< Leviticus 15 >

1 Moreouer the Lord spake vnto Moses, and to Aaron, saying,
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, Whosoeuer hath an issue from his flesh, is vncleane, because of his issue.
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 And this shalbe his vncleannes in his issue: when his flesh auoydeth his issue, or if his flesh be stopped from his issue, this is his vncleannes.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 Euery bed whereon he lyeth that hath the issue, shall be vncleane, and euery thing whereon he sitteth, shalbe vncleane.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 Whosoeuer also toucheth his bed, shall wash his clothes, and wash himselfe in water, and shall be vncleane vntill the euen.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 And he that sitteth on any thing, whereon he sate that hath the issue, shall wash his clothes, and wash himselfe in water, and shalbe vncleane vntill the euen.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 Also he that toucheth the flesh of him that hath the issue, shall wash his clothes, and wash himselfe in water, and shalbe vncleane vntil the euen.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 If he also, that hath the issue, spit vpon him that is cleane, he shall wash his clothes, and wash himselfe in water, and shalbe vncleane vntill the euen.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 And what saddle soeuer he rideth vpon, that hath the issue, shalbe vncleane,
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 And whosoeuer toucheth any thing that was vnder him, shall be vncleane vnto the euen: and he that beareth those things, shall wash his clothes, and wash himselfe in water, and shall be vncleane vntill the euen.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 Likewise whomesoeuer hee toucheth that hath the issue (and hath not washed his handes in water) shall wash his clothes and wash himselfe in water, and shalbe vncleane vntill the euen.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 And the vessel of earth that he toucheth, which hath the issue, shalbe broken: and euery vessel of wood shalbe rinsed in water.
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 But if he that hath an issue, be cleansed of his issue, then shall he count him seuen dayes for his cleansing, and wash his clothes, and wash his flesh in pure water: so shall he be cleane.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 Then the eight day he shall take vnto him two Turtle doues or two yong pigeons, and come before the Lord at the doore of the Tabernacle of the Congregation, and shall giue them vnto the Priest.
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 And the Priest shall make of the one of them a sinne offring, and of the other a burnt offering: so the Priest shall make an atonement for him before the Lord, for his issue.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 Also if any mans issue of seede depart from him, he shall wash all his flesh in water, and be vncleane vntill the euen.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 And euery garment, and euery skinne whereupon shalbe issue of seede, shall be euen washed with water, and be vncleane vnto the euen.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 If he that hath an issue of seede, do lie with a woman, they shall both wash themselues with water, and be vncleane vntill the euen.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 Also when a woman shall haue an issue, and her issue in her flesh shalbe blood, she shalbe put apart seuen dayes: and whosoeuer toucheth her, shalbe vncleane vnto the euen.
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 And whatsoeuer she lieth vpon in her separation, shalbe vncleane, and euery thing that she sitteth vpon, shalbe vncleane.
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 Whosoeuer also toucheth her bedde, shall wash his clothes, and wash himselfe with water, and shalbe vncleane vnto the euen.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 And whosoeuer toucheth any thing that she sate vpon, shall wash his clothes, and wash him selfe in water, and shalbe vncleane vnto the euen:
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
23 So that whether he touche her bed, or any thing whereon shee hath sit, he shalbe vncleane vnto the euen.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 And if a man lye with her, and the flowers of her separation touch him, he shalbe vncleane seuen dayes, and all the whole bed whereon he lieth, shalbe vncleane.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 Also when a womans issue of blood runneth long time besides the time of her floures, or when she hath an issue, longer then her floures, all the dayes of the issue of her vncleannesse shee shalbe vncleane, as in the time of her floures.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 Euery bed whereon shee lyeth (as long as her issue lasteth) shalbe to her as her bed of her separation: and whatsoeuer she sitteth vpon, shalbe vncleane, as her vncleannes whe she is put apart.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 And whosoeuer toucheth these things, shall be vncleane, and shall wash his clothes, and wash him selfe in water, and shalbe vncleane vnto the euen.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 But if she be clensed of her issue, then shee shall count her seuen dayes, and after, shee shall be cleane.
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 And in the eight day shee shall take vnto her two Turtles or two yong pigeons, and bring them vnto the Priest at the doore of the Tabernacle of the Congregation.
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 And the Priest shall make of ye one a sinne offring, and of the other a burnt offring, and the Priest shall make an atonement for her before the Lord, for the issue of her vncleannes.
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 Thus shall yee separate the children of Israel from their vncleannes, that they dye not in their vncleannesse, if they defile my Tabernacle that is among them.
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 This is the lawe of him that hath an issue, and of him from whome goeth an issue of seede whereby he is defiled:
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 Also of her that is sicke of her floures, and of him that hath a running issue, whether it bee man or woman, and of him that lyeth with her which is vncleane.
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.

< Leviticus 15 >