< Matthew 18 >

1 The same time the disciples came vnto Iesus, saying, Who is the greatest in the kingdome of heauen?
Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
2 And Iesus called a litle childe vnto him, and set him in the mids of them,
Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
3 And sayd, Verely I say vnto you, except ye be conuerted, and become as litle children, ye shall not enter into the kingdome of heauen.
Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
4 Whosoeuer therefore shall humble himselfe as this litle childe, the same is the greatest in the kingdome of heauen.
Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
5 And whosoeuer shall receiue one such litle childe in my name, receiueth me.
“Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
6 But whosoeuer shall offend one of these litle ones which beleeue in me, it were better for him, that a milstone were hanged about his necke, and that he were drowned in the depth of the sea.
Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
7 Wo be vnto the world because of offences: for it must needes be that offences shall come, but wo be to that man by whome the offence commeth.
“Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
8 Wherefore, if thy hand or thy foote cause thee to offend, cut them off, and cast them from thee: it is better for thee to enter into life, halt, or maimed, then hauing two hands, or two feete, to be cast into euerlasting fire. (aiōnios g166)
Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
9 And if thine eye cause thee to offende, plucke it out, and cast it from thee: it is better for thee to enter into life with one eye, then hauing two eyes to be cast into hell fire. (Geenna g1067)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
10 See that ye despise not one of these litle ones: for I say vnto you, that in heauen their Angels alwayes behold the face of my Father which is in heauen.
“Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
11 For the Sonne of man is come to saue that which was lost.
Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
12 How thinke ye? If a man haue an hundreth sheepe, and one of them be gone astray, doeth he not leaue ninetie and nine, and go into the mountaines, and seeke that which is gone astray?
“Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
13 And if so be that he finde it, verely I say vnto you, he reioyceth more of that sheepe, then of the ninetie and nine which went not astray:
Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
14 So is it not ye wil of your Father which is in heauen, that one of these litle ones should perish.
Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
15 Moreouer, if thy brother trespasse against thee, goe and tell him his fault betweene thee and him alone: if he heare thee, thou hast wonne thy brother.
“Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
16 But if he heare thee not, take yet with thee one or two, that by the mouth of two or three witnesses euery worde may be confirmed.
Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
17 And if he refuse to heare them, tell it vnto the Church: and if he refuse to heare the Church also, let him be vnto thee as an heathen man, and a Publicane.
Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
18 Verely I say vnto you, Whatsoeuer ye bind on earth, shall be bound in heauen: and whatsoeuer ye loose on earth, shalbe loosed in heauen.
“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
19 Againe, verely I say vnto you, that if two of you shall agree in earth vpon any thing, whatsoeuer they shall desire, it shall be giuen them of my Father which is in heauen.
“Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
20 For where two or three are gathered together in my Name, there am I in the mids of them.
Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
21 Then came Peter to him, and said, Master, howe oft shall my brother sinne against me, and I shall forgiue him? vnto seuen times?
Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
22 Iesus said vnto him, I say not to thee, Vnto seuen times, but, Vnto seuentie times seuen times.
Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Therefore is the kingdome of heauen likened vnto a certaine King, which would take an account of his seruants.
“Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
24 And when he had begun to reckon, one was brought vnto him, which ought him ten thousand talents.
Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
25 And because he had nothing to pay, his Lord commanded him to be solde, and his wife, and his children, and all that he had, and the dette to be payed.
Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
26 The seruant therefore fell downe, and worshipped him, saying, Lord, refraine thine anger toward me, and I will pay thee all.
“Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
27 Then that seruants Lord had compassion, and loosed him, and forgaue him the dette.
Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
28 But when the seruant was departed, hee found one of his felow seruants, which ought him an hundred pence, and he layde hands on him, and thratled him, saying, Pay me that thou owest.
“Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
29 Then his fellow seruant fell downe at his feete, and besought him, saying, Refraine thine anger towards me, and I will pay thee all.
“Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
30 Yet he would not, but went and cast him into prison, till he should pay the dette.
“Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
31 And when his other felowe seruants sawe what was done, they were very sory, and came, and declared vnto their Lord all that was done.
Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
32 Then his Lord called him vnto him, and sayd to him, O euil seruant, I forgaue thee all that dette, because thou prayedst me.
“Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
33 Oughtest not thou also to haue had pitie on thy fellowe seruant, euen as I had pitie on thee?
Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
34 So his Lord was wroth, and deliuered him to the tormentours, till he should pay all that was due to him.
Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
35 So likewise shall mine heauenly Father doe vnto you, except ye forgiue from your hearts, eche one to his brother their trespasses.
“Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”

< Matthew 18 >