< Ezekiel 16 >

1 Again, the worde of the Lord came vnto me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Sonne of man, cause Ierusalem to knowe her abominations,
“Mwanadamu, mwambie Yerusalemu kuhusu machukizo yake,
3 And say, Thus saith the Lord God vnto Ierusalem, Thine habitation and thy kindred is of the land of Canaan: thy father was an Amorite, and thy mother an Hittite.
na useme, 'Bwana Yahwe asema hivi kwa Yerusalemu: Mwanzo wako na kuzaliwa kwako kulichukua nafasi katika nchi ya Kanaani; baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.
4 And in thy natiuitie whe thou wast borne, thy nauell was not cut: thou wast not washed in water to soften thee: thou wast not salted with salt, nor swadled in cloutes.
Katika siku ya kuzaliwa kwako, mama yako hakukata kitovu chako, wala hakukuosha kwenye maji usafishwe au kukuchua kwa chumvi, wala kukusitiri nguo.
5 None eye pitied thee to do any of these vnto thee, for to haue compassion vpon thee, but thou wast cast out in the open fielde to the contempt of thy person in ye day that thou wast borne.
Hakuna jicho lililokuhurumia kufanya haya mambo kwa ajili yako, kukuhurumia wewe. Katika siku uliyozaliwa, kwa kuchukiwa uhai wako, ulitupwa nje uwandani.
6 And when I passed by thee, I saw thee polluted in thine owne blood, and I said vnto thee, whe thou wast in thy blood, Thou shalt liue: euen when thou wast in thy blood, I saide vnto thee, Thou shalt liue.
Lakini nilipita karibu nawe, nalikuona ukijinyonga kwa damu yako mwenyewe, “kubaki hai!”
7 I haue caused thee to multiplie as the bud of the fielde, and thou hast increased and waxen great, and thou hast gotten excellent ornaments: thy breastes are facioned, thine heare is growen, where as thou wast naked and bare.
Nimekufanya ukue kama mmea katika shamba. Umeongezeka na kuwa mkubwa, na umekuwa mzuri wa wazuri. Maziwa yako yakawa thabiti, na nywele zako zikawa nyingi, ingawa ulikuwa uchi huna nguo.
8 Nowe when I passed by thee, and looked vpon thee, beholde, thy time was as the time of loue, and I spred my skirtes ouer thee, and couered thy filthines: yea, I sware vnto thee, and entred into a couenant with thee, saith the Lord God, and thou becamest mine.
Nilipita karibu nawe tena, na nalikuona. Tazama! wakati wa upendo umefika kwako, hivyo nikatandika joho langu juu yako na kufunika uchi wako. Kisha nikaapa kwako na kukuleta kwenye agano-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na ukawa wangu.
9 Then washed I thee with water: yea, I washed away thy blood from thee, and I anointed thee with oyle.
Basi nilikuosha kwa maji na kukufuta damu yako, na kukupaka mafuta.
10 I clothed thee also with broydred worke, and shod thee with badgers skin: and I girded thee about with fine linen, and I couered thee with silke.
Nilikuvalisha nguo ya taraza na kukuwekea makuzi ya ngozi kwenye miguu yako. Nilikufungia kwa kitani kizuri na kukufunika kwa hariri.
11 I decked thee also with ornaments, and I put bracelets vpon thine handes, and a chaine on thy necke.
Kisha nalikupamba kwa vito, na kukuvalisha vikuku kwenye mikono yako, na mkufu kwenye shingo yako.
12 And I put a frontlet vpon thy face, and earings in thine eares, and a beautifull crowne vpon thine head.
Nalitia hazama katika pua yako na hereni katika masikio yako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
13 Thus wast thou deckt with gold and siluer, and thy rayment was of fine linen, and silke, and broydred worke: thou didest eate fine floure, and honie and oyle, and thou wast very beautifull, and thou didest grow vp into a kingdome.
Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, na ulivaa kitani safi, hariri, na ngu za taraza; ulikula unga mzuri, asali, na mafuta, na ulikuwa mzuri sana, na ukawa malkia.
14 And thy name was spred among the heathen for thy beautie: for it was perfite through my beautie which I had set vpon thee, saith the Lord God.
Umaarufu wako ukaenda miongoni mwa mataifa kwa sababu ya uzuri wako, kwa kuwa ulikuwa mkamili katika ukuu niliokuwa nimekupa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 Nowe thou didest trust in thine owne beautie, and playedst the harlot, because of thy renowne, and hast powred out thy fornications on euery one that passed by, thy desire was to him.
Lakini ulitumaini uzuri wako, na ukafanya kama kahaba kwa sababu ya umaarufu wako; umeyamwaga matendo yako ya kikahaba kwa kila aliyepita karibu, ili kwamba uzuri wako uwe wake.
16 And thou didest take thy garments, and deckedst thine hie places with diuers colours, and playedst the harlot thereupon: the like thinges shall not come, neither hath any done so.
