< Luke 24 >

1 Nowe the first day of the weeke early in the morning, they came vnto the sepulchre, and brought the odours, which they had prepared, and certaine women with them.
Mapema sana siku ya kwanza ya juma, walikuja kaburini, wakileta manukato ambayo walikuwa wameyaandaa.
2 And they found the stone rolled away from the sepulchre,
Wakakuta jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
3 And went in, but found not the body of the Lord Iesus.
Wakaingia ndani, lakini hawakuukuta mwili wa Bwana Yesu.
4 And it came to passe, that as they were amased thereat, beholde, two men suddenly stood by them in shining vestures.
Ilitokea kwamba, wakati wamechanganyikiwa kuhusu hili, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi ya kung'aa.
5 And as they were afraide, and bowed downe their faces to the earth, they sayd to them, Why seeke ye him that liueth, among the dead?
Wanawake wakiwa wamejaa hofu na wakiinamisha nyuso zao chini, wakawaambia wanawake, “Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
6 He is not here, but is risen: remember how he spake vnto you, when he was yet in Galile,
Hayupo hapa, ila amefufuka! Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa angali Galilaya,
7 Saying, that the sonne of man must be deliuered into the hands of sinfull men, and be crucified, and the third day rise againe.
akisema kwamba Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe, na siku ya tatu, afufuke tena.”
8 And they remembred his wordes,
Wale wanawake wakakumbuka maneno yake,
9 And returned from the sepulchre, and tolde all these things vnto the eleuen, and to all the remnant.
na wakarudi kutoka kaburini na wakawaambia mambo haya yote wale kumi na moja na wengine wote.
10 Now it was Mary Magdalene, and Ioanna, and Mary the mother of Iames, and other women with them, which tolde these things vnto the Apostles.
Basi Maria Magdalena, Joana, Maria mama wa Yakobo, na wanawake wengine pamoja nao wakatoa taarifa hizi kwa mitume.
11 But their wordes seemed vnto them, as a fained thing, neither beleeued they them.
Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaha tu kwa mitume, na hawakuwaamini wale wanawake.
12 Then arose Peter, and ran vnto the sepulchre, and looked in, and saw the linnen clothes laide by themselues, and departed wondering in himselfe at that which was come to passe.
Hata hivyo Petro aliamka, na akakimbia kuelekea kaburini, na akichungulia na kuangalia ndani, aliona sanda peke yake. Petro kisha akaondoka akaenda nyumbani kwake, akistaajabu nini ambacho kimetokea.
13 And beholde, two of them went that same day to a towne which was from Hierusalem about threescore furlongs, called Emmaus.
Na tazama, wawili miongoni mwao walikuwa wakienda siku hiyo hiyo katika kijiji kimoja kiitwacho Emmau, ambacho kilikuwa maili sitini kutoka Yerusalemu.
14 And they talked together of al these things that were done.
Wakajadiliana wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotokea.
15 And it came to passe, as they communed together, and reasoned, that Iesus himselfe drewe neere, and went with them.
Ikatokea kwamba, wakati walipokuwa wakijadiliana na kuulizana maswali, Yesu akasogea karibu akaambatana nao.
16 But their eyes were holden, that they could not know him.
Lakini macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye.
17 And he sayd vnto them, What maner of communications are these that ye haue one to another as ye walke and are sad?
Yesu akawaambia, “Nini ambacho ninyi wawili mnakiongelea wakati mnatembea?” Wakasimama pale wakionekana na huzuni.
18 And the one (named Cleopas) answered, and sayd vnto him, Art thou onely a stranger in Hierusalem, and hast not knowen the things which are come to passe therein in these dayes?
Mmoja wao, jina lake Cleopa, akamjibu, “Je wewe ni mtu pekee hapa Yerusalemu ambaye hajui mambo yaliyotokea huko siku hizi?”
19 And he said vnto them, What things? And they sayd vnto him, Of Iesus of Nazareth, which was a Prophet, mightie in deede and in word before God, and all people,
Yesu akawaambia, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo kuhusu Yesu Mnazareti, ambaye alikuwa nabii, muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote.
20 And howe the hie Priests, and our rulers deliuered him to be condemned to death, and haue crucified him.
Na kwa jinsi ambayo wakuu wa makuhani na viongozi wetu walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha.
21 But we trusted that it had bene he that should haue deliuered Israel, and as touching all these things, to day is ye third day, that they were done.
Lakini tulitumaini kwamba yeye ndiye atakaye waweka huru Israeli. Ndiyo, mbali na haya yote, sasa ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
22 Yea, and certaine women among vs made vs astonied, which came early vnto the sepulchre.
Lakini pia, baadhi ya wanawake kutoka katika kundi letu walitushangaza, baada ya kuwapo kaburini asubuhi na mapema.
23 And when they found not his body, they came, saying, that they had also seene a vision of Angels, which sayd, that he was aliue.
