< Nehemiah 3 >

1 Then arose Eliashib the hie Priest with his brethren the Priestes, and they buylt the sheepegate: they repayred it, and set vp the doores thereof: euen vnto the tower of Meah repayred they it, and vnto the tower of Hananeel.
Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani, wakajenga lango la kondoo. Walitakasa na kuweka milango yake. Waliweka wakfu hadi mnara wa Hamea na hadi mnara wa Hananeli.
2 And next vnto him buylded the men of Iericho, and beside him Zaccur the sonne of Imri.
Baada yao watu wa Yeriko walijenga, na baada yao Zakuri mwana wa Imri alijenga.
3 But the fish port did the sonnes of Senaah buylde, which also layde the beames thereof, and set on the doores thereof, the lockes thereof, and the barres thereof.
Wana wa Senaa wakajenga lango la samaki. Wanaweka mihimili yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
4 And next vnto them fortified Merimoth, the sonne of Vrijah, the sonne of Hakkoz: and next vnto them fortified Meshullam, the sonne of Berechiah, the sonne of Meshezabeel: and next vnto them fortified Zadok, the sonne of Baana:
Meremoth aliandaa sehemu inayofuata. Yeye ni mwana wa Uria mwana wa Hakosi. Na baada yao Meshulamu akatengeneza. Yeye ni mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli. Karibu nao Sadoki akatengeneza. Yeye ni mwana wa Baana.
5 And next vnto them fortified the Tekoites: but the great men of them put not their neckes to the worke of their lordes.
Baada yao Watekoi wakatengeneza, lakini viongozi wao walikataa kufanya kazi iliyoagizwa na wakuu wao.
6 And the gate of the olde fishpoole fortified Iehoiada the sonne of Paseah, and Meshullam the sonne of Besodaiah: they laid the beames thereof, and set on the doores thereof, and the lockes thereof, and the barres thereof.
Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya, walitengeneza lango la Kale. Wanaweka mihimili, na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
7 Next vnto them also fortified Melatiah the Gibeonite, and Iadon the Meronothite, men of Gibeon, and of Mizpah, vnto the throne of the Duke, which was beyond the Riuer.
Nao, Melatia Mgibeoni, na Yadoni Meronothi, watu wa Gibeoni na Mispa, walifanyia matengenezo juu ya sehemu ambapo mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto aliishi.
8 Next vnto him fortified Vzziel the sonne of Harhohiah of the golde smithes: next vnto him also fortified Hananiah, the sonne of Harakkahim, and they repayred Ierusalem vnto the broad wall.
Na baada yake Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa wafua dhahabu, akatengeneza; na baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato. Wakajenga tena Yerusalemu mpaka Ukuta mpana.
9 Also next vnto them fortified Rephaiah, the sonne of Hur, the ruler of the halfe part of Ierusalem.
Na baada yao Refaya mwana wa Huri akajenga. Alikuwa mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu.
10 And next vnto him fortified Iedaiah the sonne of Harumaph, euen ouer against his house: and next vnto him fortified Hattush, the sonne of Hashabniah.
Na baada yao Yedaya mwana wa Harumafu akajenga karibu na nyumba yake. Na baada yake Hatushi mwana wa Hashabneya akajenga.
11 Malchiiah the sonne of Harim, and Hashub the sonne of Pahath Moab fortified the seconde porcion, and the tower of the fornaces.
Malkiya mwana wa Harimu na Hashubu mwana wa Pahat Moabu, wajenga sehemu nyingine pamoja na mnara wa tanuu.
12 Next vnto him also fortified Shallum, the sonne of Halloesh, the ruler of the halfe part of Ierusalem, he, and his daughters.
Baada yao Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akajenga, pamoja na binti zake.
13 The valley gate fortified Hanum, and the inhabitants of Zanuah: they buylt it, and set on the doores thereof, the lockes thereof, and the barres thereof, euen a thousand cubites on the wall vnto the dung porte.
Hanuni na wenyeji wa Zanoa walijenga lango la bondeni. Walijenga tena na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake. Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.
14 But the dung port fortified Malchiah, the sonne of Rechab, the ruler of the fourth part of Beth-haccarem: he built it, and set on the doores thereof, the lockes thereof, and the barres thereof.
Malkiya, mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-Hakeremu, akajenga lango la jaa. Alijenga na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake.
15 But the gate of the fountaine fortified Shallun, the sonne of Col-hozeh, the ruler of the fourth part of Mizpah: he builded it, and couered it, and set on the doores thereof, the lockes thereof, and the barres thereof, and the wall vnto the fishpoole of Shelah by the Kings garden, and vnto the steppes that goe downe from the citie of Dauid.
Shalumu mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa, akajenga lango la Chemchemi. Alijenga, na kuweka kifuniko juu yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake. Alijenga upya ukuta wa Pwani wa Silowamu kwa bustani ya mfalme, hadi ngazi ya kuongoza kutoka mji wa Daudi.
