< Ezekiel 45 >

1 Moreover when yee shall deuide the land for inheritance, ye shall offer an oblation vnto the Lord an holy portion of the land, fiue and twentie thousand reedes long, and ten thousand broad: this shalbe holy in all the borders thereof round about.
Wakati mtakapogawanya nchi kama urithi, mtafanya sadakwa kwa Yahwe; sadaka hiyo itakuwa sehemu takatifu ya nchi, dhiraa elfu ishirini na tano urefu, na dhiraa elfu kumi upana. Patakuwa patakatifu, ndani ya mipaka yake yote.
2 Of this there shalbe for the Sanctuarie fiue hundreth in length with fiue hundreth in breadth, all square round about, and fiftie cubites rounde about for the suburbes thereof.
Kutoka hapa kutakuwa na dhiraa mia tano kwa dhiraa mia tano za mraba kuzunguka mahali patakatifu, kwa kuuzunguka mpaka dhiraa hamsini upana.
3 And of this measure shalt thou measure the length of fiue and twentie thousande, and the breadth of tenne thousande: and in it shalbe the Sanctuarie, and the most holy place.
Kutoka hili eneo utapima fungu ambalo ni dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana; patakuwa patakatifu; mahali patakatifu palipo tukuka.
4 The holy portion of the lande shalbe the Priests, which minister in the Sanctuarie, which came neere to serue the Lord: and it shalbe a place for their houses, and an holy place for the Sanctuarie.
Patakuwa patakatifu katika nchi kwa ajili ya makuhani wanaomtumikia Yahwe, ajaye kwa Yahwe kumtumikia. Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba na eneo takatifu kwa ajili mahali patakatifu.
5 And in the fiue and twentie thousande of length, and the ten thousand of breadth shall the Leuites that minister in the house, haue their possession for twentie chambers.
Hivyo itakuwa dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana, patakuwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika kwenye nyumba.
6 Also ye shall appoynt the possession of the citie, fiue thousand broad, and fiue and twentie thousand log ouer against the oblation of ye holy portion: it shalbe for the whole house of Israel.
Mtadhihirisha eneo moja kwa ajili ya mji, dhiraa elfu tano na urefu ishirini na tano, hapo patakuwa kando kando ya eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu; huu mji utakuwa wa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 And a portion shalbe for the prince on ye one side, and on that side of the oblation of the holy portion, and of the possession of the citie, euen before the oblation of the holy portion, and before the possession of the citie from the West corner Westward, and from the East corner Eastward, and the length shalbe by one of the portions from the West border vnto the East border.
Nchi ya mwana mfalme itakuwa kwa pande zote za eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu na mji. Patakuwa kwa upande wao wa magaharibi na upande wa mashariki. Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu, kutoka magaribi hata mashariki.
8 In this lande shalbe his possession in Israel: and my princes shall no more oppresse my people, and the rest of the land shall they giue to ye house of Israel, according to their tribes.
Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli. Wana wafalme hawatawakandamiza watu wangu; badala yake, watawapatia nchi kwa nyumba ya Israeli, kwa ajili ya makabila yao.
9 Thus saith the Lord God, Let it suffice you, O princes of Israel: leaue off crueltie and oppression, and execute iudgment and iustice: take away your exactions from my people, sayth the Lord God.
Bwana Yahwe asema hivi: Inatosha kwa ajili yenu, mwana mfalme wa Israeli! Ondoa dhuluma na mgogoro; fanya hukumu na haki! Usiwafukuze wapangaji wa watu wangu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
10 Ye shall haue iust balances, and a true Ephah, and a true Bath.
Mtakuwa na mzani sahihi, efa sahihi, na bathi sahihi!
11 The Ephah and the Bath shalbe equall: a Bath shall conteyne the tenth part of an Homer, and an Ephah the tenth part of an Homer: the equalitie thereof shalbe after the Homer.
Efa na bathi zitakuwa kiasi kile kile, ili kwamba bathi iwe zaka ya homeri; efa itakuwa zaka ya hamori moja. Vipimo vyao vitakuwa vinafanana na homeri.
12 And the shekel shalbe twentie gerahs, and twentie shekels, and fiue and twentie shekels and fifteene shekels shalbe your Maneh.
Shekeli zitakuwa gera ishirini, shekeli sita zitakuwa mane yenu.
13 This is the oblation that ye shall offer, ye sixt part of an Ephah of an Homer of wheat, and ye shall giue the sixt part of an Ephah of an Homer of barley.