Walipoukosa mwili wake, wakaja, wakisema kwamba waliona pia maono ya malaika waliosema kwamba yu hai.
24 Therefore certaine of them which were with vs, went to the sepulchre, and found it euen so as the women had sayd, but him they saw not.
Baadhi ya wanaume ambao walikuwa pamoja nasi walienda kaburini, na kukuta ni kama vile wanawake walivyosema. Lakini hawakumuona yeye.”
25 Then he sayd vnto them, O fooles and slowe of heart to beleeue all that the Prophets haue spoken!
Yesu akawaambia, “Ninyi watu wajinga na wenye mioyo mizito ya kuamini yote ambayo manabii wamesema!
26 Ought not Christ to haue suffered these things, and to enter into his glory?
Je haikuwa lazima Yesu kuteseka kwa mambo haya, na kuingia katika utukufu wake?”
27 And he began at Moses, and at all the Prophets, and interpreted vnto them in all the Scriptures the things which were written of him.
Kisha kuanzia kutoka kwa Musa na manabii wote, Yesu akawatafsiria mambo yanayomuhusu yeye katika maandiko yote.
28 And they drew neere vnto ye towne, which they went to, but he made as though hee would haue gone further.
Walipokaribia kile kijiji, huko walikokuwa wakienda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea mbele.
29 But they constrained him, saying, Abide with vs: for it is towards night, and the day is farre spent. So he went in to tarie with them.
Lakini walimlazimisha, wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana inaelekea jioni na siku ni kama imeisha.” Hivyo Yesu akaingia kwenda kukaa nao.
30 And it came to passe, as hee sate at table with them, he tooke the bread, and blessed, and brake it, and gaue it to them.
Ilitokea kwamba, wakati amekaa nao kula, alichukua mkate, akaubariki, na kuuvunja, akawapa.
31 Then their eyes were opened, and they knewe him: and he was no more seene of them.
Kisha macho yao yakafunguliwa, wakamjua, na akatoweka ghafla mbele ya macho yao.
32 And they saide betweene themselues, Did not our heartes burne within vs, while he talked with vs by the way, and when he opened to vs the Scriptures?
Wakasemezana wao kwa wao, “Hivi mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipoongea nasi njiani, wakati alipotufungulia maandiko?”
33 And they rose vp the same houre, and returned to Hierusalem, and found the Eleuen gathered together, and them that were with them,
Wakanyanyuka saa hiyo hiyo, na kurudi Yerusalemu. Wakawakuta wale kumi na mmoja wamekusanyika pamoja, na wale waliokuwa pamoja nao,
34 Which said, The Lord is risen in deede, and hath appeared to Simon.
wakisema, “Bwana amefufuka kwelikweli, na amemtokea Simoni.”
35 Then they tolde what things were done in the way, and howe he was knowen of them in breaking of bread.
Hivyo wakawaambia mambo yaliyotokea njiani, na namna Yesu alivyodhihirishwa kwao katika kuumega mkate.
36 And as they spake these things, Iesus himselfe stoode in the middes of them, and saide vnto them, Peace be to you.
Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
37 But they were abashed and afraide, supposing that they had seene a spirit.
Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
38 Then he saide vnto them, Why are ye troubled? and wherefore doe doutes arise in your hearts?
Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
39 Beholde mine handes and my feete: for it is I my selfe: handle me, and see: for a spirit hath not flesh and bones, as ye see me haue.
Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
40 And when he had thus spoken, he shewed them his hands and feete.
Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
41 And while they yet beleeued not for ioy, and wondred, he saide vnto them, Haue ye here any meate?
Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
42 And they gaue him a piece of a broyled fish, and of an honie combe,
Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
43 And hee tooke it, and did eate before them.
Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
44 And he saide vnto them, These are the wordes, which I spake vnto you while I was yet with you, that all must be fulfilled which are written of me in the Lawe of Moses, and in the Prophets, and in the Psalmes.
Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
45 Then opened he their vnderstanding, that they might vnderstand the Scriptures,
Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
46 And said vnto them, Thus is it written, and thus it behoued Christ to suffer, and to rise againe from the dead the third day,
Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
47 And that repentance, and remission of sinnes should be preached in his Name among all nations, beginning at Hierusalem.
Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
48 Nowe ye are witnesses of these things.
Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
49 And beholde, I doe sende the promise of my Father vpon you: but tary ye in the citie of Hierusalem, vntill ye be endued with power from an hie.
Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
50 Afterward he lead them out into Bethania, and lift vp his hands, and blessed them.
Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
51 And it came to passe, that as he blessed them, he departed from them, and was caried vp into heauen.
Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
52 And they worshipped him, and returned to Hierusalem with great ioy,
Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
53 And were continually in the Temple, praysing, and lauding God, Amen.
Waliendelea kuwepo hekaluni, wakimbariki Mungu.

< Luke 24 >