< Matthew 15 >

1 Then came to Iesus the Scribes and Pharises, which were of Hierusalem, saying,
Ndipo Mafarisayo na waadishi walikuja kwa Yesu kutoka Yerusalemu. Na kusema,
2 Why do thy disciples transgresse the tradition of the Elders? for they wash not their hands when they eate bread.
“Kwa nini wanafunzi wanayahalifu mapokeo ya wazee? Kwa kuwa hawanawi mikono yao wanapokuwa wanakula chakula.''
3 But he answered and said vnto them, Why doe yee also transgresse the commandement of God by your tradition?
Yesu akawajibu na kuwaambia, “Nanyi kwa nini mnaihalifu sheria ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 For God hath commanded, saying, Honour thy father and mother: and he that curseth father or mother, let him die the death.
Kwa kuwa Mungu alisema, 'Mheshimu baba yako na mama yako; na 'Asemaye uovu kwa baba yake na mama yake, hakika atakufa.'
5 But ye say, Whosoeuer shall say to father or mother, By the gift that is offered by me, thou maiest haue profite,
Lakini ninyi husema, 'Kila amwambiaye baba yake na mama yake, '“Kila msaada ambao angepata kutoka kwangu sasa ni zawadi kutoka kwa Mungu,'''
6 Though hee honour not his father, or his mother, shalbe free: thus haue ye made the commandement of God of no aucthoritie by your tradition.
“Mtu huyo hana haja ya kumuheshimu baba yake. Katika namna hii mmelitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.
7 O hypocrites, Esaias prophecied well of you, saying,
Enyi wanafiki, ni vema kama Isaya alivyo tabiri juu yenu aliposema,
8 This people draweth neere vnto me with their mouth, and honoureth me with the lips, but their heart is farre off from me.
'Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 But in vaine they worship me, teaching for doctrines, mens precepts.
Wananiabudu bure, kwa sababu wanafundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”'
10 Then hee called the multitude vnto him, and said to them, Heare and vnderstand.
Ndipo akawaita makutano na kuwaambia,” Sikilizeni na mfahamu
11 That which goeth into the mouth, defileth not the man, but that which commeth out of the mouth, that defileth the man.
Hakuna kitu kiingiacho mdomoni mwa mtu na kumfanya najisi. Bali, kile kitokacho kinywani, hiki ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.''
12 Then came his disciples, and saide vnto him, Perceiuest thou not, that the Pharises are offended in hearing this saying?
Ndipo wanafunzi wakamwendea na kusema na Yesu, “Je!, Unafahamu Mafarisayo walipolisikia lile neno walikwazika?”
13 But hee answered and saide, Euery plant which mine heauenly Father hath not planted, shalbe rooted vp.
Yesu aliwajibu na kusema, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang'olewa.
14 Let them alone, they be the blinde leaders of the blinde: and if the blinde leade ye blinde, both shall fall into the ditche.
Waacheni pekee, wao ni viongozi vipofu. Kama mtu kipofu atamuongoza kipofu mwenzake, wote wawili wataanguka shimoni.”
15 Then answered Peter, and said to him, Declare vnto vs this parable.
Petro akajibu na kumwambia Yesu,” Tuelezee mfano huu kwetu,
16 Then said Iesus, Are ye yet without vnderstanding?
Yesu akajibu, ''Nanyi pia bado hamuelewi?
17 Perceiue ye not yet, that whatsoeuer entreth into the mouth, goeth into the bellie, and is cast out into the draught?
Ninyi hamuoni kuwa kila kiendacho mdomoni hupitia tumboni na kwenda chooni?
18 But those thinges which proceede out of the mouth, come from the heart, and they defile the man.
Lakini vitu vyote vitokavyo mdomoni hutoka ndani ya moyo. Ndivyo vitu vimtiavyo mtu unajisi.
19 For out of the heart come euil thoughts, murders, adulteries, fornications, thefts, false testimonies, slaunders.
Kwa kuwa katika moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi.
20 These are the things, which defile the man: but to eat with vnwashen hands, defileth not ye man.
Haya ndiyo mambo yamtiayo mtu unajisi. Lakini kula bila kunawa mikono hakumfanyi mtu kuwa najisi.”
21 And Iesus went thence, and departed into the coastes of Tyrus and Sidon.
Ndipo Yesu akatoka mahali pale na akajitenga kuelekea pande za miji ya Tiro na Sidoni.