Hili ndilo toleo mtakalotoa: efa sita kwa kila homeri ya ngano, na mtatoa efa sita kwa kila homeri ya shayiri.
14 Concerning ye ordinance of the oyle, euen of the Bath of oyle, ye shall offer the tenth part of a Bath out of ye Cor (ten Baths are an Homer: for ten Baths fill an Homer)
Sadaka ya kawaida ya mafuta itakuwa zaka ya bathi kwa kila kori (ambazo ni bathi), au kwa kila hamori, kwa kuwa hamori moja ni bathi kumi pia.
15 And one lambe of two hundreth sheepe out of ye fat pastures of Israel for a meat offring, and for a burnt offring and for peace offrings, to make reconciliation for them, sayth the Lord God.
Kondoo mmoja au mbuzi kutoka mifugo kwa kila wanyama mia mbili kutoka malisho ya maji ya mikoa ya Israeli yatatumika kwa sadaka ya kuteketezwa yoyote au sadaka ya amani kufanya upatanisho kwa ajili ya watu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
16 All the people of the lande shall giue this oblation for the prince in Israel.
Watu wote wa nchi watatoa hii sadaka kwa mwana mfalme wa Israeli.
17 And it shalbe ye princes part to giue burnt offrings, and meat offrings, and drinke offrings in the solemne feasts and in the newe moones, and in the Sabbaths, and in all the hie feasts of the house of Israel: he shall prepare the sinne offring, and the meat offring, and the burnt offring, and the peace offrings to make reconciliation for the house of Israel.
Utakuwa wajibu wa mwana mfalme kutoa wanyama kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka ya unga, sadaka ya kinywaji, katika siku za sikukuu na sherehe za mwezi mpya, na katika siku za Sabato-sikukuu zote za kudumu za nyumba ya Israeli. Ataandaa kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za unga, sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani kwa ajili ya upatanisho badala ya nyumba ya Israeli.
18 Thus sayth the Lord God, In the first moneth, in the first day of the moneth, thou shalt take a yong bullocke without blemish and clense the Sanctuarie.
Bwana Yahwe asema hivi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utachukua ng'ombe mmoja asiyekuwa na dosari kutoka kwenye kundi na kufanya sadaka ya dhambi kwa ajili ya patakatifu.
19 And the Priest shall take of the blood of the sinne offring, and put it vpon the posts of the house, and vpon the foure corners of the frame of the altar, and vpon the postes of the gate of the inner court.
Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi na kuiweka juu ya miimo ya mlango na kwenye pembe nne za mpaka wa madhabahu, na miimo ya lango la uzio wa ndani.
20 And so shalt thou doe the seuenth day of the moneth, for euery one that hath erred and for him that is deceiued: so shall you reconcile the house.
Utafanya hivyo siku ya saba ya mwezi kwa dhambi ya kila mtu kwa ajali au ujinga; katika njia hii mtaipatanisha hekalu.
21 In the first moneth in the foureteenth day of the moneth, ye shall haue the Passeouer, a feast of seuen dayes, and ye shall eate vnleauened bread.
Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na sikukuu, sikukuu ya siku saba. Matakula makate usiotiwa chachu.
22 And vpon that day, shall the prince prepare for him selfe, and for all the people of the lande, a bullocke for a sinne offring.
Siku hiyo, mwana mfalme ataandaa ng'ombe kwa ajili yake na kwa ajili ya watu wote wa nchi kama sadaka ya dhambi.
23 And in the seuen dayes of the feast he shall make a burnt offring to the Lord, euen of seuen bullockes, and seuen rammes without blemish dayly for seuen dayes, and an hee goate dayly for a sinne offring.
Kwa siku saba za sikukuu, mwana wa mfalme ataandaa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yahwe: ng'ombe saba na kondoo dume saba zisizokuwa na dosari kila siku kwa mda wa siku saba, na mbuzi dume kila siku kama sadaka ya dhambi.
24 And he shall prepare a meate offring of an Ephah for a bullocke, an Ephah for a ramme, and an Hin of oyle for an Ephah.
Kisha mwana mfalme atatengeneza sadaka ya chakula ya efa moja kwa kila ng'ombe na efa moja kwa kila kondoo dume pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
25 In the seuenth moneth, in the fifteenth day of the moneth, shall he do the like in the feast for seuen dayes, according to the sinne offring, according to the burnt offring, and according to the meate offring, and according to the oyle.
Katika siku ya saba ya mwezi siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu, mwana wa mfalme atafanya matoleo katika siku hizi saba: sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za chakula, na sadaka za mafuta.

< Ezekiel 45 >