< Ezekiel 5 >

1 And thou sonne of man, take thee a sharpe knife, or take thee a barbours rasor and cause it to passe vpon thine head, and vpon thy beard: then take thee balances to weigh, and deuide the heare.
“Kisha wewe mwana wa adamu, chukua upanga mkali kama wembe wa kinyozi kwa ajili yako mwenyewe, na pitisha hayo makali juu ya kichwa chako na ndevu zako, kisha chukua mizani za kupimia uzito na uzigawanye nywele zako.
2 Thou shalt burne with fire the thirde part in the middes of the citie, when the dayes of the siege are fulfilled, and thou shalt take the other thirde part, and smite about it with a knife, and the last thirde part thou shalt scatter in the winde, and I will drawe out a sworde after them.
Choma theluthi ya tatu ya hiyo kwa moto katikati ya mji wakati siku za kuzingirwa zitakapokamilika, na chukua theluthi ya nywele na uipige kwa panga na kuuzunguka mji. Kisha tawanya theluthi yake kwenye upepo, na nitasogeza panga karibu ili kufukuza watu.
3 Thou shalt also take thereof a fewe in nomber, and binde them in thy lappe.
Lakini chukua kiasi kidogo cha nywele na zifunge kwenye pindo za nguo yako.
4 Then take of them againe and cast them into the middes of the fire, and burne them in the fire: for thereof shall a fire come foorth into all the house of Israel.
Kisha chukua tena zile nyewele na zitupe katikati ya moto; na zichome kwenye moto; kutoka hapo utatoka nje kwenda nyumba zote za Israeli.”
5 Thus saith the Lord God, This is Ierusalem: I haue set it in the middes of the nations and countreyes, that are rounde about her.
Bwana Yahwe asema hivi, “Hii ndio Yerusalemu katikati ya mataifa, nilipomuweka, na ambapo nilipomzunguka kwa nchi zingine.
6 And she hath changed my iudgements into wickednes more then the nations, and my statutes more then the countreis, that are round about her: for they haue refused my iudgemets and my statutes, and they haue not walked in them.
Lakini anaudhaifu wa kukataa amri zangu zaidi kuliko mataifa yalivyo, na sheria yangu zaidi kuliko mataifa ambayo yanayomzunguka. Watu wamezikataa humuku zangu na kuacha kutembea katika sheria zangu.”
7 Therefore thus saith the Lord God, Because your multitude is greater then the nations that are rounde about you, and ye haue not walked in my statutes, neither haue ye kept my iudgements: no, ye haue not done according to the iudgements of the nations, that are rounde about you,
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, “Kwa sababu mmekuwa kikwazo kuliko mataifa ambayo yanayowazunguka na kuacha kutembea kwenye amri zangu wala kutenda kulingana na amri zangu, wala hata kutenda kulingana na amri za mataifa yanayowazunguka,”
8 Therefore thus saith the Lord God, Beholde, I, euen I come against thee, and will execute iudgement in the middes of thee, euen in the sight of the nations.
kwa hiyo Bwana asema hivi, “Tazama! Mimi mwenyewe nitatenda juu yenu. Nitato hukumu kati yenu ili mataifa waone.
9 And I will doe in thee, that I neuer did before, neither will do any more the like, because of all thine abominations.
Nitawafanyia yale ambayo sijawahi kuyafanya na kile ambacho sintokifanya tena, kwa sababu ya matendo yenu ya kuchukiza.
10 For in the middes of thee, the fathers shall eate their sonnes, and the sonnes shall eate their fathers, and I will execute iudgement in thee, and the whole remnant of thee will I scatter into all the windes.
Kwa hiyo baba watawala watoto kati yenu, na watoto watawala baba zao, kwa kuwa nitafanya hukumu juu yenu na kuwatawanya kila mahali wote ninyi mliobaki.
11 Wherefore, as I liue, saith the Lord God, Surely because thou hast defiled my Sanctuarie with all thy filthinesse, and with all thine abominations, therefore will I also destroy thee, neither shall mine eye spare thee, neither will I haue any pitie.
Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-bila shaka hii ilikuwa kwa sababu umapanajisi patakatifu pangu kwa mambo ya machukizo yako yote na kwa matendo yako yote niyachukiayo, kwamba mimi mwenyewe nitakupunguza katika hesabu; jicho langu halitakuhurumia, na sintoacha kukuharibu.
12 The third part of thee shall die with the pestilence, and with famine shall they bee consumed in the middes of thee: and another third part shall fall by the sword round about thee: and I will scatter the last third part into all windes, and I will drawe out a sword after them.
Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na wataliwa na njaa katikati yenu. Theluthi wataanguka kwa upanga likiwazunguka. Kisha nitawatawanya theluthi katika mahali pote, na nitafuatisha upanga kuwafukuza pia.
13 Thus shall mine anger bee accomplished, and I will cause my wrath to cease in them, and I will be comforted: and they shall knowe, that I the Lord haue spoke it in my zeale, when I haue accomplished my wrath in them.
Hivi ndivyo ghadhabu yangu itavyokamilika, na nitasababisha ghadhabu yangu juu yao hata kulala. Nitajiridhisha, na watajua kwamba, mimi Yahwe, nimenena kwa ghadhabu yangu wakati nitakapo kamilisha ghadhabu yangu dhidi yao.
14 Moreouer, I will make thee waste, and abhorred among the nations, that are round about thee, and in the sight of all that passe by.
Nitakufanya mkiwa kwa mataifa yanayokuzunguka kwenye uso wa kila mtu apitaye karibu.
15 So thou shalt bee a reproche and shame, a chastisement and an astonishment vnto the nations, that are rounde about thee, when I shall execute iudgements in thee, in anger and in wrath, and in sharpe rebukes: I the Lord haue spoken it.
Hivyo Yerusalemu itakuwa jambo kwa watu wengine kushutumu na kufanya mzaha, na chukizo kwa mataifa ambayo yanayowazunguka. Nitafanya hukumu dhidi yenu kwa ghadhabu na hasira, na kwa kukemea kwa hasira-Mimi, Yahwe nimesema hivi!
16 When I shall sende vpon them the euill arrowes of famine, which shalbe for their destruction, and which I will sende to destroy you: and I will encrease the famine vpon you, and wil breake your staffe of bread.
Nitatuma mishale mikali ya njaa juu yenu ambayo itakuwa na maana ya kwamba nitawaharibu. Kwa kuwa nitaongeza njaa juu yenu na kuvunja tegemeo lenu la mkate.
17 So will I send vpon you famine, and euill beastes, and they shall spoyle thee, and pestilence and blood shall passe through thee, and I will bring the sworde vpon thee: I the Lord haue spoken it.
Nitaleta njaa na majanga dhidi yenu hivyo mtakuwa wagumba. Tauni na damu zitapita kati yako, na nitaleta upanga dhidi yenu-Mimi Yahwe, nimesema hivi.”

< Ezekiel 5 >