< Job 28 >

1 The siluer surely hath his veyne, and ye gold his place, where they take it.
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
2 Yron is taken out of the dust, and brasse is molten out of the stone.
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
3 God putteth an end to darkenesse, and he tryeth the perfection of all things: he setteth a bond of darkenesse, and of the shadowe of death.
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
4 The flood breaketh out against the inhabitant, and the waters forgotten of the foote, being higher then man, are gone away.
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
5 Out of the same earth commeth bread, and vnder it, as it were fire is turned vp.
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
6 The stones thereof are a place of saphirs, and the dust of it is golde.
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
7 There is a path which no foule hath knowen, neyther hath the kites eye seene it.
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
8 The lyons whelpes haue not walked it, nor the lyon passed thereby.
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
9 He putteth his hand vpon the rockes, and ouerthroweth the mountaines by the rootes.
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
10 He breaketh riuers in the rockes, and his eye seeth euery precious thing.
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
11 He bindeth the floods, that they doe not ouerflowe, and the thing that is hid, bringeth he to light.
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
12 But where is wisdome found? and where is the place of vnderstanding?
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
13 Man knoweth not the price thereof: for it is not found in the land of the liuing.
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
14 The depth sayth, It is not in mee: the sea also sayth, It is not with me.
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
15 Golde shall not be giuen for it, neyther shall siluer be weighed for the price thereof.
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
16 It shall not be valued with the wedge of golde of Ophir, nor with the precious onix, nor the saphir.
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
17 The golde nor the chrystall shall be equall vnto it, nor the exchange shalbe for plate of fine golde.
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
18 No mention shall be made of coral, nor of the gabish: for wisedome is more precious then pearles.
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
19 The Topaz of Ethiopia shall not be equall vnto it, neither shall it be valued with the wedge of pure gold.
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
20 Whence then commeth wisedome? and where is the place of vnderstanding,
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
21 Seeing it is hid from the eyes of all the liuing, and is hid from the foules of the heauen?
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
22 Destruction and death say, We haue heard the fame thereof with our eares.
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
23 But God vnderstandeth the way thereof, and he knoweth the place thereof.
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
24 For he beholdeth the endes of the world, and seeth all that is vnder heauen,
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
25 To make the weight of the windes, and to weigh the waters by measure.
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
26 When he made a decree for the rayne, and a way for the lightening of the thunders,
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
27 Then did he see it, and counted it: he prepared it and also considered it.
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
28 And vnto man he said, Behold, the feare of the Lord is wisedome, and to depart from euil is vnderstanding.
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”

< Job 28 >