< Hebrews 10 >

1 For the Law hauing the shadowe of good things to come, and not the very image of the things, can neuer with those sacrifices, which they offer yeere by yeere continually, sanctifie the commers thereunto.
Kwa vile sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo, si yale yaliyo halisi. Sheria kamwe haiwezi kuwakamilisha wale ambao wanaomkaribia Mungu kwa njia ya dhabihu zilezile ambazo makuhani waliendelea kutoa mwaka baada ya mwaka.
2 For would they not then haue ceased to haue bene offered, because that the offerers once purged, should haue had no more conscience of sinnes?
Au vinginevyo dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa? Kwa kigezo hicho waabuduo, wakiwa wamesafishwa mara moja, wasingelikuwa na utambuzi zaidi wa dhambi.
3 But in those sacrifices there is a remembrance againe of sinnes euery yeere.
Bali katika dhabihu hizo kuna ukumbusho wa dhambi zilizotendwa mwaka baada ya mwaka.
4 For it is vnpossible that the blood of bulles and goates should take away sinnes.
Kwa kuwa haiwezekani kwa damu ya mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi.
5 Wherefore when he commeth into the world, he saith, Sacrifice and offring thou wouldest not: but a body hast thou ordeined me.
Wakati Kristo alipokuja duniani, alisema, “Hamkutamani matoleo au dhabihu, badala yake, mliandaa mwili kwa ajili yangu.
6 In burnt offerings, and sinne offrings thou hast had no pleasure.
Hamkuwa na thamani katika matoleo yote ya kuteketezwa au dhabihu kwa ajili ya dhambi.
7 Then I sayd, Lo, I come (In the beginning of the booke it is written of me) that I should doe thy will, O God.
Kisha nilisema, “Ona, hapa ninayafanya mapenzi yako, Mungu, kama ilivyoandikwa kunihusu mimi katika gombo”.
8 Aboue, when he sayd, Sacrifice and offring, and burnt offrings, and sinne offrings thou wouldest not haue, neither hadst pleasure therein (which are offered by the Lawe)
Alisema kama ilivyo semwa hapo juu: “Hamkutamani dhabihu, matoleo, au sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi, wala hukuona furaha ndani yake” dhabihu ambazo zinatolewa kulingana na sheria.
9 Then sayd he, Lo, I come to doe thy wil, O God, he taketh away the first, that he may stablish the second.
Kisha alisema, “Ona, niko hapa kufanya mapenzi yako”. Ameweka pembeni taratibu zilizo za awali ili kuimarisha zile za pili.
10 By the which wil we are sanctified, euen by the offring of the body of Iesus Christ once made.
Katika taratibu za pili, tumekwisha tengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake kupitia kujitoa kwa mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa nyakati zote.
11 And euery Priest standeth dayly ministring, and oft times offreth one maner of offring, which can neuer take away sinnes:
Ni kweli, kila kuhani husimama kwa huduma siku kwa siku, akitoa dhabihu ile ile, ambayo, kwa vyovyote, kamwe isingeweza kuziondoa dhambi.
12 But this man after he had offered one sacrifice for sinnes, sitteth for euer at the right hand of God,
Lakini baada ya Kristo kutoa dhabihu mara moja kwa dhambi milele yote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,
13 And from hencefoorth tarieth, till his enemies be made his footestoole.
akisubiri mpaka maadui zake watiwe chini na kufanywa kiti kwa ajili ya miguu yake.
14 For with one offering hath he consecrated for euer them that are sanctified.
Kwa kuwa kwa njia ya toleo moja amewakamilisha milele wale ambao wametengwa kwa Mungu.
15 For the holy Ghost also beareth vs record: for after that he had sayd before,
Na Roho Mtakatifu pia ashuhudia kwetu. Kwa kuwa kwanza alisema,
16 This is the Testament that I will make vnto them after those dayes, sayth the Lord, I wil put my Lawes in their heart, and in their mindes I will write them.
“Hili ni agano nitakalofanya pamoja nao baada ya siku hizo; asema Bwana: nitaweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao”.
17 And their sinnes and iniquities will I remember no more.
Kisha alisema, “Hawatazikumbuka tena dhambi na matendo yao mafu”.
18 Nowe where remission of these things is, there is no more offering for sinne.
Sasa mahali palipo na msamaha kwa hawa, hakuna tena dhabihu yoyote kwa ajili ya dhambi.
19 Seeing therefore, brethren, that by the blood of Iesus we may be bolde to enter into the Holy place,
Kwa hiyo, ndugu, tunao ujasiri wa kuingia mahali patakatifu zaidi kwa damu ya Yesu.
20 By the newe and liuing way, which hee hath prepared for vs, through the vaile, that is, his flesh:
Hiyo ni njia ambayo ameifungua kwa ajili yetu kwa njia ya mwili wake, mpya na hai inayopitia kwenye pazia.
