< Judges 1 >

1 After that Ioshua was dead, the children of Israel asked ye Lord, saying, Who shall goe vp for vs against the Canaanites, to fight first against them?
Baada ya kifo cha Yoshua, wana wa Israeli walimuuliza Yahweh wakisema, “Ni nani atawashambulia kwanza Wakanaani kwa ajili yetu, ili kupigana nao?
2 And the Lord said, Iudah shall goe vp: behold, I haue giuen the land into his hande.
Yahweh akasema, “Yuda atawashambulia. Tazama, nimewapa kumiliki nchi hii.
3 And Iudah said vnto Simeon his brother, Come vp with me into my lot, that we may fight against the Canaanites: and I likewise will goe with thee into thy lot: so Simeon went with him.
Watu wa Yuda wakawaambia wana wa Simeoni, ndugu zao, “Njoo pamoja nasi katika eneo letu ambalo tumepewa ili kwa pamoja tupigane na Wakanaani. Na sisi pia tutakwenda nanyi katika eneo mlilopewa.” Basi kabila la Simeoni wakaenda pamoja nao.
4 Then Iudah went vp, and the Lord deliuered the Canaanites and the Perizzites into their hands, and they slew of them in Bezek ten thousand men.
Watu wa Yuda wakashinda, na Bwana akawapa ushindi juu ya Wakanaani na Waperizi. Wakawaua watu elfu kumi huko Bezeki.
5 And they founde Adoni-bezek in Bezek: and they fought against him, and slewe the Canaanites, and the Perizzites.
Wakamkuta Adoni Bezeki huko Bezeki, nao wakapigana naye na kuwashinda Wakanaani na Waperizi.
6 But Adoni-bezek fled, and they pursued after him, and caught him, and cut off the thumbes of his hands and of his feete.
Lakini Adoni Bezeki akamkimbilia, wakamfuata na kumshika, nao wakavikata vidole gumba na vidole vyake vikubwa.
7 And Adoni-bezek said, Seuentie Kings hauing the thumbes of their hands and of their feete cut off, gathered bread vnder my table: as I haue done, so God hath rewarded me. so they brought him to Ierusalem, and there he died.
Adoni Bezek akasema, “Wafalme sabini, ambao na vidole gumba vyako na vidole vikubwa vilivyokatwa, walikusanya chakula chao chini ya meza yangu. Kama nilivyofanya, hata hivyo Mungu amefanya kwangu.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
8 (Nowe the children of Iudah had fought against Ierusalem, and had taken it and smitten it with the edge of the sworde, and had set the citie on fire.)
Watu wa Yuda wakapigana dhidi ya jiji la Yerusalemu na kulichukua. Walishambulia kwa makali ya upanga na wakauwasha mji kwa moto.
9 Afterwarde also the children of Iudah went downe to fight against the Canaanites, that dwelt in the mountaine, and towarde the South, and in the lowe countrey.
Baada ya hayo, watu wa Yuda walikwenda kupigana na Wakanaani waliokaa mlimani, Negebu, na magharibi mwa milima.
10 And Iudah went against the Canaanites that dwelt in Hebron, which Hebron beforetime was called Kiriath-arba: and they slewe Sheshai, and Ahiman and Talmai.
Yuda akaenda dhidi ya Wakanaani waliokaa Hebroni (jina la Hebroni hapo awali ilikuwa Kiriath-arba), nao wakamshinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
11 And from thence hee went to the inhabitantes of Debir, and the name of Debir in olde time was Kiriath-sepher.
Kutoka huko watu wa Yuda walipigana na wenyeji wa Debiri (jina la Debiri hapo awali ilikuwa Kiriath-seferi).
12 And Caleb saide, He that smiteth Kiriath-sepher, and taketh it, euen to him wil I giue Achsah my daughter to wife.
Kalebu akasema, Yeyote atakayeivamia Kiriath-seferi na kuichukua, nitampa Aksa, binti yangu, awe mkewe.
