< Luke 3 >

1 Nowe in the fifteenth yeere of the reigne of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being gouernour of Iudea, and Herod being Tetrarch of Galile, and his brother Philip Tetrarch of Iturea, and of the countrey of Trachonitis, and Lysanias the Tetrarch of Abilene,
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 (When Annas and Caiaphas were the hie Priestes) the worde of God came vnto Iohn, the sonne of Zacharias in the wildernes.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 And hee came into all the coastes about Iordan, preaching the baptisme of repentance for the remission of sinnes,
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 As it is written in the booke of the sayings of Esaias the Prophet, which saith, The voyce of him that crieth in the wildernes is, Prepare ye the way of the Lord: make his paths straight.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Euery valley shalbe filled, and euery mountaine and hill shall be brought lowe, and crooked things shalbe made straight, and the rough wayes shalbe made smoothe.
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 And all flesh shall see the saluation of God.
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Then said he to the people that were come out to be baptized of him, O generations of vipers, who hath forewarned you to flee from the wrath to come?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Bring foorth therefore fruites worthy amendment of life, and beginne not to say with your selues, We haue Abraham to our father: for I say vnto you, that God is able of these stones to raise vp children vnto Abraham.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 Nowe also is the axe layed vnto the roote of the trees: therefore euery tree which bringeth not foorth good fruite, shalbe hewen downe, and cast into the fire.
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 Then the people asked him, saying, What shall we doe then?
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 And he answered, and said vnto them, He that hath two coates, let him part with him that hath none: and hee that hath meate, let him doe likewise.
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Then came there Publicanes also to bee baptized, and saide vnto him, Master, what shall we doe?
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 And hee saide vnto them, Require no more then that which is appointed vnto you.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 The souldiers likewise demaunded of him, saying, And what shall we doe? And he saide vnto them, Doe violence to no man, neither accuse any falsely, and be content with your wages.
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 As the people waited, and all men mused in their heartes of Iohn, if he were not that Christ,
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 Iohn answered, and saide to them all, In deede I baptize you with water, but one stronger then I, commeth, whose shoes latchet I am not worthy to vnloose: hee will baptize you with the holy Ghost, and with fire.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Whose fanne is in his hande, and hee will make cleane his floore, and will gather the wheate into his garner, but the chaffe will hee burne vp with fire that neuer shalbe quenched.
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 Thus then exhorting with many other things, he preached vnto the people.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 But when Herod the Tetrarch was rebuked of him, for Herodias his brother Philips wife, and for all the euils which Herod had done,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 He added yet this aboue all, that he shut vp Iohn in prison.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 Nowe it came to passe, as all the people were baptized, and that Iesus was baptized and did pray, that the heauen was opened:
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 And the holy Ghost came downe in a bodily shape like a doue, vpon him, and there was a voyce from heauen, saying, Thou art my beloued Sonne: in thee I am well pleased.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 And Iesus himselfe began to bee about thirtie yeere of age, being as men supposed the sonne of Ioseph, which was the sonne of Eli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 The sonne of Matthat, the sonne of Leui, the sonne of Melchi, the sonne of Ianna, the sonne of Ioseph,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 The sonne of Mattathias, the sonne of Amos, the sonne of Naum, the sonne of Esli, the sonne of Nagge,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 The sonne of Maath, the sonne of Mattathias, the sonne of Semei, the sonne of Ioseph, the sonne of Iuda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 The sonne of Ioanna, the sonne of Rhesa, the sonne of Zorobabel, the sonne of Salathiel, the sonne of Neri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 The sonne of Melchi, the sonne of Addi, the sonne of Cosam, the sonne of Elmodam, the sonne of Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 The sonne of Iose, the sonne of Eliezer, the sonne of Iorim, the sonne of Matthat, the son of Leui,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 The sonne of Simeon, the sonne of Iuda, the sonne of Ioseph, the sonne of Ionan, the sonne of Eliacim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 The sonne of Melea, the sonne of Mainan, the sonne of Mattatha, the sonne of Nathan, the sonne of Dauid,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 The sonne of Iesse, the sonne of Obed, the sonne of Booz, the sonne of Salmon, the sonne of Naasson,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 The sonne of Aminadab, the sonne of Aram, the sonne of Esrom, the sonne of Phares, the sonne of Iuda,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 The sonne of Iacob, the sonne of Isaac, the sonne of Abraham, the sonne of Thara, the sonne of Nachor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 The sonne of Saruch, the sonne of Ragau, the sonne of Phalec, the sonne of Eber, the sonne of Sala,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 The sonne of Cainan, the sonne of Arphaxad, the sonne of Sem, the sonne of Noe, the sonne of Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 The sonne of Mathusala, the sonne of Enoch, the sonne of Iared, the sonne of Maleleel, the sonne of Cainan,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 The sonne of Enos, the sonne of Seth, the sonne of Adam, the sonne of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >