< Ezekiel 8 >

1 And in the sixt yere, in the sixt moneth, and in the fift day of the moneth, as I sate in mine house, and the Elders of Iudah sate before me, the hand of the Lord God fell there vpon me.
Hivyo ikawa kuhusu katika mwaka wa sita na mwezi wa sita, katika siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nimeketi kwenye nyumba yangu na wazee wa Yuda waliketi mbele yangu, kwamba mkono wa Bwana Yahwe ukanijaza juu yangu huko.
2 Then I beheld, and lo, there was a likenesse, as the appearance of fire, to looke to, from his loynes downeward, and from his loynes vpward, as the appearance of brightnes, and like vnto amber.
Hivyo nikaona, na tazama, kulikuwa na mfano kama mwonekano wa mwanadamu. Kutoka kwenye mwonekano wake wa nyonga kwenda chini kulikuwa na moto. Na kutoka kwenye nyonga kwenda juu kulikuwa na mwonekano wa kitu kinachong'aa, kama mng'ao wa chuma.
3 And he stretched out the likenes of an had, and tooke me by an hearie locke of mine head, and the Spirit lift me vp betweene the earth, and the heauen, and brought mee by a Diuine vision to Ierusalem, into the entry of ye inner gate that lieth toward the North, where remained the idole of indignation, which prouoked indignation.
Kisha akanyoosha kutoka kwenye mkono na kunichukua kwa nywele za kichwa changu; Roho akaniacha juu kati ya dunia na mbingu, na katika maono kutoka kwa Mungu, akaniletea hata Yerusalemu, kwenye mlango wa kuingia ndani ya lango la kaskazini, ambako sanamu ile iletayo wivu mkubwa ilipokuwa imesiamama.
4 And beholde, the glorie of the God of Israel was there according to the vision, that I saw in the fielde.
Kisha tazama, utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa huko, kulingana na ono nililokuwa nimeliona kwenye uwanda.
5 Then saide he vnto mee, Sonne of man, lift vp thine eyes nowe towarde the North. So I lift vp mine eyes towarde the North, and beholde, Northward, at the gate of the altar, this idole of indignation was in the entrie.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, inua juu macho yako kwenda upande wa kaskazini.” Hivyo nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na kwenye lango la kaskazini kulekea kwenye madhabahu, huko kwenye lango la kuingilia, kulikuwa na sanamu ya wivu.
6 He said furthermore vnto me, Sonne of man, seest thou not what they doe? euen the great abominations that the house of Israel committeth here to cause me to depart from my Sanctuarie? but yet turne thee and thou shalt see greater abominations.
Hivyo akanambia, “Mwanadamu, unaona wanayoyafanya? Haya ni machukizo makubwa ambayo nyumba ya Israeli wanayoyafanya hapa kunifanya niende mbali kutoka patakatifu pangu. Lakini utageuka na kuona machukizo makubwa zaidi.”
7 And he caused me to enter at the gate of the court: and when I looked, beholde, an hole was in the wall.
Kisha akanileta hata kwenye mlango wa uzio, na nikatazama, kulikuwa na shimo kwenye ukuta.”
8 Then said he vnto me, Sonne of man, digge nowe in the wall. And when I had digged in the wall, beholde, there was a doore.
Akanambia, “Mwanadamu, chimba kwenye huu ukuta.” Basi nikachimba kwenye huo ukuta, na kulikuwa na mlango.
9 And he said vnto mee, Go in, and beholde the wicked abominations that they doe here.
Kisha akanambia, “Nenda na ukaone machukizo ya uovu ambayo wanayoyafanya hapa.”
10 So I went in, and sawe, and beholde, there was euery similitude of creeping thinges and abominable beasts and all the idoles of the house of Israel painted vpon the wall round about.
Basi nilipokuwa nikienda ndani na nikaona, na tazama! Kulikuwa na kila umbo la vitu vikitembea polepole na mnyama achukizaye sana! Kila sanamu wa nyumba ya Israeli ilikuwa imechongwa kwenye ukuta pande zote.
11 And there stoode before them seuentie men of the Ancients of the house of Israel, and in the middes of them stoode Iaazaniah, ye sonne of Shaphan, with euerie man his censour in his hand, and the vapour of the incense went vp like a cloude.
Wazee sabini wa wa nyumba ya Israeli walikuwa huko, na Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama katikati yao. Walikuwa wamesimama mbele ya picha, na kila mtu alikuwa na chetezo kwenye mkono wake ili kwamba harufu ya ubani ingeweza kupanda juu.
12 Then saide hee vnto mee, Sonne of man, hast thou seene what the Ancients of the house of Israel do in the darke, euery one in the chamber of his imagerie? for they say, The Lord seeth vs not, the Lord hath forsaken the earth.
Akanambia, “mwanadamu, unaona kile ambacho wazee wa nyumba ya Israeli wanachokifanya kwenye giza? Kila mmoja hufanya hivi kwenye chumba cha sanamu yake, kwa kuwa husema, 'Yahwe hatuone! Yahwe ameitelekeza hii nchi.”'
13 Againe he saide also vnto me, Turne thee againe, and thou shalt see greater abominations that they doe.
Kisha akanambia, “Geuka tena na tazama machukizo makubwa ambayo wanayoyafanya.”
14 And he caused me to enter into the entrie of the gate of the Lords house, which was toward the North: and beholde there sate women mourning for Tammuz.
Tena akanileta kwenye lango la kuingia la nyumba ya Yahwe lililokuwa upande waa kaskazini, na tazama! Wanawake walikuwa wameketi huko wakimlilia Tamuzi.
15 Then saide hee vnto me, Hast thou seene this, O sonne of man? Turne thee againe, and thou shalt see greater abominations then these.
Hivyo akanambia, “Umeiona hii, mwanadamu? Geuka tena na uone machukizo makubwana zaidi kuliko hayo.”
16 And he caused me to enter into the inner court of the Lordes house, and beholde, at the doore of the Temple of the Lord, betweene the porche and the altar were about fiue and twentie men with their backs toward the Temple of the Lord, and their faces towarde the East, and they worshipped the sunne, towarde the East.
Akanileta hata kwenye uzio wa ndani wa nyumba ya Yahwe, na tazama! huko kwenye lango la kuingia kwenye madhabahu, kulikuwa na takribani watu ishirini na tano waliokuwa wamelipa mgongo hekalu la Yahwe na nyuso zao kuelekea mashariki, na walikuwa wakiabudu jua.
17 The he said vnto me, Hast thou seene this, O sonne of man? Is it a small thing to the house of Iudah to commit these abominations which they do here? for they haue filled the land with crueltie, and haue returned to prouoke mee: and loe, they haue cast out stinke before their noses.
Akanambia, “Unaona hii, mwanadamu? Je ni kitu kidigo kwa ajili ya nyumba ya Yuda kufanya haya machukizo wanayoyafanya? Kwa kuwa wameijaza nchi kwa uovu na wamerudi tena ili kuniletea hasira, kuweka tawi kwenye pua zao.
18 Therefore will I also execute my wrath: mine eye shall not spare them, neither will I haue pitie, and though they crie in mine eares with a loude voyce, yet will I not heare them.
Hivyo nitatenda miongoni mwao pia; jicho langu halitakuwa na huruma, sitaacha kuwaharibu. hata watalia kwenye masikio yangu kwa sauti kubwa, sitawasikia.”

< Ezekiel 8 >