< Genesis 13 >

1 Then Abram went vp from Egypt, he, and his wife, and all that he had, and Lot with him toward the South.
Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
2 And Abram was very rich in cattell, in siluer and in golde.
Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
3 And he went on his iourney from ye South toward Beth-el, to the place where his tent had bene at ye beginning, betweene Beth-el and Haai,
Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
4 Vnto the place of the altar, which he had made there at the first: and there Abram called on the Name of the Lord.
Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
5 And Lot also, who went with Abram, had sheepe, and cattell and tentes,
aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
6 So that the land coulde not beare them, that they might dwell together: for their substance was great, so that they coulde not dwell together.
Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
7 Also there was debate betweene ye heardmen of Abrams cattell, and the heardmen of Lots cattell. (and the Canaanites and the Perizzites dwelled at that time in the land.)
Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
8 Then saide Abram vnto Lot, Let there be no strife, I pray thee, betweene thee and me, neither betweene mine heardmen and thine heardmen: for we be brethren.
Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
9 Is not the whole land before thee? depart I pray thee from me: if thou wilt take the left hand, then I will goe to the right: or if thou goe to the right hand, then I will take the left.
Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
10 So when Lot lifted vp his eyes, he saw that all the plaine of Iorden was watered euery where: (for before the Lord destroyed Sodom and Gomorah, it was as the garden of the Lord, like the land of Egypt, as thou goest vnto Zoar)
Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
11 Then Lot chose vnto him all the plaine of Iorden, and tooke his iourney from the East: and they departed the one from the other.
Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
12 Abram dwelled in the lande of Canaan, and Lot abode in the cities of the plaine, and pitched his tent euen to Sodom.
Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
13 Now the men of Sodom were wicked and exceeding sinners against the Lord.
Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
14 Then the Lord saide vnto Abram, (after that Lot was departed from him) Lift vp thine eyes nowe, and looke from the place where thou art, Northward, and Southward, and Eastwarde, and Westward:
Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
15 For all the land, which thou seest, will I giue vnto thee and to thy seede for euer,
Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
16 And I will make thy seede, as the dust of the earth: so that if a man can number the dust of the earth, then shall thy seede be numbred.
Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
17 Arise, walke through the land, in ye length thereof, and breadth thereof: for I will giue it vnto thee.
Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
18 Then Abram remoued his tent, and came and dwelled in the plaine of Mamre, which is in Hebron, and builded there an altar vnto ye Lord.
Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.

< Genesis 13 >