< Hosea 6 >

1 Come, and let vs returne to the Lord: for he hath spoyled, and he will heale vs: he hath wounded vs, and he will binde vs vp.
“Njoo, turudi kwa Bwana. Kwa maana ametuvunja vipande vipande, lakini atatuponya; ametujeruhi, lakini atatufunga majeraha yetu.
2 After two dayes will he reuiue vs, and in the third day he will raise vs vp, and we shall liue in his sight.
Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, na tutaishi mbele yake.
3 Then shall we haue knowledge, and indeuour our selues to know the Lord: his going forth is prepared as the morning, and he shall come vnto vs as the raine, and as the latter raine vnto the earth.
Nasi tumjue Bwana; tukaendelee kumjua Bwana. Kuja kwake ni hakika kama asubuhi; atakuja kwetu kama mvua, kama mvua ya vuli ambayo huinyeshea ardhi.”
4 O Ephraim, what shall I doe vnto thee? O Iudah, how shall I intreate thee? for your goodnesse is as a morning cloude, and as the morning dewe it goeth away.
Efuraimu, nikufanyie nini? Yuda, nikufanyie nini? Uaminifu wako ni kama wingu la asubuhi, kama umande unaoondoka mapema.
5 Therefore haue I cut downe by the Prophets: I haue slaine them by the wordes of my mouth, and thy iudgements were as the light that goeth forth.
Kwa hiyo nimewavunja vipande vipande kwa vinywa vya manabii, nimewaua kwa maneno ya kinywa changu. Maagizo yako ni kama nuru inayoangaza.
6 For I desired mercie, and not sacrifice, and the knowledge of God more then burnt offrings.
Kwa maana natamani uaminifu wala si dhabihu, na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 But they like men haue transgressed the couenant: there haue they trespassed against me.
Kama Adamu wamevunja agano; hawakuwa waaminifu kwangu.
8 Gilead is a citie of them that worke iniquitie, and is polluted with blood.
Gileadi ni jiji la wahalifu wenye miguu ya damu.
9 And as the eues waite for a man, so the companie of Priestes murder in the way by consent: for they worke mischiefe.
Kama makundi ya wanyang'anyi wanaomngojea mtu, hivyo makuhani hujiunga pamoja kufanya mauaji kwa njia ya Shekemu; wamefanya uhalifu wa aibu.
10 I haue seene vileny in the house of Israel: there is ye whoredome of Ephraim: Israel is defiled.
Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo baya; Uzinzi wa Efraimu ukopale, na Israeli ametiwa unajisi.
11 Yea, Iudah hath set a plant for thee, whiles I woulde returne ye captiuitie of my people.
Kwa maana wewe, Yuda, mavuno yameteuliwa, nitakaporudisha urithi wa watu wangu.

< Hosea 6 >