< Genesis 10 >

1 Now these are the generations of the sonnes of Noah, Shem, Ham and Iapheth: vnto whom sonnes were borne after the flood.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 The sonnes of Iapheth were Gomer and Magog, and Madai, and Iauan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 And the sonnes of Gomer, Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 Also the sonnes of Iauan, Elishah and Tarshish, Kittim, and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 Of these were the yles of the Gentiles deuided in their landes, euery man after his tongue, and after their families in their nations.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 Moreouer, ye sonnes of Ham were Cush, and Mizraim, and Put, and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 And the sonnes of Cush, Seba and Hauilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabtecha: also the sonnes of Raamah were Sheba and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 And Cush begate Nimrod, who began to be mightie in the earth.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 He was a mightie hunter before the Lord. wherefore it is saide, As Nimrod the mightie hunter before the Lord.
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 And the beginning of his kingdome was Babel, and Erech, and Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 Out of that land came Asshur, and builded Niniueh, and the citie Rehoboth, and Calah:
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 Resen also betweene Niniueh and Calah: this is a great citie.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 And Mizraim begate Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim.
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 Pathrusim also, and Casluhim (out of whom came the Philistims) and Caphtorims.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 Also Canaan begat Zidon his first borne, and Heth,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 And Iebusi, and Emori, and Girgashi,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 And Hiui, and Arki, and Sini,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 And Aruadi, and Zemari, and Hamathi: and afterwarde were the families of the Canaanites spred abroade.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 Then the border of the Canaanites was from Zidon, as thou commest to Gerar vntil Azzah, and as thou goest vnto Sodom, and Gomorah, and Admah, and Zeboijm, euen vnto Lasha.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 These are the sonnes of Ham according to their families, according to their tongues in their countries and in their nations.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 Vnto Shem also the father of all the sonnes of Eber, and elder brother of Iapheth were children borne.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 The sonnes of Shem were Elam and Asshur, and Arpachshad, and Lud, and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 And the sonnes of Aram, Vz and Hul, and Gether and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 Also Arpachshad begate Shelah, and Shelah begate Eber.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 Vnto Eber also were borne two sonnes: the name of the one was Peleg: for in his dayes was the earth diuided: and his brothers name was Ioktan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 Then Ioktan begate Almodad and Sheleph, and Hazarmaueth, and Ierah,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 And Hadoram, and Vzal, and Dicklah,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 And Obal, and Abimael, and Sheba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 And Ophir, and Hauilah, and Iobab: all these were the sonnes of Ioktan.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 And their dwelling was from Mesha, as thou goest vnto Sephar a mount of the East.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 These are the sonnes of Shem according to their families, according to their tongues, in their countreis and nations.
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 These are the families of the sonnes of Noah, after their generations among their people: and out of these were the nations diuided in the earth after the flood.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< Genesis 10 >