< Job 40 >

1 Moreouer ye Lord spake vnto Iob, and said,
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Is this to learne to striue with the Almightie? he that reprooueth God, let him answere to it.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then Iob answered the Lord, saying,
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Beholde, I am vile: what shall I answere thee? I will lay mine hand vpon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once haue I spoken, but I will answere no more, yea twise, but I will proceede no further.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Againe the Lord answered Iob out of the whirle winde, and said,
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Girde vp now thy loynes like a man: I will demaunde of thee, and declare thou vnto me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou disanul my iudgement? or wilt thou condemne me, that thou mayst be iustified?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Or hast thou an arme like God? or doest thou thunder with a voyce like him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Decke thy selfe now with maiestie and excellencie, and aray thy selfe with beautie and glory.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Cast abroad the indignation of thy wrath, and beholde euery one that is proude, and abase him.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Looke on euery one that is arrogant, and bring him lowe: and destroy the wicked in their place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together, and binde their faces in a secret place.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then will I confesse vnto thee also, that thy right hand can saue thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Behold now Behemoth (whom I made with thee) which eateth grasse as an oxe.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Behold now, his strength is in his loynes, and his force is in the nauil of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 When hee taketh pleasure, his taile is like a cedar: the sinews of his stones are wrapt together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are like staues of brasse, and his small bones like staues of yron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the chiefe of the wayes of God: he that made him, will make his sworde to approch vnto him.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Surely the mountaines bring him foorth grasse, where all the beastes of the fielde play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Lyeth hee vnder the trees in the couert of the reede and fennes?
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Can the trees couer him with their shadow? or can the willowes of the riuer compasse him about?
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, he spoyleth the riuer, and hasteth not: he trusteth that he can draw vp Iorden into his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Hee taketh it with his eyes, and thrusteth his nose through whatsoeuer meeteth him.
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >