< Hebrews 12 >

1 Wherefore, let vs also, seeing that we are compassed with so great a cloude of witnesses, cast away euery thing that presseth downe, and the sinne that hangeth so fast on: let vs runne with patience the race that is set before vs,
Kwa sababu hii, kwa kuwa tumezungukwa na wingu kubwa namna hii la mashahidi, basi na tuweke kando kila kitu kinachotuzuia na ile dhambi inayotuzinga kwa urahisi, nasi tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa kwa ajili yetu.
2 Looking vnto Iesus the authour and finisher of our faith, who for the ioy that was set before him, endured the crosse, and despised the shame, and is set at the right hand of the throne of God.
Basi na tumtazame sana Yesu mwanzilishi na mkamilishaji wa imani yetu, yeye ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake alistahimili msalaba, bila kujali aibu ya huo msalaba, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Consider therefore him that endured such speaking against of sinners, lest ye should be wearied and faint in your mindes.
Mtafakarini sana yeye aliyestahimili upinzani mkuu namna hii kutoka kwa watu wenye dhambi, ili kwamba msije mkachoka na kukata tamaa.
4 Ye haue not yet resisted vnto blood, striuing against sinne.
Katika kushindana kwenu dhidi ya dhambi, bado hamjapigana kiasi cha kumwaga damu yenu.
5 And ye haue forgotten the consolation, which speaketh vnto you as vnto children, My sonne, despise not the chastening of the Lord, neither faint when thou art rebuked of him.
Nanyi mmesahau yale maneno ya kuwaonya yanayowataja ninyi kuwa wana, yakisema: “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usikate tamaa akikukemea,
6 For whom the Lord loueth, he chasteneth: and he scourgeth euery sonne that he receiueth:
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, na humwadhibu kila mmoja anayemkubali kuwa mwana.”
7 If ye endure chastening, God offereth him selfe vnto you as vnto sonnes: for what sonne is it whom the father chasteneth not?
Vumilieni taabu kwa ajili ya kufunzwa adabu. Mungu anawatendea ninyi kama watoto wake, kwa maana ni mtoto yupi asiyeadibishwa na mzazi wake?
8 If therefore ye be without correction, whereof al are partakers, then are ye bastards, and not sonnes.
Kama hakuna kuadibishwa (ambalo ni fungu la watoto wote), basi ninyi ni watoto wa haramu wala si watoto halali.
9 Moreouer we haue had the fathers of our bodies which corrected vs, and we gaue them reuerence: should we not much rather be in subiection vnto the father of spirites, that we might liue?
Tena, sisi sote tunao baba wa kimwili, waliotuadibisha nasi tukawaheshimu kwa ajili ya hilo. Je, si inatupasa kujinyenyekeza zaidi kwa Baba wa roho zetu ili tuishi?
10 For they verely for a few dayes chastened vs after their owne pleasure: but he chasteneth vs for our profite, that we might be partakers of his holinesse.
Baba zetu walituadibisha kwa kitambo kidogo kama wao wenyewe walivyoona vyema, lakini Mungu hutuadibisha kwa faida yetu ili tupate kushiriki utakatifu wake.
11 Now no chastising for the present seemeth to be ioyous, but, grieuous: but afterwarde, it bringeth the quiet fruite of righteousnesse, vnto them which are thereby exercised.
Kuadibishwa wakati wowote hakuonekani kuwa kitu cha kufurahisha bali chenye maumivu kinapotekelezwa. Lakini baadaye huzaa matunda ya haki na amani kwa wale waliofunzwa nayo.
12 Wherfore lift vp your hands which hang downe, and your weake knees,
Kwa hiyo, itieni nguvu mikono yenu iliyo dhaifu na magoti yenu yaliyolegea.
13 And make straight steppes vnto your feete, lest that which is halting, be turned out of the way, but let it rather be healed.
Sawazisheni mapito ya miguu yenu, ili kitu kilicho kiwete kisidhoofishwe bali kiponywe.
14 Followe peace with all men, and holinesse, without the which no man shall see ye Lord.
Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo utakatifu, ambao bila kuwa nao hakuna mtu atakayemwona Bwana.
15 Take heede, that no man fall away from the grace of God: let no roote of bitternes spring vp and trouble you, lest thereby many be defiled.