21 And seeing we haue an hie Priest, which is ouer the house of God,
Na kwa sababu tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 Let vs drawe neere with a true heart in assurance of faith, our hearts being pure from an euill conscience,
na tumkaribie na moyo wa kweli katika utimilifu wa uhakika wa imani tukiwa na mioyo iliyonyunyiziwa safi kutoka uovu wa dhamiri na kuwa na miili yetu iliyooshwa kwa maji safi.
23 And washed in our bodies with pure water, let vs keepe the profession of our hope, without wauering, (for he is faithfull that promised)
Basi na tushikilie kwa uthabiti katika ungamo la ujasiri wa tumaini letu, bila ya kugeuka, kwa sababu Mungu aliyeahidi ni mwaminifu.
24 And let vs consider one another, to prouoke vnto loue, and to good workes,
Na tuzidi kutafakari namna ya kumtia moyo kila mmoja kupenda na matendo mema.
25 Not forsaking the fellowship that we haue among our selues, as the maner of some is: but let vs exhort one another, and that so much the more, because ye see that the day draweth neere.
Na tusiache kukusanyika pamoja, kama wafanyavyo wengine. Badala yake, kutiana moyo kila mmoja zaidi na zaidi, kama muonavyo siku inakaribia.
26 For if we sinne willingly after that we haue receiued and acknowledged that trueth, there remaineth no more sacrifice for sinnes,
Kama tukifanya makusudi kuendelea kutenda dhambi baada ya kuwa tumepokea elimu ya ukweli, Dhabihu nyingine ya dhambi haisalii tena.
27 But a fearefull looking for of iudgement, and violent fire, which shall deuoure the aduersaries.
Badala yake, kuna tarajio pekee la hukumu ya kutisha, na ukali wa moto ambao utawateketeza maadui wa Mungu.
28 He that despiseth Moses Law, dieth without mercy vnder two, or three witnesses:
Yeyote ambaye ameikataa sheria ya Musa hufa bila rehema mbele ya ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
29 Of howe much sorer punishment suppose ye shall hee be worthy, which treadeth vnder foote the Sonne of God, and counteth the blood of the Testament as an vnholy thing, wherewith he was sanctified, and doeth despite the Spirit of grace?
kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahiri kilammoja ambaye amemdharau mwana wa Mungu, yeyote aliyeitendea damu ya agano kama kitu kisicho kitakatifu, damu ambayo kwayo aliiweka wakfu kwa Mungu - yeyote ambaye amemtukana Roho wa neema?
30 For we know him that hath sayd, Vengeance belongeth vnto mee: I will recompense, saith the Lord. And againe, The Lord shall iudge his people.
Kwakuwa tunajua mmoja ambaye aliyesema, “Kisasi ni changu, nitalipa”. Na tena, “Bwana atawahukumu watu wake”.
31 It is a fearefull thing to fall into the hands of the liuing God.
Ni jambo la kuogofya mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai!
32 Nowe call to remembrance the dayes that are passed, in the which, after ye had receiued light, ye endured a great fight in afflictions,
Lakini kumbuka siku zilizopita, baada ya kutiwa kwenu nuru, ni jinsi gani mliweza kuvumilia maumivu makali.
33 Partly while yee were made a gazing stocke both by reproches and afflictions, and partly while ye became companions of them which were so tossed to and from.
Mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso, na mlikuwa washiriki pamoja na wale waliopitia mateso kama hayo.
34 For both ye sorowed with mee for my bonds, and suffered with ioy the spoyling of your goods, knowing in your selues howe that ye haue in heauen a better, and an enduring substance.
Kwa kuwa mlikuwa na moyo wa huruma kwa hao waliokuwa wafungwa, na mlipokea kwa furaha adhabu ya urithi wenu, mkijua kwamba ninyi wenyewe mlikuwa na urithi bora na wa kudumu milele.
35 Cast not away therefore your confidence which hath great recompense of reward.
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.
36 For ye haue neede of patience, that after ye haue done the will of God, ye might receiue the promise.
Kwa kuwa mnahitaji uvumilivu, ili kwamba mpate kupokea ambacho Mungu amekiahidi, baada ya kuwa mmekwisha yatenda mapenzi yake.
37 For yet a very litle while, and hee that shall come, will come, and will not tary.
Kwa kuwa baada ya kitambo kidogo, mmoja anayekuja, atakuja hakika na hatakawia.
38 Nowe the iust shall liue by faith: but if any withdrawe himselfe, my soule shall haue no pleasure in him.
Mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Kama atarudi nyuma, sitapendezwa naye.”
39 But we are not they which withdrawe our selues vnto perdition, but follow faith vnto the conseruation of the soule.
Lakini sisi si kama wale warudio nyuma kwa kuangamia. Badala yake, sisi ni baadhi ya wale tulio na imani ya kuzilinda roho zetu.

< Hebrews 10 >