16 After him fortified Nehemiah the sonne of Azbuk, the ruler of ye halfe part of Beth-zur, vntill the otherside ouer against the sepulchres of Dauid, and to the fishpoole that was repaired, and vnto the house of the mightie.
Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-suri, akajenga mahali hapo, toka maburini ya Daudi, mpaka birika lililojengwa na watu, na nyumba ya watu wenye nguvu.
17 After him fortified the Leuites, Rehum the sonne of Bani, and next vnto him fortified Hashabiah the ruler of the halfe part of Keilah in his quarter.
Baada yake, Walawi walijenga, pamoja na Rehumi mwana wa Bani na baada yake, Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, kwa wilaya yake.
18 After him fortified their brethren: Bauai, the sonne of Henadad the ruler of the halfe part of Keilah:
Baada yake watu wa nchi zao walijenga, ikiwa ni pamoja na Binui mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
19 And next vnto him fortified Ezer, the sonne of Ieshua the ruler of Mizpah, the other portion ouer against the going vp to the corner of the armour.
Baada yake alijenga Ezeri, mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alijenga sehemu nyingine kuelekea ghala ya silaha, kwenye kona ya ukuta.
20 After him was earnest Baruch the sonne of Zacchai, and fortified another portion from the corner vnto the doore of the house of Eliashib the hie Priest.
Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akajenga kwa hiari sehemu nyingine, toka kona ya ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
21 After him fortified Merimoth, the sonne of Vriiah, the sonne of Hakkoz, another portion from the doore of the house of Eliashib, euen as long as the house of Eliashib extended.
Baada yake Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, akajenga sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
22 After him also fortified the Priests, the men of the playne.
Kisha baada yake makuhani, watu wa eneo hilo karibu na Yerusalemu, walijenga.
23 After them fortified Beniamin, and Hasshub ouer against their house: after him fortified Azariah, the sonne of Maaseiah, the sonne of Ananiah, by his house.
Baada yao Benyamini na Hashubu walijenga kuielekea nyumba yao. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, alijenga karibu na nyumba yake.
24 After him fortified Binnui, the sonne of Henadad another portion, from the house of Azariah vnto the turning and vnto the corner.
Baada yake Binui mwana wa Henadadi akajenga sehemu nyingine, kutoka nyumba ya Azaria hadi kona ya ukuta.
25 Palal, the sonne of Vzai, from ouer against the corner, and the high tower, that lieth out from the Kings house, which is beside the court of the prison. After him, Pedaiah, the sonne of Parosh.
Palali, mwana wa Uzai, akajenga juu ya kona ya ukuta na mnara unaoenea juu kutoka nyumba ya juu ya mfalme katika uwanda wa walinzi. Baada yake Pedaya mwana wa Paroshi akajenga.
26 And the Nethinims they dwelt in ye fortresse vnto the place ouer against the water gate, Eastwarde, and to the tower that lyeth out.
Sasa watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli walijenga mpaka upande wa Hifadhi ya Maji upande wa mashariki wa mnara unaojitokeza.
27 After him fortified the Tekoites another portion ouer against the great tower, that lyeth out, euen vnto the wall of the fortresse.
Baada yake, Watekoi walijenga sehemu nyingine, kuelekea mnara mkubwa ulio nje, mpaka ukuta wa Ofeli.
28 From aboue the horsegate forth fortified the Priests, euery one ouer against his house.
Makuhani wakajenga juu ya lango la farasi, kila mmoja kuelekea nyumba yake.
29 After them fortified Zadok the sonne of Immer ouer against his house: and after him fortified Shemaiah, the sonne of Shechadiah the keeper of the East gate.
Baada yao Sadoki, mwana wa Imeri, alijenga sehemu hiyo kuelekea nyumba yake. Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki, akajenga.
30 After him fortified Hananiah, the sonne of Shelemiah, and Hanun, the sonne of Zalaph, the sixt, another portion after him fortified Meshullam, the sonne of Berechiah, ouer against his chamber.
Baada yake Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, wakajenga sehemu nyingine. Meshulamu mwana wa Berekia akajenga kuelekea kwenye vyumba vyake.
31 After him fortified Malchiah the goldesmiths sonne, vntil the house of the Nethinims, and of ye marchants ouer against the gate Miphkad, and to the chamber in the corner.
Baada yake Malkiya, mmoja wa wafua dhahabu, akajenga mpaka nyumba ya watumishi wa hekalu na wafanyabiashara waliokuwa wakielekea lango la gereza na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
32 And betweene the chamber of the corner vnto the sheepegate fortified the goldesmithes and the marchantes.
Wafanyabiashara wa dhahabu na wafanyabiashara walijenga kati ya chumba cha juu cha kona na Lango la Kondoo.

< Nehemiah 3 >