< Judges 6 >

1 Afterwarde the children of Israel committed wickednesse in the sight of the Lord, and the Lord gaue them into the handes of Midian seuen yeres.
Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
2 And the hand of Midian preuayled against Israel, and because of the Midianites the children of Israel made them dennes in the mountaines, and caues, and strong holdes.
Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
3 When Israel had sowen, then came vp the Midianites, the Amalekites, and they of the East, and came vpon them,
Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
4 And camped by them, and destroyed the fruite of the earth, euen til thou come vnto Azzah, and left no foode for Israel, neither sheepe, nor oxe, nor asse.
Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
5 For they went vp, and their cattel, and came with their tentes as grashoppers in multitude: so that they and their camels were without number: and they came into the land to destroy it.
Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
6 So was Israel exceedingly impouerished by the Midianites: therefore the children of Israel cryed vnto the Lord.
Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
7 And when the children of Israel cryed vnto the Lord because of the Midianites,
Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
8 The Lord sent vnto the children of Israel a Prophet, who sayd vuto them, Thus sayth the Lord God of Israel, I haue brought you vp from Egypt, and haue brought you out of the house of bondage,
Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
9 And I haue deliuered you out of the hand of the Egyptians, and out of the hand of all that oppressed you, and haue cast them out before you, and giuen you their land.
Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
10 And I sayde vnto you, I am the Lord your God: feare not the gods of the Amorites in whose lande you dwell: but ye haue not obeyed my voyce.
Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
11 And the Angell of the Lord came, and sate vnder the oke which was in Ophrah, that perteined vnto Ioash the father of the Ezrites, and his sonne Gideon threshed wheate by the winepresse, to hide it from the Midianites.
Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
12 Then the Angel of the Lord appeared vnto him, and said vnto him, The Lord is with thee, thou valiant man.
Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
13 To whome Gideon answered, Ah my Lord, if the Lord be with vs, why then is all this come vpon vs? and where be all his miracles which our fathers tolde vs of, and sayd, Did not the Lord bring vs out of Egypt? but now the Lord hath forsaken vs, and deliuered vs into the hand of the Midianites.
Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
14 And the Lord looked vpon him, and sayd, Goe in this thy might, and thou shalt saue Israel out of the handes of the Midianites: haue not I sent thee?
Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
15 And he answered him, Ah my Lord, whereby shall I saue Israel? beholde, my father is poore in Manasseh, and I am the least in my fathers house.
Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
16 Then the Lord sayd vnto him, I wil therefore be with thee, and thou shalt smite the Midianites, as one man.
Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
17 And he answered him, I pray thee, if I haue founde fauour in thy sight, then shewe me a signe, that thou talkest with me.
Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
18 Depart not hence, I pray thee, vntil I come vnto thee, and bring mine offring, and lay it before thee. And he sayde, I will tary vntill thou come againe.
Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
19 Then Gideon went in, and made ready a kidde, and vnleauened bread of an Ephah of floure, and put the flesh in a basket, and put the broth in a pot, and brought it out vnto him vnder the oke, and presented it.
Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
20 And the Angell of God saide vnto him, Take the flesh and the vnleauened bread, and lay them vpon this stone, and powre out the broth: and he did so.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Then the Angell of the Lord put forth the ende of the staffe that he had in his hand, and touched the flesh and the vnleauened bread: and there arose vp fire out of the stone, and consumed the flesh and the vnleauened bread: so the Angel of the Lord departed out of his sight.
Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
22 And when Gideon perceiued that it was an Angel of the Lord, Gideon then sayde, Alas, my Lord God: for because I haue seene an Angell of the Lord face to face, I shall die.
Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 And the Lord said vnto him, Peace be vnto thee: feare not, thou shalt not die.
Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
24 Then Gideon made an altar there vnto the Lord, and called it, Iehouah shalom: vnto this day it is in Ophrah, of the father of the Ezrites.
Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
25 And the same night the Lord sayd vnto him, Take thy fathers yong bullocke, and an other bullocke of seuen yeeres olde, and destroy the altar of Baal that thy father hath, and cut downe the groue that is by it,
Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
26 And build an altar vnto the Lord thy God vpon the top of this rocke, in a plaine place: and take the seconde bullocke, and offer a burnt offringe with the woode of the groue, which thou shalt cut downe.
Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
27 Then Gideon tooke tenne men of his seruants, and did as ye Lord bade him: but because he feared to doe it by day for his fathers housholde, and the men of the citie, he did it by night.
Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
28 And when the men of the citie arose early in the morning, beholde, the altar of Baal was broken, and the groue cut downe that was by it, and the seconde bullocke offred vpon the altar that was made.
Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
29 Therefore they saide one to another, Who hath done this thing? and when they inquired and asked, they saide, Gideon the sonne of Ioash hath done this thing.
Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
30 Then the men of the citie said vnto Ioash, Bring out thy sonne, that hee may dye: for he hath destroyed the altar of Baal, and hath also cut downe the groue that was by it.
Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
31 And Ioash said vnto all that stood by him, Will ye pleade Baals cause? or will ye saue him? he that will contend for him, let him dye or the morning. If he be God, let him pleade for himselfe against him that hath cast downe his altar.
Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
32 And in that day was Gideon called Ierubbaal, that is, Let Baal pleade for himselfe because he hath broken downe his altar.
Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
33 Then all the Midianites and the Amalekites and they of ye East, were gathered together, aud went and pitched in the valley of Izreel.
Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
34 But the Spirit of the Lord came vpon Gideon, and he blew a trumpet, and Abiezer was ioyned with him.
Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
35 And he sent messengers thorowout al Manasseh, which also was ioyned with him, and he sent messengers vnto Asher, and to Zebulun and to Naphtali, and they came vp to meete them.
Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
36 Then Gideon said vnto God, If thou wilt saue Israel by mine hand, as thou hast sayd,
Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
37 Beholde, I wil put a fleece of wooll in the threshing place: if the dewe come on the fleece onely, and it be drie vpon all the earth, then shall I be sure, that thou wilt saue Israel by mine hand, as thou hast said.
tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
38 And so it was: for he rose vp earely on the morow, and thrust the fleece together, and wringed the dew out of the fleece, and filled a bowle of water.
Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
39 Againe, Gideon sayde vnto God, Be not angry with me, that I may speake once more: let me prooue once againe, I pray thee, with the fleece: let it now be drie onely vpon the fleece, and let dewe be vpon all the ground.
Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
40 And God did so that same night: for it was drie vpon the fleece onely, and there was dewe on all the ground.
Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.

< Judges 6 >