< Job 10 >

1 My soule is cut off though I liue: I wil leaue my complaint vpon my selfe, and wil speake in the bitternesse of my soule.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 I will say vnto God, Condemne mee not: shew me, wherefore thou contendest with mee.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Thinkest thou it good to oppresse me, and to cast off the labour of thine handes, and to fauour the counsel of the wicked?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Hast thou carnall eyes? or doest thou see as man seeth?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Are thy dayes as mans dayes? or thy yeres, as the time of man,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 That thou inquirest of mine iniquitie, and searchest out my sinne?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 Thou knowest that I can not do wickedly: for none can deliuer me out of thine hand.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 Thine handes haue made me, and fashioned mee wholy rounde about, and wilt thou destroy me?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Remember, I pray thee, that thou hast made me as the clay, and wilt thou bring me into dust againe?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Hast thou not powred me out as milke? and turned me to cruds like cheese?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 Thou hast clothed me with skin and flesh, and ioyned me together with bones and sinewes.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 Thou hast giuen me life, and grace: and thy visitation hath preserued my spirit.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Though thou hast hid these things in thine heart, yet I knowe that it is so with thee.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 If I haue sinned, then thou wilt streightly looke vnto me, and wilt not holde mee giltlesse of mine iniquitie.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 If I haue done wickedly, wo vnto me: if I haue done righteously, I will not lift vp mine head, being full of confusion, because I see mine affliction.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 But let it increase: hunt thou me as a lyon: returne and shew thy selfe marueilous vpon me.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 Thou renuest thy plagues against me, and thou increasest thy wrath against me: changes and armies of sorowes are against me.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 Wherfore then hast thou brought me out of the wombe? Oh that I had perished, and that none eye had seene me!
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 And that I were as I had not bene, but brought from the wombe to the graue!
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Are not my dayes fewe? let him cease, and leaue off from me, that I may take a litle comfort,
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 Before I goe and shall not returne, euen to the land of darkenesse and shadow of death:
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 Into a land, I say, darke as darknes it selfe, and into the shadow of death, where is none order, but the light is there as darkenesse.
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >