< Leviticus 18 >

1 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, I am the Lord your God.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 After ye doings of the land of Egypt, wherin ye dwelt, shall ye not doe: and after the maner of the land of Canaan, whither I will bring you, shall ye not do, neither walke in their ordinances,
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 But do after my iudgements, and keepe mine ordinances, to walke therein: I am the Lord your God.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 Ye shall keepe therefore my statutes, and my iudgements, which if a man doe, he shall then liue in them: I am the Lord.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 None shall come neere to any of ye kinred of his flesh to vncouer her shame: I am the Lord.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 Thou shalt not vncouer the shame of thy father, nor the shame of thy mother: for she is thy mother, thou shalt not discouer her shame.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 The shame of thy fathers wife shalt thou not discouer: for it is thy fathers shame.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 Thou shalt not discouer the shame of thy sister the daughter of thy father, or the daughter of thy mother, whether shee bee borne at home, or borne without: thou shalt not discouer their shame.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 The shame of thy sonnes daughter, or of thy daughters daughter, thou shalt not, I say, vncouer their shame: for it is thy shame.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 The shame of thy fathers wiues daughter, begotten of thy father (for she is thy sister) thou shalt not, I say, discouer her shame.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Thou shalt not vncouer the shame of thy fathers sister: for she is thy fathers kinswoman.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Thou shalt not discouer the shame of thy mothers sister: for she is thy mothers kinsewoman.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Thou shalt not vncouer the shame of thy fathers brother: that is, thou shalt not goe in to his wife, for she is thine aunte.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Thou shalt not discouer the shame of thy daughter in lawe: for she is thy sonnes wife: therefore shalt thou not vncouer her shame.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 Thou shalt not discouer the shame of thy brothers wife. for it is thy brothers shame.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 Thou shalt not discouer the shame of the wife and of her daughter, neither shalt thou take her sonnes daughter, nor her daughters daughter, to vncouer her shame: for they are thy kinsfolkes, and it were wickednesse.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Also thou shalt not take a wife with her sister, during her life, to vexe her, in vncouering her shame vpon her.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 Thou shalt not also go vnto a woman to vncouer her shame, as long as she is put apart for her disease.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 Moreouer, thou shalt not giue thy selfe to thy neighbours wife by carnall copulation, to be defiled with her.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 Also thou shalt not giue thy children to offer them vnto Molech, neither shalt thou defile the name of thy God: for I am the Lord.
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 Thou shalt not lie with ye male as one lieth with a woman: for it is abomination.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 Thou shalt not also lie with any beast to bee defiled therewith, neither shall any woman stand before a beast, to lie downe thereto: for it is abomination.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Yee shall not defile your selues in any of these things: for in al these the nations are defiled, which I will cast out before you:
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 And the land is defiled: therefore I wil visit the wickednesse thereof vpon it, and the lande shall vomit out her inhabitants.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 Ye shall keepe therefore mine ordinances, and my iudgements, and commit none of these abominations, aswell hee that is of the same countrey, as the straunger that soiourneth among you.
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 (For all these abominations haue the men of the land done, which were before you, and the land is defiled:
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 And shall not the lande spue you out if ye defile it, as it spued out the people that were before you?)
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 For whosoeuer shall commit any of these abominations, the persons that doe so, shall bee cut off from among their people.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Therefore shall yee keepe mine ordinances that ye do not any of the abominable customes, which haue bene done before you, and that yee defile not your selues therein: for I am the Lord your God.
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< Leviticus 18 >