< Matthew 22 >

1 Then Iesus answered, and spake vnto them againe in parables, saying,
Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
2 The kingdome of heauen is like vnto a certaine King which maried his sonne,
“Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
3 And sent foorth his seruants, to call them that were bidde to the wedding, but they woulde not come.
Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
4 Againe hee sent foorth other seruants, saying. Tell them which are bidden, Beholde, I haue prepared my dinner: mine oxen and my fatlings are killed, and all thinges are readie: come vnto the mariage.
“Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
5 But they made light of it, and went their wayes, one to his farme, and another about his marchandise.
“Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
6 And the remnant tooke his seruants, and intreated them sharpely, and slewe them.
Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
7 But when the King heard it, he was wroth, and sent foorth his warriers, and destroyed those murtherers, and burnt vp their citie.
Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
8 Then saide hee to his seruants, Truely the wedding is prepared: but they which were bidden, were not worthy.
“Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
9 Go ye therefore out into the high wayes, and as many as ye finde, bid them to the mariage.
Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
10 So those seruantes went out into the hie wayes, and gathered together all that euer they found, both good and bad: so the wedding was furnished with ghestes.
Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
11 Then the King came in, to see the ghestes, and sawe there a man which had not on a wedding garment.
“Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
12 And he sayd vnto him, Friend, how camest thou in hither, and hast not on a wedding garment? And he was speachlesse.
Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
13 Then sayd the King to the seruants, Binde him hand and foote: take him away, and cast him into vtter darkenes: there shalbe weeping and gnashing of teeth.
“Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
14 For many are called, but fewe chosen.
“Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
15 Then went the Pharises and tooke counsell how they might tangle him in talke.
Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
16 And they sent vnto him their disciples with the Herodians, saying, Master, we knowe that thou art true, and teachest the way of God truely, neither carest for any man: for thou considerest not the person of men.
Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
17 Tell vs therefore, how thinkest thou? Is it lawfull to giue tribute vnto Cesar, or not?
Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
18 But Iesus perceiued their wickednes, and sayd, Why tempt ye me, ye hypocrites?
Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
19 Shewe me the tribute money. And they brought him a peny.
Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
20 And he sayde vnto them, Whose is this image and superscription?
Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
21 They sayd vnto him, Cesars. Then sayd he vnto them, Giue therefore to Cesar, the things which are Cesars, and giue vnto God, those things which are Gods.
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
22 And when they heard it, they marueiled, and left him, and went their way.
Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
23 The same day the Sadduces came to him (which say that there is no resurrection) and asked him,
Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
24 Saying, Master, Moses sayd, If a man die, hauing no children, his brother shall marie his wife by the right of alliance, and raise vp seede vnto his brother.
“Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
25 Nowe there were with vs seuen brethren, and the first maried a wife, and deceased: and hauing none yssue, left his wife vnto his brother.
Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
26 Likewise also the second, and the third, vnto the seuenth.
Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
27 And last of all the woman died also.
Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
28 Therefore in the resurrection, whose wife shall she be of the seuen? for all had her.
Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
29 Then Iesus answered, and sayd vnto them, Ye are deceiued, not knowing the Scriptures, nor the power of God.
Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
30 For in the resurrection they neither marie wiues, nor wiues are bestowed in mariage, but are as the Angels of God in heauen.
Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
31 And concerning the resurrection of the dead, haue ye not read what is spoken vuto you of God, saying,
Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
32 I am the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Iacob? God is not the God of the dead, but of the liuing.
‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
33 And when the multitude heard it, they were astonied at his doctrine.
Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
34 But when the Pharises had heard, that he had put the Sadduces to silence, they assembled together.
Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
35 And one of them, which was an expounder of the Lawe, asked him a question, tempting him, and saying,
Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
36 Master, which is ye great commandement in the Lawe?
“Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
37 Iesus sayd to him, Thou shalt loue the Lord thy God with all thine heart, with all thy soule, and with all thy minde.
Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
38 This is the first and the great commandement.
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 And the second is like vnto this, Thou shalt loue thy neighbour as thy selfe.
Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
40 On these two commandements hangeth the whole Lawe, and the Prophets.
Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
41 While the Pharises were gathered together, Iesus asked them,
Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
42 Saying, What thinke ye of Christ? whose sonne is he? They sayd vnto him, Dauids.
“Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
43 He sayd vnto them, How then doeth Dauid in spirit call him Lord, saying,
Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
44 The Lord sayd to my Lord, Sit at my right hand, till I make thine enemies thy footestoole?
“‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
45 If then Dauid call him Lord, howe is he his sonne?
Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
46 And none could answere him a worde, neither durst any from that day foorth aske him any moe questions.
Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.

< Matthew 22 >