< Genesis 5 >

1 This is the booke of the generations of Adam. In the day that God created Adam, in the likenes of God made he him,
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 Male and female created he them, and blessed them, and called their name Adam in the day that they were created.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Nowe Adam liued an hundred and thirtie yeeres, and begate a childe in his owne likenes after his image, and called his name Sheth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 And the dayes of Adam, after he had begotten Sheth, were eight hundreth yeeres, and he begate sonnes and daughters.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 So all the dayes that Adam liued, were nine hundreth and thirtie yeeres: and he died.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 And Sheth liued an hundreth and fiue yeeres, and begate Enosh.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And Sheth liued, after he begate Enosh, eight hundreth and seuen yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 So all the dayes of Sheth were nine hundreth and twelue yeeres: and he died.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Also Enosh liued ninetie yeeres, and begate Kenan.
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 And Enosh liued, after he begate Kenan, eight hundreth and fifteene yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 So all the dayes of Enosh were nine hundreth and fiue yeeres: and he died
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Likewise Kenan liued seuentie yeeres, and begate Mahalaleel.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And Kenan liued, after he begate Mahalaleel, eight hundreth and fourtie yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 So all the dayes of Kenan were nine hundreth and tenne yeeres: and he died.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Mahalaleel also liued sixtie and fiue yeres, and begate Iered.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 Also Mahalaleel liued, after he begate Iered, eight hundreth and thirtie yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 So all the dayes of Mahalaleel were eight hundreth ninetie and fiue yeeres: and he died.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 And Iered liued an hundreth sixtie and two yeeres, and begate Henoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 Then Iered liued, after he begate Henoch, eight hundreth yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 So all the dayes of Iered were nine hundreth sixtie and two yeeres: and he died.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Also Henoch liued sixtie and fiue yeeres, and begate Methushelah.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 And Henoch walked with God, after he begate Methushelah, three hundreth yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 So all the dayes of Henoch were three hundreth sixtie and fiue yeeres.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 And Henoch walked with God, and he was no more seene: for God tooke him away.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Methushelah also liued an hundreth eightie and seuen yeeres, and begate Lamech.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 And Methushelah liued, after he begate Lamech, seuen hundreth eightie and two yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 So al the dayes of Methushelah were nine hundreth sixtie and nine yeeres: and he died.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Then Lamech liued an hundreth eightie and two yeeres, and begate a sonne,
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 And called his name Noah, saying, This same shall comfort vs concerning our worke and sorowe of our hands, as touching the earth, which the Lord hath cursed.
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 And Lamech liued, after he begate Noah, fiue hundreth ninetie and fiue yeeres, and begate sonnes and daughters.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 So all the dayes of Lamech were seuen hundreth seuentie and seuen yeeres: and he died.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 And Noah was fiue hundreth yeere olde. And Noah begate Shem, Ham and Iapheth.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< Genesis 5 >