22 And beholde, a woman a Cananite came out of the same coasts, and cried, saying vnto him, Haue mercie on me, O Lord, the sonne of Dauid: my daughter is miserably vexed with a deuil.
Tazama akaja mwanamke Mkanani kutoka pande hizo. Akapaza sauti akisema, ''Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu anateswa sana na pepo.''
23 But hee answered her not a worde. Then came to him his disciples, and besought him, saying, Sende her away, for she crieth after vs.
Lakini Yesu hakumjibu neno. Wanafunzi wake wakaja wakimsihi, wakisema, ''Muondoe aende zake, maana anatupigia kelele.''
24 But he answered, and said, I am not sent, but vnto the lost sheepe of the house of Israel.
Yesu aliwajibu na kusema, Sikutumwa kwa mtu yeyoye isipokuwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.''
25 Yet she came, and worshipped him, saying, Lord, helpe me.
Lakini alikuja na kuinama mbele yake, akisema, ''Bwana nisaidie.''
26 And he answered, and said, It is not good to take the childrens bread, and to cast it to whelps.
Alimjibu na kusema, “Siyo vema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa,”
27 But she said, Trueth, Lord: yet in deede the whelpes eate of the crommes, which fall from their masters table.
Akasema, “Ndiyo, Bwana, hata hivyo mbwa wadogo hula chakula kiagukacho mezani mwa Bwana wao.”
28 Then Iesus answered, and saide vnto her, O woman, great is thy faith: be it to thee, as thou desirest. And her daughter was made whole at that houre.
Ndipo Yesu akajibu na akisema “Mwanamke, imani yako ni kubwa. Na ifanyike kwako kama utakavyo.” Na binti yake alikuwa ameponywa katika wakati huo.
29 So Iesus went away from thence, and came neere vnto the sea of Galile, and went vp into a mountaine and sate downe there.
Yesu aliondoka mahali pale na kwenda karibu na bahari ya Galilaya. Kisha alienda juu ya mlima na kuketi huko.
30 And great multitudes came vnto him, hauing with them, halt, blinde, dumme, maymed, and many other, and cast them downe at Iesus feete, and he healed them.
Kundi kubwa likaja kwake. Na kumletea viwete, vipofu, bubu, vilema na wengine wengi, waliokuwa wagonjwa. Waliwaweka katika miguu ya Yesu na akawaponya.
31 In so much that the multitude wondered, to see the dumme speake, the maimed whole, the halt to goe, and the blinde to see: and they glorified the God of Israel.
Nao umati wakashangaa walipoona mabubu wakiongea, na vilema wakifanywa wazima, viwete wakitembea, na vipofu wakiona. Walimsifu Mungu wa Israeli.
32 Then Iesus called his disciples vnto him, and said, I haue compassion on this multitude, because they haue continued with mee already three dayes, and haue nothing to eate: and I wil not let them depart fasting, least they faint in the way.
Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema, “Nimewaonea huruma umati, kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu bila kula kitu chochote. Sitawaaga waende kwao bila kula, wasije wakazimia njiani.”
33 And his disciples saide vnto him, Whence should we get so much bread in the wildernes, as should suffice so great a multitude!
Wanafunzi wake wakamwambia, “Ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati mkuwbwa hivi?”
34 And Iesus said vnto them, How many loaues haue ye? And they said, Seuen, and a few litle fishes.
Yesu akawaambia, “Mna mikate mingapi?” Wakasema, “Saba, na samaki wadogo wachache.”
35 Then he commanded the multitude to sit downe on the ground,
Yesu akawaamuru umati uketi chini.
36 And tooke the seuen loaues, and the fishes, and gaue thankes, and brake them, and gaue to his disciples, and the disciples to the multitude.
Aliitwaa ile mikate saba na samaki, na baada ya kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi. Wanafunzi wakawapa umati.
37 And they did all eate, and were sufficed: and they tooke vp of the fragments that remained, seuen baskets full.
Watu wote wakala na kutosheka. Na wakakusanya mabaki ya vipande vya chakula vilivyosalia vipande vipande, vilijaa vikapu saba.
38 And they that had eaten, were foure thousand men, beside women, and litle children.
Wote waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake na watoto.
39 Then Iesus sent away the multitude, and tooke ship, and came into the partes of Magdala.
Kisha Yesu akauaga umati waende zao na akaingia ndani ya mashua na kwenda sehemu za Magadani.

< Matthew 15 >