Angalieni sana mtu yeyote asiikose neema ya Mungu na kwamba shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
16 Let there be no fornicator, or prophane person as Esau, which for one portion of meate solde his birthright.
Angalieni miongoni mwenu asiwepo mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, ambaye kwa ajili ya mlo mmoja aliuza haki ya uzaliwa wake wa kwanza.
17 For ye knowe howe that afterwarde also when he woulde haue inherited the blessing, he was reiected: for he founde no place to repentance, though he sought that blessing with teares.
Baadaye kama mnavyofahamu, alipotaka kurithi ile baraka, alikataliwa, maana hakupata nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
18 For ye are not come vnto the mount that might be touched, nor vnto burning fire, nor to blacknes and darkenes, and tempest,
Hamjaufikia mlima ule uwezao kuguswa na ambao unawaka moto; wala kwenye giza, utusitusi na dhoruba;
19 Neither vnto the sounde of a trumpet, and the voyce of wordes, which they that heard it, excused themselues, that the word should not be spoken to them any more,
kwenye mlio wa tarumbeta, au kwenye sauti isemayo maneno ya kutisha kiasi ambacho wale walioisikia waliomba wasiambiwe neno jingine zaidi,
20 (For they were not able to abide that which was commanded, yea, though a beast touche the mountaine, it shalbe stoned, or thrust through with a dart:
kwa sababu hawangeweza kustahimili neno lile lililoamriwa: “Hata kama mnyama atagusa mlima huu, atapigwa mawe.”
21 And so terrible was the sight which appeared, that Moses said, I feare and quake.)
Waliyoyaona yalikuwa ya kutisha kiasi kwamba Mose alisema, “Ninatetemeka kwa hofu.”
22 But ye are come vnto the mount Sion, and to the citie of the liuing God, the celestiall Hierusalem, and to ye company of innumerable Angels,
Lakini ninyi mmekuja Mlima Sayuni, Yerusalemu ya mbinguni, mji wa Mungu aliye hai. Mmekuja penye kusanyiko kubwa la malaika maelfu kwa maelfu wasiohesabika wanaoshangilia,
23 And to the assemblie and congregation of the first borne, which are written in heauen, and to God the iudge of all, and to the spirits of iust and perfite men,
kwenye kanisa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mmekuja kwa Mungu, mhukumu wa watu wote, kwenye roho za wenye haki waliokamilishwa,
24 And to Iesus the Mediatour of the new Testament, and to the blood of sprinkling that speaketh better things then that of Abel.
kwa Yesu mpatanishi wa agano jipya, na kwa damu iliyonyunyizwa, ile inenayo mambo mema kuliko damu ya Abeli.
25 See that ye despise not him that speaketh: for if they escaped not which refused him, that spake on earth: much more shall we not escape, if we turne away from him, that speaketh from heauen.
Angalieni, msije mkamkataa yeye anenaye. Ikiwa wao hawakuepuka adhabu walipomkataa yeye aliyewaonya hapa duniani, sisi je, tutaokokaje tusipomsikiliza yeye anayetuonya kutoka mbinguni?
26 Whose voyce then shooke the earth and nowe hath declared, saying, Yet once more will I shake, not the earth onely, but also heauen.
Wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ameahidi, “Kwa mara moja tena nitatetemesha si nchi tu bali na mbingu pia.”
27 And this worde, Yet once more, signifieth the remouing of those things which are shaken, as of things which are made with hands, that the things which are not shaken, may remaine.
Maneno haya “kwa mara moja tena” yanaonyesha kuondoshwa kwa vile vitu vinavyoweza kutetemeshwa, yaani vile vitu vilivyoumbwa, kwa kusudi vile tu visivyoweza kutetemeshwa vibaki.
28 Wherefore seeing we receiue a kingdome, which cannot be shaken, let vs haue grace whereby we may so serue God, that we may please him with reuerence and feare.
Kwa hiyo, kwa kuwa tunapokea ufalme ambao hauwezi kutetemeshwa, basi na tuwe na shukrani, na hivyo tumwabudu Mungu kwa namna inayompendeza, kwa unyenyekevu na uchaji,
29 For euen our God is a consuming fire.
kwa kuwa “Mungu wetu ni moto ulao.”

< Hebrews 12 >