13 And Othniel the sonne of Kenaz Calebs yonger brother tooke it, to whome hee gaue Achsah his daughter to wife.
Otinieli, mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, akaiteka Debiri, naye Kalebu akampa Aksa, binti yake, awe mkewe.
14 And when shee came to him, shee mooued him to aske of her father a field, and shee lighted off her asse, and Caleb saide vnto her, What wilt thou?
Ndipo Aksa alifika kwa Othnieli, naye akamsihi amuombe baba yake ampe shamba. Alipokuwa akishuka katika punda wake, Kalebu akamwuliza, “Nikufanyie nini?”
15 And shee answered him, Giue mee a blessing: for thou hast giuen me a South countrey, giue me also springs of water: and Caleb gaue her the springs aboue and the springs beneath.
Akamwambia, Nibariki. Kwa kuwa umenipa nchi ya Negebu, nipe pia chemchemi za maji. Kwa hiyo Kalebu akampa chemchemi za juu na chemchemi za chini.
16 And the childre of Keni Moses father in law went vp out of the citie of the palme trees with the children of Iudah, into the wildernesse of Iudah, that lieth in the South of Arad, and went and dwelt among the people.
Kizazi cha Mkeeni shemeji yake na Musa, walikwenda kutoka mji wa Mitende pamoja na watu wa Yuda, mpaka jangwa la Yuda, ambalo liko Negevu, kuishi na watu wa Yuda karibu na Arad.
17 But Iudah went with Simeon his brother, and they slewe the Canaanites that inhabited Zephath, and vtterly destroied it, and called the name of the citie Hormah.
Nao watu wa Yuda wakaenda pamoja na wana wa Simeoni ndugu zao, wakawaangamiza Wakanaani waliokaa Zefathi, wakaiharibu kabisa. Mji uliitwa Horma.
18 Also Iudah tooke Azzah with the coasts thereof, and Askelon with the coasts thereof, and Ekron with the coastes thereof.
Watu wa Yuda pia waliiteka Gaza na nchi iliyoizunguka, Ashkeloni na nchi iliyoizunguka, na Ekron na nchi iliyoizunguka.
19 And the Lord was with Iudah, and he possessed the mountaines: for he could not driue out the inhabitantes of the valleis, because they had charrets of yron.
Yahweh alikuwa pamoja na watu wa Yuda na wakaimiliki nchi ya milima, lakini hawakuweza kuwatoa wenyeji wa kwenye bonde kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
20 And they gaue Hebron vnto Caleb, as Moses had saide, and hee expelled thence the three sonnes of Anak.
Hebroni alipewa Kalebu (kama Musa alivyosema), naye akawafukuza kutoka huko wana watatu wa Anaki.
21 But the children of Beniamin did not cast out the Iebusites, that inhabited Ierusalem: therefore the Iebusites dwell with the children of Beniamin in Ierusalem vnto this day.
Lakini wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu. Basi Wayebusi wakakaa na watu wa Benyamini huko Yerusalemu hata leo.
22 They also that were of the house of Ioseph, went vp to Beth-el, and the Lord was with them,
Nyumba ya Yusufu ilijiandaa kuishambulia Betheli, na Yahweh alikuwa pamoja nao.
23 And the house of Ioseph caused to viewe Beth-el (and the name of the citie beforetime was Luz)
Walipeleka watu kuipeleleza Betheli (jiji lililoitwa Luzu).
24 And the spies sawe a man come out of the citie, and they saide vnto him, Shewe vs, we praie thee, the way into the citie, and we will shewe thee mercie.
Wapelelezi waliona mtu akitoka nje ya jiji, wakamwambia, “Tafadhali tuonyeshe jinsi ya kuingia ndani ya jiji, na tutakutendea mema.”
25 And when hee had shewed them the waie into the citie, they smote the citie with the edge of the sworde, but they let the man and all his housholde depart.
Aliwaonyesha njia ya kuingia kwenye mji. Waliuteka mji kwa makali ya upanga, lakini wakamuacha mtu huyo na ndugu zake wote waondoke.
