< Genesis 29 >

1 Then Iaakob lift vp his feete and came into the East countrey.
Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
2 And as he looked about, behold there was a well in the field, and lo, three flocks of sheepe lay thereby (for at that well were the flockes watered) and there was a great stone vpon the welles mouth.
Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
3 And thither were all the flockes gathered, and they rolled the stone from the welles mouth, and watered the sheepe, and put the stone againe vpon the welles mouth in his place.
Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
4 And Iaakob sayde vnto them, My brethren, whence be ye? And they answered, We are of Haran.
Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
5 Then he sayd vnto them, Know ye Laban the sonne of Nahor? Who said, We know him.
Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
6 Againe he sayd vnto them, Is he in good health? And they answered, He is in good health, and beholde, his daughter Rahel commeth with the sheepe.
Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
7 Then he sayd, Lo, it is yet hie day, neither is it time that the cattell shoulde be gathered together: water ye the sheepe and go feede them.
Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
8 But they sayde, We may not vntill all the flocks be brought together, and till men rolle the stone from the welles mouth, that we may water the sheepe.
Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
9 While he talked with them, Rahel also came with her fathers sheepe, for she kept them.
Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
10 And assoone as Iaakob saw Rahel ye daughter of Laban his mothers brother, and the sheepe of Laban his mothers brother, then came Iaakob neere, and rolled the stone from the welles mouth, and watered ye flocke of Laban his mothers brother.
Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
11 And Iaakob kissed Rahel, and lift vp his voyce and wept.
Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
12 (For Iaakob tolde Rahel, that he was her fathers brother, and that he was Rebekahs sonne) then she ranne and tolde her father.
Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
13 And when Laban heard tell of Iaakob his sisters sonne, he ranne to meete him, and embraced him and kissed him, and brought him to his house: and he tolde Laban all these things.
Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
14 To whome Laban sayd, Well, thou art my bone and my flesh. and he abode with him the space of a moneth.
Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
15 For Laban sayde vnto Iaakob, Though thou be my brother, shouldest thou therfore serue me for nought? tell me, what shalbe thy wages?
Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
16 Now Laban had two daughters, the elder called Leah, and the yonger called Rahel.
Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
17 And Leah was tender eyed, but Rahel was beautifull and faire.
Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
18 And Iaakob loued Rahel, and sayde, I will serue thee seuen yeeres for Rahel thy yonger daughter.
Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
19 Then Laban answered, It is better that I giue her thee, then that I should giue her to another man: abide with me.
Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
20 And Iaakob serued seuen yeres for Rahel, and they seemed vnto him but a few dayes, because he loued her.
Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
21 Then Iaakob sayde to Laban, Giue me my wife, that I may goe in to her: for my terme is ended.
Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
22 Wherefore Laban gathered together all the men of the place, and made a feast.
Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
23 But whe the euening was come, he tooke Leah his daughter and brought her to him, and he went in vnto her.
Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
24 And Laban gaue his mayde Zilpah to his daughter Leah, to be her seruant.
Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
25 But when the morning was come, behold, it was Leah. Then sayde he to Laban, Wherefore hast thou done thus to mee? did not I serue thee for Rahel? wherfore then hast thou beguiled me?
Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
26 And Laban answered, It is not the maner of this place, to giue the yonger before the elder.
Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
27 Fulfill seuen yeeres for her, and we wil also giue thee this for the seruice, which thou shalt serue me yet seuen yeeres more.
Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
28 Then Iaakob did so, and fulfilled her seuen yeeres, so he gaue him Rahel his daughter to be his wife.
Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
29 Laban also gaue to Rahel his daughter Bilhah his mayde to be her seruant.
Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
30 So entred he in to Rahel also, and loued also Rahel more then Leah, and serued him yet seuen yeeres more.
Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
31 When the Lord saw that Leah was despised, he made her fruitful: but Rahel was barren.
Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
32 And Leah conceiued and bare a sonne, and she called his name Reuben: for she said, Because the Lord hath looked vpon my tribulation, now therefore mine husband will loue me.
Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
33 And she conceiued againe and bare a sonne, and sayde, Because the Lord heard that I was hated, he hath therefore giuen me this sonne also, and she called his name Simeon.
Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
34 And she conceiued againe and bare a sonne, and said, Now at this time wil my husband keepe mee company, because I haue borne him three sonnes: therefore was his name called Leui.
Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
35 Moreouer shee conceiued againe and bare a sonne, saying, Nowe will I prayse the Lord: therefore shee called his name Iudah, and left bearing.
Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.

< Genesis 29 >