< Jeremiah 13 >

1 Thus sayth the Lord vnto mee, Goe, and buy thee a linen girdle, and put it vpon thy loynes, and put it not in water.
Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
2 So I bought the girdle according to the commandement of the Lord, and put it vpon my loynes.
Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
3 And the worde of the Lord came vnto me the second time, saying,
Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
4 Take the girdle that thou hast bought, which is vpon thy loynes, and arise, goe towarde Perath, and hide it there in the cleft of the rocke.
“Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
5 So I went, and hid it by Perath, as the Lord had commanded me.
Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
6 And after many dayes, the Lord sayde vnto mee, Arise, goe towarde Perath, and take the girdle from thence, which I commanded thee to hide there.
Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
7 Then went I to Perath, and digged, and tooke the girdle from the place where I had hid it, and behold, the girdle was corrupt, and was profitable for nothing.
Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
8 Then the word of the Lord came vnto me, saying,
Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
9 Thus sayth the Lord, After this maner will I destroy the pride of Iudah, and the great pride of Ierusalem.
“Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
10 This wicked people haue refused to heare my word, and walke after ye stubbernesse of their owne heart, and walke after other gods to serue them, and to worship them: therefore they shalbe as this girdle, which is profitable to nothing.
Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
11 For as the girdle cleaueth to the loynes of a man, so haue I tied to me the whole house of Israel, and the whole house of Iudah, saith the Lord, that they might bee my people: that they might haue a name and prayse, and glory, but they would not heare.
Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
12 Therefore thou shalt saye vnto them this word, Thus sayth the Lord God of Israel, Euery bottell shalbe filled with wine, and they shall say vnto thee, Doe we not knowe that euery bottell shalbe filled with wine?
Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
13 Then shalt thou say vnto them, Thus saith the Lord, Behold, I will fill all the inhabitants of this land, euen the Kings that sit vpon the throne of Dauid, and the Priestes and the Prophets and all the inhabitantes of Ierusalem with drunkennesse.
Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
14 And I wil dash them one against another, euen the fathers and the sonnes together, sayeth the Lord: I will not spare, I will not pitie nor haue compassion, but destroy them.
Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
15 Heare and giue eare, be not proude: for the Lord hath spoken it.
Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
16 Giue glory to the Lord your God before he bring darknes, and or euer your feete stumble in the darke mountaines, and whiles you look for light, he turne it into the shadowe of death and make it as darkenesse.
Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
17 But if ye will not heare this, my soule shall weepe in secrete for your pride, and mine eye shall weepe and drop downe teares, because the Lords flocke is caried away captiue.
Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
18 Say vnto the King and to the Queene, Humble yourselues, sit downe, for the crowne of your glory shall come downe from your heads.
“Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
19 The cities of the South shall be shut vp, and no man shall open them: all Iudah shall be caried away captiue: it shall be wholy caried away captiue.
Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
20 Lift vp your eyes and beholde them that come from the North: where is the flocke that was giuen thee, euen thy beautifull flocke?
Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
21 What wilt thou saye, when hee shall visite thee? (for thou hast taught them to be captaines and as chiefe ouer thee) shall not sorow take thee as a woman in trauaile?
Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
22 And if thou say in thine heart, Wherefore come these things vpon me? For the multitude of thine iniquities are thy skirts discouered and thy heeles made bare.
Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
23 Can the blacke More change his skin? or the leopard his spots? then may ye also do good, that are accustomed to do euill.
Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
24 Therefore will I scatter them, as the stubble that is taken away with the South winde.
Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
25 This is thy portion, and ye part of thy measures from me, sayth the Lord, because thou hast forgotten me and trusted in lyes.
Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
26 Therefore I haue also discouered thy skirts vpon thy face, that thy shame may appeare.
Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
27 I haue seene thine adulteries, and thy neiings, the filthinesse of thy whoredome on the hils in the fieldes, and thine abominations. Wo vnto thee, O Ierusalem: wilt thou not bee made cleane? when shall it once be?
Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”

< Jeremiah 13 >