< Hebrews 10 >

1 For the Law hauing the shadowe of good things to come, and not the very image of the things, can neuer with those sacrifices, which they offer yeere by yeere continually, sanctifie the commers thereunto.
Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2 For would they not then haue ceased to haue bene offered, because that the offerers once purged, should haue had no more conscience of sinnes?
Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3 But in those sacrifices there is a remembrance againe of sinnes euery yeere.
Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4 For it is vnpossible that the blood of bulles and goates should take away sinnes.
Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5 Wherefore when he commeth into the world, he saith, Sacrifice and offring thou wouldest not: but a body hast thou ordeined me.
Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: “Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6 In burnt offerings, and sinne offrings thou hast had no pleasure.
Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7 Then I sayd, Lo, I come (In the beginning of the booke it is written of me) that I should doe thy will, O God.
Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.”
8 Aboue, when he sayd, Sacrifice and offring, and burnt offrings, and sinne offrings thou wouldest not haue, neither hadst pleasure therein (which are offered by the Lawe)
Kwanza alisema: “Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi.” Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9 Then sayd he, Lo, I come to doe thy wil, O God, he taketh away the first, that he may stablish the second.
Kisha akasema: “Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako.” Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10 By the which wil we are sanctified, euen by the offring of the body of Iesus Christ once made.
Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11 And euery Priest standeth dayly ministring, and oft times offreth one maner of offring, which can neuer take away sinnes:
Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12 But this man after he had offered one sacrifice for sinnes, sitteth for euer at the right hand of God,
Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13 And from hencefoorth tarieth, till his enemies be made his footestoole.
Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14 For with one offering hath he consecrated for euer them that are sanctified.
Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15 For the holy Ghost also beareth vs record: for after that he had sayd before,
Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16 This is the Testament that I will make vnto them after those dayes, sayth the Lord, I wil put my Lawes in their heart, and in their mindes I will write them.
“Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao.”
17 And their sinnes and iniquities will I remember no more.
Kisha akaongeza kusema: “Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu.”
18 Nowe where remission of these things is, there is no more offering for sinne.
Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19 Seeing therefore, brethren, that by the blood of Iesus we may be bolde to enter into the Holy place,
Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20 By the newe and liuing way, which hee hath prepared for vs, through the vaile, that is, his flesh:
Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21 And seeing we haue an hie Priest, which is ouer the house of God,
Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22 Let vs drawe neere with a true heart in assurance of faith, our hearts being pure from an euill conscience,
Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23 And washed in our bodies with pure water, let vs keepe the profession of our hope, without wauering, (for he is faithfull that promised)
Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24 And let vs consider one another, to prouoke vnto loue, and to good workes,
Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25 Not forsaking the fellowship that we haue among our selues, as the maner of some is: but let vs exhort one another, and that so much the more, because ye see that the day draweth neere.
Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26 For if we sinne willingly after that we haue receiued and acknowledged that trueth, there remaineth no more sacrifice for sinnes,
Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27 But a fearefull looking for of iudgement, and violent fire, which shall deuoure the aduersaries.
Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28 He that despiseth Moses Law, dieth without mercy vnder two, or three witnesses:
Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 Of howe much sorer punishment suppose ye shall hee be worthy, which treadeth vnder foote the Sonne of God, and counteth the blood of the Testament as an vnholy thing, wherewith he was sanctified, and doeth despite the Spirit of grace?
Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30 For we know him that hath sayd, Vengeance belongeth vnto mee: I will recompense, saith the Lord. And againe, The Lord shall iudge his people.
Maana tunamfahamu yule aliyesema, “Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza,” na ambaye alisema pia, “Bwana atawahukumu watu wake.”
31 It is a fearefull thing to fall into the hands of the liuing God.
Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32 Nowe call to remembrance the dayes that are passed, in the which, after ye had receiued light, ye endured a great fight in afflictions,
Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33 Partly while yee were made a gazing stocke both by reproches and afflictions, and partly while ye became companions of them which were so tossed to and from.
Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34 For both ye sorowed with mee for my bonds, and suffered with ioy the spoyling of your goods, knowing in your selues howe that ye haue in heauen a better, and an enduring substance.
Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35 Cast not away therefore your confidence which hath great recompense of reward.
Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36 For ye haue neede of patience, that after ye haue done the will of God, ye might receiue the promise.
Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37 For yet a very litle while, and hee that shall come, will come, and will not tary.
Maana kama yasemavyo Maandiko: “Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38 Nowe the iust shall liue by faith: but if any withdrawe himselfe, my soule shall haue no pleasure in him.
Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye.”
39 But we are not they which withdrawe our selues vnto perdition, but follow faith vnto the conseruation of the soule.
Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.

< Hebrews 10 >