< Numbers 23 >

1 And Balaam sayd vnto Balak, Builde me here seuen altars, and prepare me here seuen bullockes, and seuen rammes.
Balaamu akamwabia Balaki, “Jenga madhabahu saba kwa ajili yangu na uandae mafahari saba na kondoo dume saba.”
2 And Balak did as Balaam sayd, and Balak and Balaam offred on euery altar a bullocke and a ramme.
Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyoomba. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume mmoja kwa kila madhabahu.
3 Then Balaam sayde vnto Balak, Stande by the burnt offring, and I will goe, if so be that the Lord will come and meete me: and whatsoeuer he sheweth me, I will tell thee: so he went forth alone.
Ndipo Balaamu alipomwamiba Balaki, “Simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda. Labda BWANA atakuja kukutana na mimi. Chochote atakachoniambia nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya mlima usiokuwa na miti.
4 And God met Balaam, and Balaam sayd vnto him, I haue prepared seuen altars, and haue offred vpon euery altar a bullocke and a ramme.
Wakati bado akiwa juu ya mlima. Mungu akakutana naye, na Balaamu akamwambia, “Nimejenga madhabahu saba, na nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume kwa kila madhabahu.”
5 And the Lord put an answere in Balaams mouth, and sayde, Go againe to Balak, and say on this wise.
BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Baalamu akasema, “Rudi kwa Balaki ukamwambie.”
6 So when he returned vnto him, loe, hee stoode by his burnt offering, he, and all the princes of Moab.
Kwa hiyo Balaamu akarudi kwa Balaki aliyekuwa amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na viongozi wote wa Moabu walikuwa pamoja naye.
7 Then he vttered his parable, and sayde, Balak the king of Moab hath brought mee from Aram out of the mountaines of the East, saying, Come, curse Iaakob for my sake: come, and detest Israel.
Ndipo Balaamu alipoanza kunena unabii wake akisema, “Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki, 'Njoo, nilaanie Yakobo kwa ajili yangu,' alisema, 'Njoo umtie unajisi Israeli,'
8 How shall I curse, where God hath not cursed? or howe shall I detest, where the Lord hath not detested?
Nawezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wale ambao Mungu hawapingi?
9 For from the top of the rocks I did see him, and from the hils I did beholde him: lo, the people shall dwell by themselues, and shall not be reckened among the nations.
Kwa kuwa kutoka juu ya miamba Ninamwona; kutoka kwenye milima ninamtazama. Kuna watu wanaoishi pekee yao na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kawaida.
10 Who can tell the dust of Iaakob, and the nomber of the fourth part of Israel? Let me die the death of the righteous, and let my last ende be like his.
Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au kuhesabu hata robo ya Israeli? Naomba nife kifo cha mtu mwenye haki, na mwisho wa maisha yangu uwe kama wake!”
11 Then Balak saide vnto Balaam, What hast thou done vnto mee? I tooke thee to curse mine enemies, and beholde, thou hast blessed them altogether.
Balaki akamwambia Balaamu, “Umenifanyia nini? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini ona, umewabariki,”
12 And he answered, and said, Must I not take heede to speake that, which the Lord hath put in my mouth?
Balaamu akajibu akasema, “Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA anaweka kinywani mwangu?”
13 And Balak sayde vnto him, Come, I pray thee, with mee vnto another place, whence thou mayest see them, and thou shalt see but the vtmost part of them, and shalt not see them all: therefore curse them out of that place for my sake.
Basi Balaki akamwambia, “Hebu uje nami kwenye eneo jingine ili uwaone. Utakaowaona ni wale wa karibu tu, huwezi kuwaona wote. Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu.”
14 And he brought him into Sede-sophim to the top of Pisgah, and built seuen altars, and offred a bullocke, and a ramme on euery altar.
Kwa hiyo akampeleka Balaamu kwenye shamba la Zofimu, lililo juu ya Mlima Pisiga, na kule akajenga madhabau zingine saba. Akatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume kwa kila madhabahu.
15 After, he sayde vnto Balak, Stande here by thy burnt offring, and I wil meete the Lord yonder.
Kisha Balaamu akamwambia Balaki, “Simama hapa karibu na sadaka zako, wakati mimi naenda kukutana na BWANA kule.”
