< Joshua 13 >

1 Nowe when Ioshua was olde, and striken in yeeres, the Lord said vnto him, Thou art olde and growen in age, and there remaineth exceeding much land to be possessed:
Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
2 This is the land that remaineth, all the regions of the Philistims, and all Geshuri,
Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
3 From Nilus which is in Egypt, euen vnto the borders of Ekron Northward: this is counted of the Canaanites, euen fiue Lordships of the Philistims, the Azzithites, and the Ashdodites, the Eshkelonites, the Gittites, and the Ekronites, and the Auites:
(tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
4 From the South, all the land of the Canaanites, and the caue that is beside the Sidonians, vnto Aphek, and to the borders of the Amorites:
Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
5 And the land of the Giblites, and all Lebanon, toward the sunne rising from Bahal-gad vnder mount Hermon, vntil one come to Hamath.
nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
6 All the inhabitants of the mountaines from Lebanon vnto Misrephothmaim, and all the Sidonians, I wil cast them out from before the children of Israel: only deuide thou it by lot vnto the Israelites, to inherite, as I haue commanded thee.
Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
7 Nowe therefore deuide this lande to inherite, vnto the nine tribes, and to the halfe tribe of Manasseh.
Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
8 For with halfe therof the Reubenites and the Gadites haue receiued their inheritance, which Moses gaue them beyond Iorden Eastward, euen as Moses the seruant of the Lord had giuen them,
Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
9 From Aroer that is on the brinke of the riuer Arnon, and from the citie that is in the mids of the riuer, and all the plaine of Medeba vnto Dibon,
kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
10 And all the cities of Sihon King of the Amorites, which reigned in Heshbon, vnto the borders of the children of Ammon,
miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
11 And Gilead, and the borders of the Geshurites and of the Maachathites, and all mount Hermon, with all Bashan vnto Salcah:
Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
12 All the kingdome of Og in Bashan, which reigned in Ashtaroth and in Edrei: (who remained of the rest of the gyants) for these did Moses smite, and cast them out.
ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
13 But the children of Israel expelled not the Geshurites nor the Maachathites: but the Geshurites and the Maachathites dwell among the Israelites euen vnto this day.
Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
14 Onely vnto the tribe of Leui he gaue none inheritance, but the sacrifices of the Lord God of Israel are his inheritance, as he said vnto him.
Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
15 Moses then gaue vnto the tribe of the children of Reuben inheritance, according to their families.
Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
16 And their coast was from Aroer, that is on the brinke of the riuer Arnon, and from the citie that is in the middes of the riuer, and all the plaine which is by Medeba:
Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
17 Heshbon with all the cities thereof, that are in the plaine: Dibon and Bamoth-baal, and Bethbaal-meon:
Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
18 And Iahazah, and Kedemoth and Mephaath:
na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
19 Kiriathaim also, and Sibmah, and Zerethshahar in the mount of Emek:
na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
20 And Beth-peor, and Ashdoth-pisgah, and Beth-ieshimoth:
Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
21 And all the cities of the plaine: and all the kingdome of Sihon King of the Amorites, which reigned in Heshbon, whome Moses smote with the Princes of Midian, Eui, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the dukes of Sihon, dwelling in the countrey.
miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
22 And Balaam the sonne of Beor the soothsayer did the children of Israel slay with the sword, among them that were slaine.
Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
23 And the border of the children of Reuben was Iorden with the coastes. This was the inheritance of the children of Reuben according to their families, with the cities and their villages.
Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
24 Also Moses gaue inheritance vnto ye tribe of Gad, euen vnto the children of Gad according to their families.
Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 And their coastes were Iazer, and all the cities of Gilead and halfe the lande of the children of Ammon vnto Aroer, which is before Rabbah:
Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
26 And from Heshbon vnto Ramoth, Mizpeh, and Betonim: and from Mahanaim vnto the borders of Debir:
kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
27 And in the valley Beth-aram, and Bethnimrah, and Succoth, and Zaphon, the rest of the kingdome of Sihon King of Heshbon, vnto Iorden and the borders euen vnto the Sea coast of Cinneereth, beyond Iorden Eastward.
Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
28 This is the inheritance of the children of Gad, after their families, with the cities, and their villages.
Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
29 Also Moses gaue inheritance vnto the halfe tribe of Manasseh: and this belonged to the halfe tribe of the children of Manasseh according to their families.
Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
30 And their border was from Mahanaim, euen all Bashan, to wit, all the kingdome of Og King of Bashan, and all the townes of Iair which are in Bashan, threescore cities,
Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
31 And halfe Gilead, and Ashtaroth, and Edrei, cities of the kingdom of Og in Bashan, were giuen vnto the children of Machir the sonne of Manasseh, to halfe of the children of Machir after their families.
nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
32 These are the heritages, which Moses did distribute in the plaine of Moab beyond Iorden, toward Iericho Eastward.
Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 But vnto the tribe of Leui Moses gaue none inheritance: for the Lord God of Israel is their inheritance, as he said vnto them.
Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.

< Joshua 13 >