< Leviticus 5 >

1 Also if any haue sinned, that is, If he haue heard the voyce of an othe, and hee can be a witnes, whether he hath seene or knowen of it, if hee doe not vtter it, he shall beare his iniquitie:
Kama mtu atatenda dhambi kwa sababu hakusema ukweli wakati alipotakiwa kutoa ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa, ameona au kufahamu habari zake, yeye anastahili adhabu.
2 Either if one touche any vncleane thing, whether it be a carion of an vncleane beast, or a carion of vncleane cattel, or a carion of vncleane creeping things, and is not ware of it, yet he is vncleane, and hath offended:
Au mtu akigusa kitu chochote ambacho Mungu amekitaja kuwa ni najisi hata kama ni mzoga wa wanyama wa porini au ni mzoga wa wanyama wa kufugwa au wataambaao hata kama mtu huyo hakukusudia kumgusa, yeye ni najisi na mwenye hatia.
3 Eyther if hee touche any vncleannesse of man (whatsoeuer vncleannes it be, that hee is defiled with) and is not ware of it, and after commeth to the knowledge of it, he hath sinned:
Au amegusa kitu chochote kilicho kichafu, kwa vyovyote kama hakujua, ndipo atakuwa na hatia akijua vile.
4 Either if any sweare and pronounce with his lippes to do euill, or to doe good (whatsoeuer it bee that a man shall pronounce with an othe) and it be hid from him, and after knoweth that he hath offended in one of these poyntes,
Au kama yeyote akiapa bila kufikiri kwa midomo yake kufanya ubaya, au kufanya vyema kwa vyovyote vile mtu ameapa kwa haraka atakapotambua atakuwa na hatia kwa vitu hivyo.
5 Whe he hath sinned in any of these things, then he shall confesse that he hath sinned therein.
Mtu yeyote akiwa na hatia kwa vitu hivi, lazima akiri kwa yoyote dhambi aliyotenda.
6 Therefore shall he bring his trespasse offring vnto the Lord for his sinne which he hath committed, euen a female from ye flocke, be it a lambe or a she goat for a sinne offring, and the Priest shall make an atonement for him, concerning his sinne.
Ndipo atakapoleta sadaka yake ya hatia mbele za Bwana kwa dhambi aliyokwisha tenda. Ataleta kondoo jike au mbuzi kutoka katika kundi lake kuwa matoleo ya dhambi, kuhani atafanya upatanisho kuhusu dhambi yake.
7 But if he be not able to bring a sheepe, he shall bring for his trespas which he hath committed, two turtle doues, or two yong pigeons vnto the Lord, one for a sinne offring, and the other for a burnt offring.
Kama hataweza kununua mwana kondoo ataleta kama sadaka ya hatia, hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana, mmoja kwa sadaka ya dhambi na mwingine ni sadaka ya kutekeketezwa.
8 So he shall bring them vnto the Priest, who shall offer the sinne offring first, and wring the necke of it a sunder, but not plucke it cleane off.
Atawaleta kwa kuhani, wa kwanza atatoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake katika mwili.
9 After he shall sprinkle of the blood of the sinne offring vpon the side of the altar, and the rest of the blood shall be shed at the foote of the altar: for it is a sinne offering.
Ndipo atanyunyizia damu yake katika sehemu za madhabahu, na damu inayobaki ataimwaga chini ya madhabahu. Hii ni dhabihu ya dhambi.
10 Also he shall offer the seconde for a burnt offring as the maner is: so shall the Priest make an atonement for him (for his sinne which hee hath committed) and it shalbe forgiuen him.
Ndipo ataoa ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoelekezwa, na kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi alizokwisha kufanya, na huyo mtu atakuwa amesamehewa.
11 But if he be not able to bring two turtle doues, or two yong pigeons, then he that hath sinned, shall bring for his offring, the tenth parte of an Ephah of fine floure for a sinne offring, he shall put none oyle thereto, neither put any incense thereon: for it is a sinne offering.
Lakini kama hataweza kununua hua wawili au makinda ya njiwa mawili, ndipo ataleta kama dhabihu ya dhambi zake sehemu ya kumi ya unga laini kama sadaka ya dhambi. Asiweke mafuta wala ubani juu yake, kwa kuwa ni sadaka ya dhambi.
12 Then shall hee bring it to the Priest, and the Priest shall take his handfull of it for the remembrance thereof, and burne it vpon the altar with the offrings of the Lord made by fire: for it is a sinne offring.
Atauleta kwa kuhani, na kuhani atachukua konzi moja ya unga kama ukumbusho wa wema wa Bwana na atauweka juu ya madhabahu na kuteketeza juu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
13 So the Priest shall make an atonement for him, as touching his sinne that he hath committed in one of these poyntes, and it shall bee forgiuen him: and the remnant shalbe the Priests, as the meate offring.
Kuhani atafanya upatanisho kwa dhambi yoyote aliyofanya mtu yeyote, mtu huyo atasamehewa. Na sadaka inayobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyo sadaka ya nafaka.'”
14 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Musa, akasema,
15 If any person transgresse and sinne through ignorance by taking away things consecrated vnto the Lord, hee shall then bring for his trespasse offring vnto the Lord a ramme without blemish out of the flocke, worth two shekels of siluer by thy estimation after the shekel of the Sanctuarie, for a trespasse offring.
“Kama mtu akikiuka amri na kufanya dhambi kinyume na mambo matakatifu ya Bwana, lakini akifanya bila kukusudia ataleta sadaka ya hatia kwa Bwana. Sadaka hii itakuwa ni kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi; thamani yake halisi kifedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kama sadaka ya hatia.
16 So hee shall restore that wherein hee hath offended, in taking away of the holy thing, and shall put the fift part more thereto, and giue it vnto the Priest: so the Priest shall make an atonement for him with the ram of ye trespasse offring, and it shalbe forgiuen him.
Lazima atalipa kwa Bwana kwa kile alichokosa kulingana na kitakatifu, na ataongezea moja ya tano na kumpa kuhani. Ndipo kuhani ataweka upatanisho kwa ajili yake pamoja na kondoo wa sadaka ya hatia, na mtu atakuwa amesamehewa.
17 Also if any sinne and doe against any of the commandements of the Lord, which ought not to be done, and knowe not and sinne and beare his iniquitie,
Kama mtu akitenda dhambi kwa kufanya kile ambacho Bwana aliagiza kisifanyike, hata kama hakujuwa, atakuwa na hatia na ataibeba hatia yake.
18 Then shall he bring a ramme without blemishe out of the flocke, in thy estimation worth two shekels for a trespasse offring vnto ye Priest: and the Priest shall make an atonement for him concerning his ignorance wherein he erred, and was not ware: so it shalbe forgiuen him.
Lazima ataleta kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi, anayestahili thamani ya fedha, kama sadaka ya hatia kwa kuhani. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kulingana na dhambi aliyotenda, ambayo hakujua atakuwa amesamehewa.
19 This is the trespasse offring for the trespasse committed against the Lord.
Ni sadaka ya hatia, na amekuwa na hatia mbele za Bwana.”

< Leviticus 5 >