< Judges 20 >

1 Then all the children of Israel went out, and the Congregation was gathered together as one man, from Dan to Beersheba, with the land of Gilead, vnto the Lord in Mizpeh.
Ndipo watu wote wa Israeli wakatoka kama mtu mmoja, toka Dani mpaka Beer-sheba, pamoja na nchi ya Gileadi; nao wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 And the chiefe of all the people, and all the tribes of Israel assembled in the Congregation of the people of God foure hundreth thousand footemen that drewe sword.
Viongozi wa watu wote, wa kabila zote za Israeli, wakachukua nafasi zao kwenye kusanyiko la watu wa Mungu-watu 400, 000 waendao kwa miguu, ambao walikuwa tayari kupigana na upanga.
3 (Now the children of Beniamin heard that the children of Israel were gone vp to Mizpeh) Then the children of Israel saide, Howe is this wickednesse committed?
Basi wana wa Benyamini waliposikia kwamba watu wa Israeli walikuwa wamepanda Mispa. Wana wa Israeli wakasema, “Tuambieni ni kwa namna gani huu uovu umefanyika.”
4 And the same Leuite, the womans husband that was slaine, answered and saide, I came vnto Gibeah that is in Beniamin with my concubine to lodge,
Mlawi, mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu, Nilikuja Gibea katika nchi ya Benyamini, mimi na suria wangu, ili tulale.
5 And the men of Gibeah arose against me, and beset the house round about vpon mee by night, thinking to haue slaine me, and haue forced my concubine that she is dead.
Wakati wa usiku, viongozi wa Gibea walinishambulia, wakizunguka nyumba na wakakusudia kuniua. Walimkamata na kumbaka suria wangu, naye akafa.
6 Then I tooke my concubine, and cut her in pieces, and sent her throughout all the countrey of the inheritance of Israel: for they haue committed abomination and villenie in Israel.
Nilimchukua suria wangu na kumkata mwili wake vipande vipande, na kuweka katika kila nchi ya urithi wa Israeli, kwa sababu wamefanya uovu huo na upumbavu katika Israeli.
7 Behold, ye are al children of Israel: giue your aduise, and counsell herein.
Sasa, ninyi Waisraeli wote, toeni maneno na ushauri wenu hapa.”
8 Then all the people arose as one man, saying, There shall not a man of vs goe to his tent, neither any turne into his house.
Watu wote wakaondoka pamoja kama mtu mmoja, wakasema, Hakuna hata mmoja wetu atakayeenda hemani kwake, wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 But now this is that thing which we will do to Gibeah: we wil goe vp by lot against it,
Lakini sasa hivi ndivyo tutakavyoifanyia Gibea tutaishambulia kama kura inavyotuongoza.
10 And we wil take ten men of the hundreth throughout al the tribes of Israel, and an hundreth of the thousand, and a thousand of ten thousand to bring vitaile for the people that they may do (when they come to Gibeah of Beniamin) according to all the villeny, that it hath done in Israel.
Tutachukua watu kumi katika mia moja katika makabila yote ya Israeli, na mia moja katika elfu, na elfu moja katika elfu kumi, kuwapa chakula kwa ajili ya watu hawa, ili waweze kufika Gibea katika Benyamini, watawaadhibu kwa uovu wao waliofanya katika Israeli.
11 So all the men of Israel were gathered against the citie, knit together, as one man.
Basi askari wote wa Israeli wakakusanyika juu ya mji, kama mtu mmoja.
12 And the tribes of Israel sent men through al the tribe of Beniamin, saying, What wickednesse is this that is committed among you?
Makabila ya Israeli waliwatuma watu kwa kabila lote la Benyamini, wakisema, “Uovu huu uliofanywa kati yenu ni nini?
13 Nowe therefore deliuer vs those wicked men which are in Gibeah, that we may put them to death, and put away euill from Israel: but the children of Beniamin would not obey the voyce of their brethren the children of Israel.
