse of Etham, and pitched in Marah.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 And they remoued from Marah, and came vnto Elim, and in Elim were twelue fountaines of water, and seuentie palme trees, and they pitched there.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 And they remoued from Elim, and camped by the red Sea.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 And they remoued from the red Sea, and lay in the wildernesse of Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 And they tooke their iourney out of the wildernesse of Sin, and set vp their tentes in Dophkah.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 And they departed from Dophkah, and lay in Alush.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 And they remoued from Alush, and lay in Rephidim, where was no water for the people to drinke.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 And they departed from Rephidim, and pitched in the wildernesse of Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 And they remoued from the desert of Sinai, and pitched in Kibroth Hattaauah.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 And they departed from Kibroth Hattaauah, and lay at Hazeroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 And they departed from Hazeroth, and pitched in Rithmah.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 And they departed from Rithmah, and pitched at Rimmon Parez.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 And they departed from Rimmon Parez, and pitched in Libnah.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 And they remoued from Libnah, and pitched in Rissah.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 And they iourneyed from Rissah, and pitched in Kehelathah.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 And they went from Kehelathah, and pitched in mount Shapher.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 And they remoued from mount Shapher, and lay in Haradah.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 And they remoued from Haradah, and pitched in Makheloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 And they remoued from Makheloth, and lay in Tahath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 And they departed from Tahath, and pitched in Tarah.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 And they remoued from Tarah, and pitched in Mithkah.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 And they went from Mithkah, and pitched in Hashmonah.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 And they departed from Hashmonah, and lay in Moseroth.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 And they departed from Moseroth, and pitched in Bene-iaakan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 And they remoued from Bene-iaakan, and lay in Hor-hagidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 And they went from Hor-hagidgad, and pitched in Iotbathah.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 And they remoued from Iotbathah, and lay in Ebronah.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 And they departed from Ebronah, and lay in Ezion-gaber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 And they remoued from Ezion-gaber, and pitched in the wildernesse of Zin, which is Kadesh.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 And they remooued from Kadesh, and pitched in mount Hor, in the edge of the land of Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 (And Aaron the Priest went vp into mount Hor, at the commandement of the Lord, and died there, in the fourtieth yeere after the children of Israel were come out of the lande of Egypt, in the first day of the fifth moneth.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 And Aaron was an hundreth, and three and twentie yeere olde, when hee dyed in mount Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 And King Arad the Canaanite, which dwelt in the South of the land of Canaan, heard of the comming of the children of Israel)
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 And they departed from mount Hor, and pitched in Zalmonah.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 And they departed from Zalmonah, and pitched in Punon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 And they departed from Punon, and pitched in Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 And they departed from Oboth, and pitched in Iie-abarim, in the borders of Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 And they departed from Iim, and pitched in Dibon-gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 And they remooued from Dibon-gad, and lay in Almon-diblathaim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 And they remooued from Almon-diblathaim, and pitched in the mountaines of Abarim before Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 And they departed from the mountaines of Abarim, and pitched in the plaine of Moab, by Iorden toward Iericho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 And they pitched by Iorden, from Bethieshimoth vnto Abel-shittim in the playne of Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 And the Lord spake vnto Moses in the playne of Moab, by Iorden towarde Iericho, saying,
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, When ye are come ouer Iorden to enter into the land of Canaan,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 Ye shall then driue out all the inhabitants of the land before you, and destroy all their pictures, and breake asunder all their images of metall, and plucke downe all their hie places.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 And ye shall possesse the lande and dwell therein: for I haue giue you ye land to possesse it.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 And ye shall inherite the land by lot according to your families: to the more yee shall giue more inheritance, and to the fewer the lesse inheritance. Where the lot shall fall to any man, that shall be his: according to the tribes of your fathers shall ye inherite.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 But if ye will not driue out the inhabitants of the land before you, then those which yee let ramaine of them, shalbe prickes in your eyes, and thornes in your sides, and shall vexe you in the land wherein ye dwell.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Moreouer, it shall come to passe, that I shall doe vnto you, as I thought to do vnto them.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Numbers 33 >