< Genesis 23 >

1 When Sarah was an hundreth twentie and seuen yeere olde (so long liued she).
Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
2 Then Sarah dyed in Kiriath-arba: the same is Hebron in the land of Canaan. and Abraham came to mourne for Sarah and to weepe for her.
Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
3 Then Abraham rose vp from the sight of his corps, and talked with the Hittites, saying,
Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
4 I am a stranger, and a forreiner among you, giue me a possession of buriall with you, that I may burie my dead out of my sight.
“Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
5 Then the Hittites answered Abraham, saying vnto him,
Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
6 Heare vs, my lorde: thou art a prince of God among vs: in the chiefest of our sepulchres bury thy dead: none of vs shall forbid thee his sepulchre, but thou mayest bury thy dead therein.
“Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
7 Then Abraham stoode vp, and bowed him selfe before the people of the land of the Hittites.
Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
8 And he communed with them, saying, If it be your minde, that I shall bury my dead out of my sight, heare me, and intreate for me to Ephron the sonne of Zohar,
Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
9 That he would giue me ye caue of Machpelah, which he hath in the ende of his field: that he would giue it me for as much money as it is worth, for a possession to bury in among you.
Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
10 (For Ephron dwelt among the Hittites) Then Ephron the Hittite answered Abraham in the audience of all the Hittites that went in at the gates of his citie, saying,
Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
11 No, my Lord, heare me: the fielde giue I thee, and the caue, that therein is, I giue it thee: euen in the presence of the sonnes of my people giue I it thee, to bury thy dead.
“Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
12 Then Abraham bowed himselfe before the people of the land,
Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
13 And spake vnto Ephron in the audience of the people of the countrey, saying, Seeing thou wilt giue it, I pray thee, heare me, I will giue the price of the fielde: receiue it of me, and I will bury my dead there.
Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
14 Ephron then answered Abraham, saying vnto him,
Efroni akamjibu Abraham, akisema,
15 My lord, hearken vnto me: ye land is worth foure hundreth shekels of siluer: what is that betweene me and thee? bury therefore thy dead.
“Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
16 So Abraham hearkened vnto Ephron, and Abraham weyed to Ephron the siluer, which he had named, in the audience of the Hittites, euen foure hundreth siluer shekels of currant money among marchants.
Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
17 So the fielde of Ephron which was in Machpelah, and ouer against Mamre, euen the field and the caue that was therein, and all the trees that were in the fielde, which were in all the borders round about, was made sure
Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
18 Vnto Abraham for a possession, in ye sight of the Hittites, euen of all that went in at the gates of his citie.
kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
19 And after this, Abraham buried Sarah his wife in the caue of the fielde of Machpelah ouer against Mamre: the same is Hebron in the land of Canaan.
Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
20 Thus the fielde and the caue, that is therein, was made sure vnto Abraham for a possession of buriall by the Hittites.
Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.

< Genesis 23 >