Kwa hiyo, tupeni watu hao waovu wa Gibea, tupate kuwaua, na hivyo tutaondoa kabisa uovu huu kutoka kwa Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakusikiliza sauti ya ndugu zao, watu wa Israeli,
14 But ye children of Beniamin gathered them selues together out of the cities vnto Gibeah, to come out and fight against the children of Israel.
Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika kutoka mijini kwenda Gibea, wakajiandaa kupigana na wana wa Israeli.
15 And ye children of Beniamin were nombred at that time out of the cities sixe and twenty thousand men that drewe sworde, beside the inhabitants of Gibeah, which were nombred seuen hundreth chosen men.
Watu wa Benyamini wakakusanya kutoka miji yao ili kupigana siku ile, askari elfu ishirini na sita waliopangwa kupigana na upanga. Walakini, kuna watu mia saba waliochaguliwa kutoka kwa wenyeji wa Gibea.
16 Of all this people were seuen hundreth chosen men, being left handed: all these could sling stones at an heare breadth, and not faile.
Miongoni mwa askari wote hawa walikuwa watu mia saba waliochaguliwa ambao walikuwa wenye shoto. Kila mmoja wao angeweza kupiga unywele kwa mawe na asikose.
17 Also the men of Israel, beside Beniamin, were nombred foure hundreth thousande men that drew sword, euen all men of warre.
Watu wa Israeli, bila kuhesabu namba kutoka kwa Benyamini, walikuwa na watu 400, 000 waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga. Wote hawa walikuwa watu wa vita.
18 And the children of Israel arose, and went vp to the house of God, and asked of God, saying, Which of vs shall goe vp first to fight against the children of Beniamin? And the Lord said, Iudah shalbe first.
Watu wa Israeli waliondoka, wakaenda Betheli, wakaomba ushauri kutoka kwa Mungu. Wakauliza, “Ni nani kwanza atakayewaangamiza watu wa Benyamini kwa ajili yetu?” Bwana akasema, “Yuda atashambulia kwanza.”
19 Then the children of Israel arose vp earely and camped against Gibeah.
Watu wa Israeli waliamka asubuhi na wakahamisha kambi yao karibu na Gibea.
20 And the men of Israel went out to battell against Beniamin, and the men of Israel put themselues in aray to fight against the beside Gibeah.
Watu wa Israeli walikwenda kupigana na Benyamini. Wakaweka nafasi zao za vita dhidi yao huko Gibea.
21 And the children of Beniamin came out of Gibeah, and slewe downe to the ground of the Israelites that day two and twentie thousand men.
Watu wa Benyamini wakatoka Gibea, nao wakawaua watu elfu ishirini na mbili wa jeshi la Israeli siku ile.
22 And the people, the men of Israel plucked vp their hearts, and set their battel againe in aray in the place where they put them in aray the first day.
Wana wa Israeli walijitia nguvu wenyewe, na wakaunda mstari wa vita mahali pale walipokwisha kuchukua nafasi siku ya kwanza.
23 (For the children of Israel had gone vp and wept before the Lord vnto the euening, and had asked of the Lord, saying, Shall I goe againe to battel against the children of Beniamin my brethren? and the Lord said, Go vp against them)
Na wana wa Israeli wakaenda, wakalia mbele za Bwana hata jioni. Walitaka mwongozo kutoka kwa Bwana “Je, tunapaswa kwenda tena kupigana na ndugu zetu, watu wa Benyamini?” Naye Bwana akasema, “Wapigeni!”
24 Then the children of Israel came neere against the children of Beniamin the second day.
Basi watu wa Israeli wakapigana na askari wa Benyamini siku ya pili.
25 Also the second day Beniamin came forth to meete them out of Gibeah, and slewe downe to the grounde of the children of Israel againe eighteene thousand men: all they could handle the sword.
Siku ya pili, Benyamini alitoka kupigana nao kutoka Gibea, nao wakawaua watu wa Israeli elfu kumi na nane. Wote walikuwa watu ambao walijifunza kupigana na upanga.
26 Then al the children of Israel went vp and all the people came also vnto the house of God, and wept and sate there before the Lord and fasted that day vnto the euening, and offred burnt offrings and peace offrings before the Lord.