16 And the Lord mette Balaam, and put an answere in his mouth, and sayd, Goe againe vnto Balak, and say thus.
Kwa hiyo BWANA akakutana na Balaamu na kumwekea ujumbe kinywani mwake. Alimwambia, “Rudi kwa Balaki ukamwambie huu ujumbe toka kwangu.”
17 And when he came to him, beholde, hee stoode by his burnt offering, and the princes of Moab with him: so Balak sayde vnto him, What hath the Lord sayd?
Balaamu akamrudia, na tazama, alikuwa amesimama karibu na sadaka zake za kuteketezwa, na vionigozi wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamwuliza, “BWANA amekwambiaje?”
18 And he vttered his parable, and sayde, Rise vp, Balak, and heare: hearken vnto me, thou sonne of Zippor.
Balaamu akaanza kutoa unabii. Akasema, “Inuka, Balaki na usikilize. Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori.
19 God is not as man, that he should lie, neither as the sonne of man that he shoulde repent: hath he sayde and shall he not do it? and hath he spoken, and shall he not accomplish it?
Mungu siyo mtu, kwamba umdanganye, au mwanadamu awezaye kubadili mawazo. Je, alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanya kitu bila kufanya kama alivyosema?
20 Behold, I haue receiued commandement to blesse: for he hath blessed, and I cannot alter it.
Tazama, Mimi nimeamriwa kuwabariki. Mungu ametoa baraka, nami siwezi kuibadilisha.
21 Hee seeth none iniquitie in Iaakob, nor seeth no transgression in Israel: the Lord his God is with him, and the ioyfull shoute of a king is among them.
Hajawahi kuona magumu katika Yakobo au tabu katika Israeli. BWANA Mungu wao yuko pamoja nao, na kelele za wafalme wao ziko pamoja nao.
22 God brought them out of Egypt: their strength is as an vnicorne.
Mungu aliwatoa Misri kwa nguvu kama za nyati.
23 For there is no sorcerie in Iaakob, nor soothsaying in Israel: according to this time it shalbe sayde of Iaakob and of Israel, What hath God wrought?
Hakuna uganga utakaofanikiwa dhidi ya Yakobo, na hakuna uchawi utakaomwumiza Israeli. Badala yake, itasemwa juu ya Yakobo na Israeli, 'Tazama kile ambacho Mungu amefanya!'
24 Behold, the people shall rise vp as a lyon, and lift vp himselfe as a yong lyon: hee shall not lye downe, till he eate of the pray, and till he drinke the blood of the slayne.
Tazama, watu wanainuka kama simba jike, kama vile simba ainukavyo na kuvamia. Halali chini mpaka ale windo lake na kunywa damu ya windo lake,”
25 Then Balak sayde vnto Balaam, Neither curse, nor blesse them at all.
Kisha Balaki akamwambia Balaamu, “Kamwe usiwalaani wala kuwabariki.”
26 But Balaam answered, and saide vnto Balak, Tolde not I thee, saying, All that the Lord speaketh, that must I do?
Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?
27 Againe Balak sayd vnto Balaam, Come, I pray thee, I wil bring thee vnto another place, if so be it wil please God, that thou mayest thence curse them for my sake.
Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo sasa, Nami nitakupeleka mahali pengine. Labda kule itampendeza Mungu kunilaania hawa hawa watu.”
28 So Balak brought Balaam vnto the top of Peor, that looketh toward Ieshmon.
Kwa hiyo Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, ambao unalitazama chini lile jangwa,
29 Then Balaam sayde vnto Balak, Make me here seuen altars, and prepare me here seuen bullocks, and seuen rammes.
Balaamu akamwambia Balaki, “Nijengee madhabahu saba hapa na uniandalie mafahari saba na kondoo duume saba.
30 And Balak did as Balaam had sayd, and offred a bullocke and a ram on euery altar.
“Kwa hiyo Balaki akafanya kama alivyoambiwa; akatoa sadaka ya fahari na kondoo mume kwenye kila madhabahu.

< Numbers 23 >