< Jeremiah 49 >

1 Unto the children of Ammon thus saith the Lord, Hath Israel no sonnes? or hath he none heire? Why then hath their king possessed God? and his people dwelt in his cities?
Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
2 Therefore beholde the dayes come, sayeth the Lord, that I will cause a noyse of warre to be heard in Rabbah of the Ammonites, and it shall be a desolate heape, and her daughters shall be burnt with fire: then shall Israel possesse those that possessed him, sayeth the Lord.
Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
3 Howle, O Heshbon, for Ai is wasted: crie ye daughters of Rabbah: girde you with sackecloth: mourne and runne to and from by the hedges: for their King shall goe into captiuitie; and his Priestes, and his princes likewise.
Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
4 Wherefore gloriest thou in the valleis? thy valley floweth away, O rebellious daughter: she trusted in her treasures, saying, Who shall come vnto me?
Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
5 Beholde, I will bring a feare vpon thee, sayth the Lord God of hostes, of all those that be about thee, and ye shalbe scattered euery man right foorth, and none shall gather him that fleeth.
Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
6 And afterward I will bring againe the captiuitie of the children of Ammon.
Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
7 To Edom thus sayeth the Lord of hostes: Is wisdome no more in Teman? is counsel perished from their children? is their wisdome vanished?
Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
8 Flee, ye inhabitants of Dedan (they are turned backe, and haue consulted to dwell) for I haue brought the destruction of Esau vpon him, and the time of his visitation.
Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
9 If the grape gatherers come to thee, would they not leaue some grapes? if theeues come by night, they will destroy till they haue ynough.
Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
10 For I haue discouered Esau: I haue vncouered his secrets, and he shall not be able to hide himselfe: his seede is wasted, and his brethren and his neighbours, and there shall be none to say,
Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
11 Leaue thy fathers children, and I will preserue them aliue, and let thy widowes trust in me.
Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
12 For thus sayth the Lord, Beholde, they whose iudgement was not to drinke of the cuppe, haue assuredly drunken, and art thou he that shall escape free? thou shalt not goe free, but thou shalt surely drinke of it.
Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
13 For I haue sworne by my selfe, sayeth the Lord, that Bozrah shall be waste, and for a reproche, and a desolation, and a curse, and all the cities thereof shall be perpetuall desolations.
Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
14 I haue heard a rumour from the Lord, and an ambassadour is sent vnto the heathen, saying, Gather you together, and come against her, and rise vp to the battell.
Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
15 For loe, I will make thee but small among the heathen, and despised among men.
“Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
16 Thy feare, and ye pride of thine heart hath deceiued thee, thou that dwellest in the cleftes of the rocke, and keepest the height of ye hil: though thou shouldest make thy nest as hie as the eagle, I wil bring thee downe from thece, sayth the Lord.
Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
17 Also Edom shall be desolate: euery one that goeth by it, shall be astonished, and shall hisse at all the plagues thereof,
Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
18 As in the ouerthrowe of Sodom, and of Gomorah, and the places thereof neere about, saieth the Lord: no man shall dwell there, neither shall the sonnes of men remaine in it.
Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
19 Beholde, hee shall come vp like a lyon from the swelling of Iorden vnto the strong dwelling place: for I will make Israel to rest, euen I will make him to haste away from her, and who is a chosen man that I may appoynt against her? for who is like mee? and who will appoint me the time? and who is the shepheard that will stande before me?
Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
20 Therefore heare the counsell of the Lord that hee hath deuised against Edom, and his purpose that hee hath conceiued against the inhabitants of Teman: surely the least of the flocke shall drawe them out: surely he shall make their habitations desolate with them.
Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
21 The earth is mooued at the noyse of their fall: the crie of their voice is heard in the red Sea.
Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
22 Behold, he shall come vp, and flie as the Egle, and spreade his wings ouer Bozrah, and at that day shall the heart of the strong men of Edome be as the heart of a woman in trauaile.
Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
23 Vnto Damascus he sayeth, Hamath is confounded and Arpad, for they haue heard euill tidings, and they are faint hearted as one on the fearefull sea that can not rest.
Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
24 Damascus is discouraged, and turneth her selfe to flight and feare hath seased her: anguish and sorowes haue taken her as a woman in trauaile.
Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
25 How is the glorious citie not reserued, the citie of my ioy?
Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
26 Therefore her yong men shall fall in her streetes, and all her men of warre shall be cut off in that day, sayeth the Lord of hostes.
Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
27 And I will kindle a fire in the wall of Damascus, which shall cosume the palaces of Benhadad.
“Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
28 Vnto Kedar, and to the kingdomes of Hazor, which Nebuchad-nezzar, king of Babel shall smite, thus sayeth the Lord, Arise, and goe vp vnto Kedar, and destroy the men of the East.
Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
29 Their tents and their flocks shall they take away: yea, they shall take to themselues their curtaines and all their vessels, and their camels, and they shall crie vnto them, Feare is on euery side.
Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
30 Flee, get you farre off (they haue consulted to dwell) O ye inhabitants of Hazor, saith the Lord: for Nebuchad-nezzar King of Babel hath taken counsell against you, and hath deuised a purpose against you.
Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
31 Arise, and get you vp vnto the welthy nation that dwelleth without care, saith the Lord, which haue neither gates nor barres, but dwel alone.
Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
32 And their camels shall be a bootie, and the multitude of their cattel a spoile, and I will scatter them into all windes, and to the vtmost corners, and I will bring their destruction from al the sides thereof, sayeth the Lord.
Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
33 And Hazor shall be a dwelling for dragons, and desolation for euer: there shall no man dwell there, nor the sonnes of men remaine in it.
Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
34 The woordes of the Lord that came to Ieremiah the Prophet, concerning Elam, in the beginning of the reigne of Zedekiah King of Iudah, saying,
Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
35 Thus sayeth the Lord of hostes, Beholde, I will breake the bowe of Elam, euen the chiefe of their strength.
“Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
36 And vpon Elam I will bring the foure windes from the foure quarters of heauen, and will scatter them towardes all these windes, and there shall bee no nation, whither the fugitiues of Elam shall not come.
Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
37 For I will cause Elam to be afraied before their enemies, and before them that seeke their liues, and will bring vpon them a plague, euen the indignation of my wrath, saieth the Lord, and I wil sende the sworde after them till I haue consumed them.
Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
38 And I wil set my throne in Elam, and I wil destroy both the King and the princes from thence, saith the Lord:
Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
39 but in the latter daies I wil bring againe the captiuitie of Elam, sayeth the Lord.
na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”

< Jeremiah 49 >