Basi askari wote wa Israeli na watu wote wakaenda Betheli, wakalia, wakakaa mbele za Bwana; nao wakafunga siku hiyo hata jioni, wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
27 And the children of Israel asked the Lord (for there was the Arke of the couenat of God in those dayes,
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana, - kwa sababu ya sanduku la agano la Mungu lilikuwapo siku hizo;
28 And Phinehas the sonne of Eleazar, the sonne of Aaron stoode before it at that time) saying, Shall I yet goe anie more to battel against the children of Beniamin my brethren, or shall I cease? And the Lord said, Go vp: for to morowe I will deliuer them into your hand.
na Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, aliyekuwa akihudumia mbele ya sanduku siku hizo. “Je twende vitani tena dhidi ya watu wa Benyamini, ndugu zetu, au tuache?” Bwana akasema, “Wapigeni, kwa maana kesho nitawasaidia kuwashinda.
29 And Israel set men to lie in waite round about Gibeah.
Basi Israeli akaweka watu mahali pa siri karibu na Gibea.
30 And the children of Israel went vp against the children of Beniamin the third day, and put theselues in aray against Gibeah, as at other times.
Watu wa Israeli wakapigana na wana wa Benyamini kwa siku ya tatu, nao wakajenga vita vyao juu ya Gibea, kama walivyotangulia.
31 Then the children of Beniamin comming out against the people, were drawen from the citie: and they began to smite of ye people and kill as at other times, euen by the wayes in the fielde (whereof one goeth vp to the house of God, and the other to Gibeah) vpon a thirtie men of Israel.
Watu wa Benyamini wakaenda kupigana na watu, nao wakachukuliwa mbali na mji. Walianza kuua baadhi ya watu. Kulikuwa na watu thelathini wa Israeli ambao walikufa katika mashamba na barabara. Njia moja ilienda Betheli, na nyingine ikaenda Gibea.
32 (For the children of Beniamin sayd, They are fallen before vs, as at the first. But the children of Israel saide, Let vs flee and plucke them away from the citie vnto the hie wayes)
Ndipo wana wa Benyamini wakasema, “Wameshindwa na wanatukimbia, kama hapo awali.” Lakini askari wa Israeli wakasema, “Hebu tukimbie na kuwavuta mbali na mji hadi barabarani.”
33 And all the men of Israel rose vp out of their place, and put themselues in aray at Baal-tamar: and the men that lay in wayte of the Israelites came forth of their place, euen out of the medowes of Gibeah,
Watu wote wa Israeli waliondoka kutoka mahali pao na wakajipanga kwa vita huko Baal-Tamari. Basi askari wa Israeli waliokuwa wakijificha mahali pa siri walikimbia kutoka Maare-Geba.
34 And they came ouer against Gibeah, ten thousande chosen men of all Israel, and the battell was sore: for they knewe not that the euill was neere them.
Wakatoka juu ya Gibea watu kumi elfu waliochaguliwa kutoka Israeli yote, na vita vilikuwa kali, lakini Wabenjamini hawakujua kwamba msiba ulikuwa karibu nao.
35 And the Lord smote Beniamin before Israel, and the children of Israel destroyed of the Beniamites the same day fiue and twenty thousand and an hundreth men: all they could handle the sword.
Bwana akamshinda Benyamini mbele ya Israeli. Siku hiyo, askari wa Israeli waliwauawa watu wa Benyamini 25, 100. Wote hawa waliokufa walikuwa wale waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga.
36 So the children of Beniamin sawe that they were striken downe: for the men of Israel gaue place to the Beniamites, because they trusted to the men that lay in waite, which they had laide beside Gibeah.
Basi askari wa Benyamini waliona wameshindwa. Wana wa Israeli walikuwa wametoa ardhi kwa Benyamini, kwa kuwa walikuwa wakihesabu watu waliowaweka katika nafasi zilizofichwa nje ya Gibea.
37 And they that lay in wait hasted, and brake forth toward Gibeah, and the ambushment drewe themselues along, and smote all the citie with the edge of the sword.
