< Hebrews 3 >

1 Therefore, holy brethren, partakers of the heauenly vocation, consider the Apostle and high Priest of our profession Christ Iesus:
Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa wito wa mbinguni, mumfikiri Yesu, Mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
2 Who was faithfull to him that hath appointed him, euen as Moses was in al his house.
Alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua, kama Musa alivyokuwa mwaminifu pia katika nyumba yote ya Mungu.
3 For this man is counted worthy of more glory then Moses, inasmuch as he which hath builded the house, hath more honour then the house.
Kwa kuwa Yesu amehesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko aliyokuwa nayo Musa, kwa sababu yule anayejenga nyumba anahesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
4 For euery house is builded of some man, and he that hath built all things, is God.
Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule anayejenga kila kitu ni Mungu.
5 Now Moses verely was faithfull in all his house, as a seruant, for a witnesse of the thinges which should be spoken after.
Hakika Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu, akitoa ushuhuda kuhusu mambo yatakayosemwa wakati ujao.
6 But Christ is as the Sonne, ouer his owne house, whose house we are, if we holde fast that confidence and that reioycing of that hope vnto the ende.
Lakini Kristo ni Mwana katika usimamizi wa nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tutashikilia haraka katika kujiamini na fahari ya kujiamini.
7 Wherefore, as the holy Ghost sayth, To day if ye shall heare his voyce,
Kwa hiyo, ni kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, kama utasikia sauti yake,
8 Harden not your hearts, as in the prouocation, according to the day of the tentation in the wildernes,
Usiufanye moyo wako kuwa mgumu kama Waisraeli walivyofanya katika uasi, katika wakati wa kujaribiwa nyikani.
9 Where your fathers tempted me, prooued me, and sawe my workes fourtie yeeres long.
Huu ulikuwa wakati ambao baba zenu waliniasi kwa kunijaribu, na wakati, kwa miaka arobaini, waliona matendo yangu.
10 Wherefore I was grieued with that generation, and sayde, They erre euer in their heart, neither haue they knowen my wayes.
Kwa hiyo sikufurahishwa na kizazi hicho. Nilisema, 'Wanapotea kila mara katika mioyo yao, na hawajui njia zangu.
11 Therefore I sware in my wrath, If they shall enter into my rest.
Ni kama vile nilivyoapa katika hasira yangu: hawataiingia raha yangu.”
12 Take heede, brethren, least at any time there be in any of you an euill heart, and vnfaithfull, to depart away from the liuing God.
Muwe waangalifu, ndugu, ili kwamba usije ukawepo moyo mwovu wa kutokuamini kwa mmoja wenu, moyo ambao utakwenda mbali na Mungu aliye hai.
13 But exhort one another dayly, while it is called to day, lest any of you be hardened through the deceitfulnes of sinne.
Badala yake, mhamasishane kila siku kila mmoja na mwenzie, ili kila iitwapo leo mtamani, ili kwamba mmoja kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
14 For we are made partakers of Christ, if we keepe sure vnto the ende that beginning, wherewith we are vpholden,
Kwa maana tumekuwa washiriki wa Kristo ikiwa tutashikamana na uthabiti wetu kwa nguvu katika yeye kutoka mwanzo hadi mwisho.
15 So long as it is sayd, To day if ye heare his voyce, harden not your hearts, as in the prouocation.
Kuhusu hili imekwisha kusemwa, “Leo kama mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu, kama Waisraeli walivyofanya wakati wa uasi.”
16 For some when they heard, prouoked him to anger: howbeit, not all that came out of Egypt by Moses.
Ni akina nani hao waliomsikia Mungu na kuasi? Hawakuwa wale wote ambao Musa alikuwa amewaongoza kutoka Misri?
17 But with whome was he displeased fourtie yeeres? Was hee not displeased with them that sinned, whose carkeises fell in the wildernes?
Na kina nani ambao Mungu aliwakasirikia kwa miaka arobaini? Siyo pamoja na wale waliotenda dhambi, ambao miili yao iliyokufa ililala jangwani?
18 And to whom sware he that they should not enter into his rest, but vnto them that obeyed not?
Ni akina nani aliowaapia Mungu kwamba hawataingia katika raha yake, kama siyo wale ambao hawakumtii yeye?
19 So we see that they could not enter in, because of vnbeliefe.
Tunaona kwamba hawakuweza kuingia katika raha yake kwa sababu ya kutokuamini.

< Hebrews 3 >