< Numbers 11 >

1 When the people became murmurers, it displeased the Lord: and the Lord heard it, therefore his wrath was kindled, and the fire of the Lord burnt among them, and consumed the vtmost parte of the hoste.
Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi.
2 Then the people cryed vnto Moses: and when Moses praied vnto the Lord, the fire was quenched.
Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika.
3 And he called the name of that place Taberah, because the fire of the Lord burnt among them.
Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera, kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.
4 And a nomber of people that was amog them, fell a lusting, and turned away, and the children of Israel also wept, and saide, Who shall giue vs flesh to eate?
Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule!
5 We remember the fish which we did eat in Egypt for nought, the cucumbers, and the pepons, and the leekes, and the onions, and the garleke.
Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu.
6 But now our soule is dryed away, we can see nothing but this Man.
Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”
7 (The Man also was as coriander seede, and his colour like the colour of bdelium.
Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka.
8 The people went about and gathered it, and ground it in milles, or beat it in morters, and baked it in a cauldron, and made cakes of it, and the taste of it was like vnto the taste of fresh oyle.
Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni.
9 And when the dewe fell downe vpon the hoste in the night, the Man fell with it)
Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.
10 Then Moses heard the people weepe throughout their families, euery man in the doore of his tent, and the wrath of the Lord was grieuously kindled: also Moses was grieued.
Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika.
11 And Moses saide vnto the Lord, Wherefore hast thou vexed thy seruant? and why haue I not found fauour in thy sight, seeing thou hast put the charge of al this people vpon mee?
Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu?
12 Haue I conceiued al this people? or haue I begotte them, that thou shouldest say vnto me, Cary them in thy bosome (as a nurse beareth the sucking childe) vnto the lande, for the which thou swarest vnto their fathers?
Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao?
13 Where should I haue flesh to giue vnto al this people? for they weepe vnto me, saying, Giue vs flesh that we may eate.
Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’
14 I am not able to beare al this people alone, for it is too heauie for me.
Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu.
15 Therefore if thou deale thus with mee, I pray thee, if I haue founde fauour in thy sight, kill me, that I behold not my miserie.
Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”
16 Then the Lord said vnto Moses, Gather vnto me seuetie men of ye Elders of Israel, whome thou knowest, that they are the Elders of the people, and gouernonrs ouer them, and bring them vnto the Tabernacle of the Congregation, and let them stand there with thee,
Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe.
17 And I will come downe, and talke with thee there, and take of the Spirite, which is vpon thee, and put vpon them, and they shall beare the burthen of the people with thee: so thou shalt not beare it alone.
Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.
18 Furthermore thou shalt saye vnto the people, Bee sanctified against to morowe, and yee shall eate flesh: for you haue wept in the eares of the Lord, saying, Who shall giue vs flesh to eate? for we were better in Egypt: therefore the Lord will giue you flesh, and ye shall eate.
“Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila.
19 Ye shall not eat one day nor two daies, nor fiue daies, neither ten daies, nor twentie dayes,
Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini,
20 But a whole moneth, vntill it come out at your nostrels, and bee lothesome vnto you, because ye haue contemned the Lord, which is among you, and haue wept before him, saying, Why came we hither out of Egypt?
bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?”’”
21 And Moses saide, Six hundreth thousande footemen are there of the people, among whom I am: and thou saiest, I will giue them flesh, that they may eate a moneth long.
Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’
22 Shall the sheepe and the beeues be slaine for them, to finde them? either shall all the fish of the sea be gathered together for them to suffice them?
Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”
23 And the Lord saide vnto Moses, Is the Lordes hand shortened? thou shalt see now whether my word shall come to passe vnto thee, or no.
Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”
24 So Moses went out, and told the people the wordes of the Lord, and gathered seuentie men of the Elders of the people, and set them round about the Tabernacle.
Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema.
25 Then the Lord came downe in a cloude, and spake vnto him, and tooke of the Spirit that was vpon him, and put it vpon the seuentie Ancient men: and when the Spirit rested vpon them, then they prophecied, and did not cease.
Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.
26 But there remained two of the men in the hoste: the name of the one was Eldad, and the name of the other Medad, and the Spirit rested vpon them, (for they were of them that were written, and went not out vnto the Tabernacle) and they prophecied in the hoste.
Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini.
27 Then there ranne a yong man, and tolde Moses, and saide, Eldad and Medad doe prophesie in the hoste.
Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
28 And Ioshua the sonne of Nun the seruant of Moses one of his yong men answered and said, My lord Moses, forbid them.
Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”
29 But Moses saide vnto him, Enuiest thou for my sake? yea, would God that all the Lordes people were Prophets, and that the Lord woulde put his Spirit vpon them.
Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
30 And Moses returned into the hoste, he and the Elders of Israel.
Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.
31 Then there went foorth a winde from the Lord, and brought quailes from the Sea, and let them fall vpon the campe, a dayes iourney on this side, and a dayes iourney on the other side, round about the hoste, and they were about two cubites aboue the earth.
Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.
32 Then the people arose, al that day, and all the night, and all the next day, and gathered the quailes: he that gathered the least, gathered ten Homers full, and they spred them abroade for their vse round about the hoste.
Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.
33 While the flesh was yet betweene their teeth, before it was chewed, euen the wrath of the Lord was kindled against the people, and the Lord smote the people with an exceeding great plague.
Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.
34 So the name of the place was called, Kibroth-hattaauah: for there they buried the people that fell a lusting.
Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.
35 From Kibroth-hattaauah ye people tooke their iourney to Hazeroth, and abode at Hazeroth.
Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.

< Numbers 11 >