Ndipo watu waliokuwa wameficha wakainuka na haraka na wakamkimbia Gibea. Nao wakauawa kila mtu aliyeishi mjini kwa upanga wao.
38 Also the men of Israel had appoynted a certaine time with the ambushmentes, that they should make a great flame and smoke rise vp out of the citie.
Ishara iliyopangwa kati ya askari wa Israeli na watu waliojificha kwa siri itakuwa wingu kubwa la moshi litatokea nje ya mji.
39 And when the men of Israel retired in the battel, Beniamin began to smite and kill of the men of Israel about thirtie persons: for they said, Surely they are striken downe before vs, as in the first battell.
Ishara ilipokuja askari wa Israeli wakageuka kutoka kwenye vita. Basi Benyamini wakaanza kushambulia na wakawaua watu wa Israeli thelathini, wakasema, “Hakika wanapigwa mbele yetu, kama katika vita vya kwanza.”
40 But when the flame bega to arise out of the citie, as a pillar of smoke, the Beniamites looked backe, and behold, the flame of the citie began to ascend vp to heauen.
Lakini wakati nguzo ya moshi ilipoanza kuinuka nje ya mji, Wabenjamini waligeuka na kuona moshi ukitanda mbinguni kutoka mji mzima.
41 Then the men of Israel turned againe, and the men of Beniamin were astonied: for they saw that euill was neere vnto them.
Ndipo watu wa Israeli wakawageuka. Wana wa Benyamini waliogopa, kwa sababu waliona kwamba maafa yaliwajia.
42 Therefore they fled before the men of Israel vnto the way of the wildernesse, but the battell ouertooke them: also they which came out of the cities, slew them among them.
Basi wakakimbia kutoka kwa wana wa Israeli, kuelekea njia ya jangwani. Lakini vita viliwapata. Askari wa Israeli walitoka mijini na wakawaua pale waliposimama.
43 Thus they compassed the Beniamites about, and chased them at ease, and ouerranne them, euen ouer against Gibeah on the Eastside.
Waliwalzungukia wana wa Benjamini na wakawafuata. Nao wakawakanyaga huko Noha, wakawaua mpaka upande wa mashariki wa Gibea.
44 And there were slaine of Beniamin eyghteene thousad men, which were all men of warre.
Kutoka kabila la Benyamini, watu kumi na nane elfu walikufa, wote walikuwa wanaume waliojulikana katika vita.
45 And they turned and fled to the wildernes vnto the rocke of Rimmon: and the Israelites glayned of them by the way fiue thousand men, and pursued after them vnto Gidom, and slewe two thousand men of them,
Wakageuka na kukimbia kuelekea jangwani hadi mwamba wa Rimoni. Waisraeli waliuawa zaidi ya elfu tano kati yao barabarani. Waliendelea kuwafuata, wakifuata kwa njia kuu kwenda Gidomu, na huko waliuawa elfu mbili zaidi.
46 So that all that were slayne that day of Beniamin, were fiue and twentie thousand men that drewe sword, which were all men of warre:
Askari wote wa Benyamini walioshuka siku hiyo walikuwa watu ishirini na tano waliokuwa wamejifunza kupigana kwa upanga; wote walikuwa wanajulikana katika vita.
47 But sixe hundreth men turned and fled to the wildernesse vnto the rocke of Rimmon, and abode in the rocke of Rimmon foure moneths.
Lakini watu mia sita wakageuka na kukimbilia jangwani, kuelekea mwamba wa Rimoni. Wakakaa katika mwamba wa Rimoni kwa muda wa miezi minne.
48 Then the men of Israel returned vnto the children of Beniamin, and smote them with the edge of the sword from the men of the citie vnto the beasts, and all that came to hand: also they set on fire all the cities that they coulde come by.
Askari wa Israeli waliwarudia watu wa Benyamini na wakawashinda na kuwaua-mji mzima, ng'ombe, na kila kitu walichopata. Pia walichoma moto kila mji katika njia yao.

< Judges 20 >