< Leviticus 4 >

1 Moreouer the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Speake vnto the children of Israel, saying, If any shall sinne through ignorance, in any of the commandementes of the Lord, (which ought not to be done) but shall doe contrary to any of them,
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
3 If the Priest that is anointed doe sinne (according to the sinne of the people) then shall he offer, for his sinne which hee hath sinned, a yong bullocke without blemish vnto the Lord for a sinne offring,
“‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
4 And hee shall bring the bullocke vnto the dore of the Tabernacle of the Congregation before the Lord, and shall put his hande vpon the bullocks head, and kill the bullocke before the Lord.
Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
5 And the Priest that is anointed shall take of the bullocks blood, and bring it into the Tabernacle of the Congregation.
Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
6 Then the Priest shall dippe his finger in the blood, and sprinkle of the blood seuen times before the Lord, before the vaile of the Sanctuarie.
Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
7 The Priest also shall put some of the blood before the Lord, vpon the hornes of the altar of sweete incense, which is in the Tabernacle of the Congregation, then shall hee powre all the rest of the blood of the bullocke at the foote of the altar of burnt offring, which is at the doore of the Tabernacle of the Congregation.
Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 And hee shall take away all the fat of the bullocke for the sinne offring: to wit, the fat that couereth the inwardes, and all the fatte that is about the inwardes.
Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
9 He shall take away also the two kidneis, and the fat that is vpon them, and vpon the flankes, and the kall vpon the liuer with the kidneis,
figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
10 As it was taken away from the bullock of the peace offrings, and the Priest shall burne them vpon the altar of burnt offring.
kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
11 But the skinne of the bullocke, and all his flesh, with his heade, and his legs, and his inwardes, and his dung shall he beare out.
Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
12 So he shall cary the whole bullocke out of the host vnto a cleane place, where the ashes are powred, and shall burne him on ye wood in the fire: where ye ashes are cast out, shall he be burnt.
yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
13 And if the whole Congregation of Israel shall sinne through ignorance, and the thing be hid from the eyes of the multitude, and haue done against any of the commandements of the Lord which should not be done, and haue offended:
“‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
14 When the sinne which they haue committed shalbe knowen, then the Congregation shall offer a yong bullocke for the sinne, and bring him before the Tabernacle of the Congregation,
Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
15 And the Elders of the Congregation shall put their handes vpon the head of the bullocke before the Lord, and he shall kill the bullocke before the Lord.
Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
16 Then the Priest that is anointed, shall bring of the bullockes blood into the Tabernacle of the Congregation,
Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
17 And the Priest shall dip his finger in the blood, and sprinkle it seuen times before the Lord, euen before the vaile.
Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
18 Also he shall put some of ye blood vpon the hornes of the altar, which is before the Lord, that is in the Tabernacle of the Congregation: then shall he powre all the rest, of the blood at ye foote of the altar of burnt offring, which is at the doore of the Tabernacle of the Congregation,
Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
19 And he shall take all his fat from him, and burne it vpon the altar.
Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
20 And the Priest shall doe with this bullocke, as he did with the bullocke for his sinne: so shall he do with this: so the Priest shall make an atonement for them, and it shalbe forgiuen them.
naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
21 For he shall carie the bullocke without the hoste, and burne him as he burned the first bullock: for it is an offring for the sinne of the Congregation.
Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
22 When a ruler shall sinne, and do through ignorance against any of the commandements of the Lord his God, which should not be done, and shall offend,
“‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
23 If one shewe vnto him his sinne, which he hath committed, the shall he bring for his offring an hee goat without blemish,
Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
24 And shall lay his hand vpon the heade of the he goate, and kill it in the place where he should kill the burnt offring before the Lord: for it is a sinne offring.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
25 Then the Priest shall take of the blood of the sinne offring with his finger, and put it vpon the hornes of the burnt offring altar, and shall powre the rest of his blood at the foote of the burnt offring altar,
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
26 And shall burne all his fat vpon the altar, as the fat of the peace offring: so the Priest shall make an atonement for him, concerning his sinne, and it shalbe forgiuen him.
Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
27 Likewise if any of the people of ye lande shall sinne through ignoraunce in doing against any of the commandements of the Lord, which should not be done, and shall offend,
“‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
28 If one shewe him his sinne which he hath committed, then he shall bring for his offring, a shee goate without blemish for his sinne which he hath committed,
Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
29 And he shall lay his hand vpon the head of the sinne offring, and slay the sinne offring in the place of burnt offring.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
30 Then the Priest shall take of the blood thereof with his finger, and put it vpon the hornes of the burnt offring altar, and powre all the rest of the blood thereof at the foote of the altar,
Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
31 And shall take away all his fat, as the fat of the peace offringes is taken away, and the Priest shall burne it vpon the altar for a sweete sauour vnto the Lord, and the Priest shall make an atonement for him, and it shalbe forgiuen him.
Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
32 And if he bring a lambe for his sinne offring, he shall bring a female without blemish,
“‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
33 And shall lay his hand vpon the head of the sinne offring, and hee shall slay it for a sinne offring in the place where hee shoulde kill the burnt offring.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
34 Then the Priest shall take of the blood of the sinne offring with his finger, and put it vpon the hornes of the burnt offring altar, and shall powre al the rest of the blood thereof at the foote of the altar.
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
35 And he shall take away all the fat thereof, as the fatte of the lambe of the peace offrings is taken away: then the Priest shall burne it vpon the altar with the oblations of the Lord made by fire, and the Priest shall make an atonement for him concerning his sinne that he hath committed, and it shalbe forgiuen him.
Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.

< Leviticus 4 >