26 Then the man went into the lande of the Hittites, and built a citie, and called the name thereof Luz, which is the name thereof vnto this daie.
Na mtu huyo akaenda nchi ya Wahiti, akajenga mji, akauita Luzu, ambalo jina lake hata leo.
27 Neither did Manasseh destroie Bethshean with her townes, nor Taanach with her townes, nor the inhabitantes of Dor with her townes, nor the inhabitants of Ibleam with her townes, neither the inhabitants of Megiddo with her townes: but the Canaanites dwelled still in that lande.
Watu wa Manase hawakuwafukuza watu waliokuwa katika miji ya Bethsheani na vijiji vyake, au Taanaki na vijiji vyake, au wale waliokaa Dori na vijiji vyake, wala wale waliokaa Ibleamu na vijiji vyake, wala walioshi Megido na vijiji vyake, kwa sababu Wakanaani walikuwa wameamua kuishi katika nchi hiyo.
28 Neuerthelesse when Israel was strong, they put the Canaanites to tribute, and expelled them not wholly.
Israeli ipokuwa na nguvu, waliwalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu, lakini hawakuwafukuza kabisa.
29 Likewise Ephraim expelled not the Canaanites that dwelt in Gezer, but the Canaanites dwelt in Gezer among them.
Efraimu hakuwafukuza Wakanaani waliokaa Gezeri; kwa hiyo Wakanaani wakakaa kati yao.
30 Neither did Zebulun expell the inhabitants of Kitron, nor the inhabitants of Nahalol, but the Canaanites dwelt among them, and became tributaries.
Zebuloni hakuwafukuza watu wa Kitroni, wala watu waliokuwa Nahaloli; na Wakanaani wakaendelea kuishi pamoja nao; lakini Zabuloni akawalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu.
31 Neither did Asher cast out the inhabitants of Accho, nor the inhabitants of Zidon, nor of Ahlab, nor of Achzib, nor of Helbah, nor of Aphik, nor of Rehob,
Asheri hakuwafukuza watu wanaoishi Aka, au watu wanaoishi Sidoni, au wale wanaoishi Alabu, Akzib, Helba, Afeka, au Rehobu.
32 But the Asherites dwelt among the Canaanites the inhabitantes of the lande: for they did not driue them out.
Kwa hiyo kabila ya Asheri iliishi kati ya Wakanaani (waliokaa katika nchi hiyo), kwa sababu hawakuwafukuza.
33 Neither did Naphtali driue out the inhabitants of Beth-shemesh, nor the inhabitants of Beth-anath, but dwelt among the Canaanites the inhabitants of the lande: neuerthelesse the inhabitantes of Beth-shemesh, and of Beth-anath became tributaries vnto them.
Na kabila la Naftali halikuwafukuza watu waliokuwa wakiishi Bethshemeshi, wala waliokuwa wakiishi Bethanathi. Kwa hiyo kabila la Naftali liliishi kati ya Wakanaani (watu waliokuwa wakiishi katika nchi hiyo). Hata hivyo, wenyeji wa Bethshemeshi na Bethanathi walilazimishwa kufanya kazi ngumu kwa Naphthali.
34 And the Amorites droue the children of Dan into the mountaine: so that they suffered them not to come downe to the valley.
Waamori waliwalazimisha kabila la Dani kuishi katika nchi ya kilima, hawakuwaruhusu kuja bondeni.
35 And the Ammonites dwelt still in mount Heres in Aijalon, and in Shaalbim, and when the hand of Iosephs familie preuailed, they became tributaries:
Basi Waamori waliishi katika mlima wa Heresi, huko Aiyaloni, na Shaalbimu, lakini nguvu za kijeshi za nyumba ya Yusufu ziliwashinda, nao wakalazimishwa kuwatumikia kwa kazi ngumu.
36 And the coast of the Amorites was from Maaleh-akrabbim, euen from Selah and vpward.
Mpaka wa Waamori ulikuwa kutoka kilima cha Akrabimu huko Sela hadi nchi ya vilima.

< Judges 1 >