< Jonah 2 >

1 Then Ionah prayed vnto the Lord his God out of the fishes belly,
Kisha Yona akamwomba Bwana Mungu wake kutoka katika tumbo la samaki.
2 And said, I cryed in mine affliction vnto the Lord, and he heard me: out of the bellie of hell cryed I, and thou heardest my voyce. (Sheol h7585)
Akasema, Nimemwita Bwana juu ya shida yangu naye akanijibu; kutoka tumbo la Kuzimu nililia kwa msaada! Uliisikia sauti yangu. (Sheol h7585)
3 For thou haddest cast me into the bottome in the middes of the sea, and the floods compassed me about: all thy surges, and all thy waues passed ouer me.
Ulikuwa umenitupa ndani ya kina, ndani ya moyo wa bahari, na maji yaliyonizunguka; mawimbi yako yote na gharika yalipita juu yangu.
4 Then I saide, I am cast away out of thy sight: yet will I looke againe towarde thine holy Temple.
Nikasema, 'Nimefukuzwa mbele ya macho yako; lakini nitaangalia tena juu ya hekalu lako takatifu. '
5 The waters compassed me about vnto the soule: the depth closed me rounde about, and the weedes were wrapt about mine head.
Maji yalifunika kunizunguka karibu na shingo yangu; kina kilinizunguka; mwani ukakizinga kichwa changu.
6 I went downe to the bottome of the moutaines: the earth with her barres was about me for euer, yet hast thou brought vp my life from the pit, O Lord my God.
Nilikwenda chini ya milima; nchi na baa zake zimefungwa juu yangu milele. Lakini wewe umeinua uhai wangu shimoni, Bwana, Mungu wangu!
7 When my soule fainted within me, I remembred the Lord: and my prayer came vnto thee, into thine holy Temple.
Wakati nafsi yangu ilipozimia ndani yangu, nikamwita Bwana; basi sala yangu ilikujia, katika hekalu lako takatifu.
8 They that waite vpon lying vanities, forsake their owne mercie.
Wote ambao huzingatia miungu isiyofaa hukataa uaminifu wako wao wenyewe.
9 But I will sacrifice vnto thee with the voice of thankesgiuing, and will pay that that I haue vowed: saluation is of the Lord.
Lakini mimi, nitakuchinjia kwa sauti ya shukrani; Nitayatimiza yale niliyoapa. Wokovu hutoka kwa Bwana!
10 And the Lord spake vnto the fish, and it cast out Ionah vpon the dry lande.
Kisha Bwana akanena na samaki, akamtapika Yona juu ya nchi kavu.

< Jonah 2 >