< Jeremiah 13 >

1 Thus sayth the Lord vnto mee, Goe, and buy thee a linen girdle, and put it vpon thy loynes, and put it not in water.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
2 So I bought the girdle according to the commandement of the Lord, and put it vpon my loynes.
Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
3 And the worde of the Lord came vnto me the second time, saying,
Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
4 Take the girdle that thou hast bought, which is vpon thy loynes, and arise, goe towarde Perath, and hide it there in the cleft of the rocke.
“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
5 So I went, and hid it by Perath, as the Lord had commanded me.
Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
6 And after many dayes, the Lord sayde vnto mee, Arise, goe towarde Perath, and take the girdle from thence, which I commanded thee to hide there.
Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
7 Then went I to Perath, and digged, and tooke the girdle from the place where I had hid it, and behold, the girdle was corrupt, and was profitable for nothing.
Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
8 Then the word of the Lord came vnto me, saying,
Ndipo neno la Bwana likanijia:
9 Thus sayth the Lord, After this maner will I destroy the pride of Iudah, and the great pride of Ierusalem.
“Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 This wicked people haue refused to heare my word, and walke after ye stubbernesse of their owne heart, and walke after other gods to serue them, and to worship them: therefore they shalbe as this girdle, which is profitable to nothing.
Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
11 For as the girdle cleaueth to the loynes of a man, so haue I tied to me the whole house of Israel, and the whole house of Iudah, saith the Lord, that they might bee my people: that they might haue a name and prayse, and glory, but they would not heare.
Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
12 Therefore thou shalt saye vnto them this word, Thus sayth the Lord God of Israel, Euery bottell shalbe filled with wine, and they shall say vnto thee, Doe we not knowe that euery bottell shalbe filled with wine?
“Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
13 Then shalt thou say vnto them, Thus saith the Lord, Behold, I will fill all the inhabitants of this land, euen the Kings that sit vpon the throne of Dauid, and the Priestes and the Prophets and all the inhabitantes of Ierusalem with drunkennesse.
Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
14 And I wil dash them one against another, euen the fathers and the sonnes together, sayeth the Lord: I will not spare, I will not pitie nor haue compassion, but destroy them.
Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
15 Heare and giue eare, be not proude: for the Lord hath spoken it.
Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
16 Giue glory to the Lord your God before he bring darknes, and or euer your feete stumble in the darke mountaines, and whiles you look for light, he turne it into the shadowe of death and make it as darkenesse.
Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
17 But if ye will not heare this, my soule shall weepe in secrete for your pride, and mine eye shall weepe and drop downe teares, because the Lords flocke is caried away captiue.
Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
18 Say vnto the King and to the Queene, Humble yourselues, sit downe, for the crowne of your glory shall come downe from your heads.
Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
19 The cities of the South shall be shut vp, and no man shall open them: all Iudah shall be caried away captiue: it shall be wholy caried away captiue.
Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
20 Lift vp your eyes and beholde them that come from the North: where is the flocke that was giuen thee, euen thy beautifull flocke?
Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
21 What wilt thou saye, when hee shall visite thee? (for thou hast taught them to be captaines and as chiefe ouer thee) shall not sorow take thee as a woman in trauaile?
Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
22 And if thou say in thine heart, Wherefore come these things vpon me? For the multitude of thine iniquities are thy skirts discouered and thy heeles made bare.
Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
23 Can the blacke More change his skin? or the leopard his spots? then may ye also do good, that are accustomed to do euill.
Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
24 Therefore will I scatter them, as the stubble that is taken away with the South winde.
“Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
25 This is thy portion, and ye part of thy measures from me, sayth the Lord, because thou hast forgotten me and trusted in lyes.
Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 Therefore I haue also discouered thy skirts vpon thy face, that thy shame may appeare.
Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
27 I haue seene thine adulteries, and thy neiings, the filthinesse of thy whoredome on the hils in the fieldes, and thine abominations. Wo vnto thee, O Ierusalem: wilt thou not bee made cleane? when shall it once be?
uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”

< Jeremiah 13 >