< Genesis 12 >

1 For the Lord had said vnto Abram, Get thee out of thy countrey, and from thy kindred, and from thy fathers house vnto the land that I will shewe thee.
Kisha Yahwe akamwambia Abram, “Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako, na kwa jamaa za baba yako, uende katika nchi nitakayo kuonesha.
2 And I will make of thee a great nation, and will blesse thee, and make thy name great, and thou shalt be a blessing.
Nitakufanya uwe taifa kubwa, na nitakubariki na kulifanya jinalako kuwa kubwa, na utafanyika baraka.
3 I will also blesse them that blesse thee, and curse them that curse thee, and in thee shall all families of the earth be blessed.
Nitawabariki wakubarikio, lakini asiye kuheshimu nita mlaani. Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa.
4 So Abram departed, euen as ye Lord spake vnto him, and Lot went with him. (And Abram was seuentie and fiue yeere olde, when he departed out of Haran)
Kwa hiyo Abram akaondoka kama vile Yahwe alivyo mwambia kufanya, na Lutu akaenda pamoja naye. Abram alikuwa na miaka sabini na mitano wakati alipotoka Harani.
5 Then Abram tooke Sarai his wife, and Lot his brothers sonne, and all their substance that they possessed, and the soules that they had gotten in Haran, and they departed, to goe to the land of Canaan: and to the land of Canaan they came.
Abram akamchukua Sarai mkewe, Lutu, mtoto wa ndugu yake, na vyote walivyomiliki ambavyo wamevikusanya, na watu ambao wamewapata wakiwa huko Harani. Wakatoka kwenda katika nchi ya Kanaani, wakafika nchi ya Kanaani.
6 So Abram passed through the land vnto the place of Shechem, and vnto the plaine of Moreh (and the Canaanite was then in ye land)
Abram akapitia katikati ya nchi hadi Shekemu, hadi mwaloni wa More. Wakati huo wakanaani waliishi katika nchi hiyo.
7 And the Lord appeared vnto Abram, and said, Vnto thy seede will I giue this land. And there builded he an altar vnto the Lord, which appeared vnto him.
Yahwe akamtokea Abram, na kusema, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Kwa hiyo Abram akamjengea madhabahu, Yahwe ambaye alimtokea.
8 Afterward remouing thence vnto a moutaine Eastward from Beth-el, he pitched his tent hauing Beth-el on the Westside, and Haai on the East: and there he built an altar vnto the Lord, and called on the Name of the Lord.
Kutoka pale akaenda kwenye nchi ya mlima mashariki mwa Betheli, ambapo alipiga hema yake, magaribi kukiwa na Betheli na mashariki kukiwa na mji wa Ai. Akajenga madhabahu ya Yahwe pale na kuliitia jina la Yahwe.
9 Againe Abram went forth going and iourneying toward the South.
Kisha Abram akaendelea kusafiri, akielekea upande wa Negebu.
10 Then there came a famine in the land: therefore Abram went downe into Egypt to soiourne there: for there was a great famine in the lande.
Kulikuwa na njaa katika nchi, kwa hiyo Abram akaenda kukaa Misri, kwa kuwa njaa ilikua kali katika nchi.
11 And when he drewe neere to enter into Egypt, he said to Sarai his wife, Beholde nowe, I know that thou art a faire woman to looke vpon:
Wakati alipokaribia kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “tazama, najua kuwa wewe ni mwanamke mzuri.
12 Therefore it will come to passe, that when the Egyptians see thee, they will say, She is his wife: so will they kill me, but they will keepe thee aliue.
Wamisri watakapokuona watasema, huyu ni mke wake, na wataniua mimi, lakini watakuacha wewe hai.
13 Say, I pray thee, that thou art my sister, that I may fare well for thy sake, and that my life may be preserued by thee.
Hivyo wewe sema kuwa ni dada yangu, ili kwamba niwe salama kwa sababu yako, na kumba maisha yangu yatasalimika kwa sababu yako.”
14 Nowe when Abram was come into Egypt, the Egyptians behelde the woman: for she was very faire.
Ikawa kwamba Abram alipoingia Misri, Wamisri wakaona kwamba Sarai ni mzuri sana.
15 And the Princes of Pharaoh sawe her, and commended her vnto Pharaoh: so the woman was taken into Pharaohs house:
Wakuu wa Farao wakamuona, na kumsifia kwa Farao, na huyu mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao.
16 Who intreated Abram well for her sake, and he had sheepe, and beeues, and hee asses, and men seruants and maide seruants, and shee asses, and camelles.
Farao akamtendea kwa wema Abram kwa ajili yake, na akampatia kondoo, maksai, punda waume watumishi wa kiume, watumishi wa kike, punda wake, na ngamia.
17 But the Lord plagued Pharaoh and his house with great plagues, because of Sarai Abrams wife.
Kisha Yahwe akampiga Farao na nyumba yake kwa mapigo makuu kwa sababau ya Sarai, mke wa Abram.
18 Then Pharaoh called Abram, and saide, Why hast thou done this vnto me? Wherefore diddest thou not tell me, that she was thy wife?
Farao akamwita Abram na kusema, “Nini hiki ambacho umenifanyia? Kwa nini hukuniambia kuwa alikuwa mke wako?
19 Why saidest thou, She is my sister, that I should take her to be my wife? Nowe therefore beholde thy wife, take her and goe thy way.
Kwa nini ulisema, 'ni dada yangu; na mimi nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa kwa sababu hiyo huyu hapa mke wako. Mchukue na uende zako.”
20 And Pharaoh gaue men commandement concerning him: and they conueyed him forth, and his wife, and all that he had.
Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye, na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo.

< Genesis 12 >