Kisha ulichukua nguo zako na pamoja nao umepatengeneza mahali pa juu kwa ajili yako palipambwa kwa rangi tofauti tofauti, na hapo ulifanya kama kahaba. Hii haitatokea. Wala haitatokea.
17 Thou hast also taken thy faire iewels made of my golde and of my siluer, which I had giuen thee, and madest to thy selfe images of men, and didest commit whoredome with them,
Umevichukua vito vizuri vya dhahabu na fedha nilizowapatia, na umejitengenezea sanamu za wanaume, na umefanya pamoja nao ukahaba afanyao.
18 And tookest thy broydred garments, and coueredst them: and thou hast set mine oyle and my perfume before them.
Ulichukua nguo zako za tarizi na kuwafunika, na kuwawekea mafuta yangu na manukato mbele yao.
19 My meate also, which I gaue thee, as fine floure, oyle, and honie, wherewith I fedde thee, thou hast euen set it before them for a sweete sauour: thus it was, saith the Lord God.
Mkate wangu niliokupatia-ulitengenezwa kwa unga mzuri, mafuta, na asali-umeviweka mbele yao kwa ajili ya kunukia harufu nzuri, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyotokea-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 Moreouer thou hast taken thy sonnes and thy daughters, whome thou hast borne vnto me, and these hast thou sacrificed vnto them, to be deuoured: is this thy whoredome a small matter?
Kisha uliwachukua watoto wako ulionizalia, na kuwatoa sadaka kwa picha ili waliwe kama chakula. Je! matendo yako ya kikahaba ni kitu kidogo?
21 That thou hast slaine my children, and deliuered them to cause them to passe through fire for them?
Umewachinja watoto wangu na kuwatupia kwenye moto.
22 And in all thine abominations and whoredomes thou hast not remembred the dayes of thy youth, when thou wast naked and bare, and wast polluted in thy blood.
Katika machukizo yako yote na matendo yako ya kikahaba hukutafakari kuhusu siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi na bila nguo kama kama umepigwa katika damu.
23 And beside all thy wickednes (wo, wo vnto thee, saith the Lord God)
Ole! Ole wako! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwahiyo, zaidi ya hapo kwa haya maovu yote,
24 Thou hast also built vnto thee an hie place, and hast made thee an hie place in euery streete.
umejijengea chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi.
25 Thou hast built thine hie place at euery corner of the way, and hast made thy beautie to be abhorred: thou hast opened thy feete to euery one that passed by, and multiplied thy whoredome.
Umepajenga mahali pako palipoinuka kwenye kichwa cha kila njia na kuunajisi uzuri wako, kwa kuwa umeutoa mwili wako kwa kila mtu apitaye karibu na umefanya matendo mengi zaidi ya ukahaba.
26 Thou hast also committed fornication with the Egyptians thy neighbours, which haue great members, and hast encreased thy whoredome, to prouoke me.
Umetenda kama kahaba pamoja na Wamisri, tamaa ya jirani zako, na umetenda matendo mengi zaidi ya kikahaba, ili kuchochea hasira yangu.
27 Beholde, therefore I did stretche out mine hand ouer thee, and will diminish thine ordinarie, and deliuer thee vnto the will of them that hate thee, euen to the daughters of the Philistims, which are ashamed of thy wicked way.
Tazama! Nitakunyooshea mkono wangu na kupunguza chakula chako. Nitauchukua uhai wako juu ya adui zako, binti za Wafilisti, ambao walikuwa na haya ya tabia yako ya uchafu.
28 Thou hast played the whore also with the Assyrians, because thou wast insaciable: yea, thou hast played the harlot with them, and yet couldest not be satisfied.
Umetenda kama kahaba pamoja na Waashuru kwa sababu hukuweza kuridhika. Umetenda kama kahaba na bado hukuridhika.
29 Thou hast moreouer multiplied thy fornication from the land of Canaan vnto Caldea, and yet thou wast not satisfied herewith.
Umefanya matendo mengi zaidi ya kikahaba katika nchi ya jamii ya wana maji wa Ukaldayo, na wala hukuridhika kwa hayo.
30 Howe weake is thine heart, saith the Lord God, seeing thou doest all these thinges, euen the worke of a presumptuous whorish woman?
Jinsi moyo wako ulivyo dhaifu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwamba utaweza kuyafanya haya mambo yote, matendo ya aibu ya kikahaba?
31 In that thou buildest thine hie place in the corner of euery way, and makest thine hie place in euery streete, and hast not bene as an harlot that despiseth a reward,
Mmepajenga mahali penu pa juu kwenye kichwa cha kila mtaa na kufanya chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi. Bado hukuwa kama kahaba kwa sababu ulikataa kulipwa ujira.
32 But as a wife that playeth the harlot, and taketh others for her husband:
Wewe mwanamke mzinifu, wewe upokeaye wageni badala ya mume wako.
33 They giue giftes to all other whores, but thou giuest giftes vnto all thy louers, and rewardest them, that they may come vnto thee on euery side for thy fornication.
Watu hulipa kwa kila kahaba, lakini wewe huwapa mshara wako wapenzi wako wote na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote kwa matendo yako ya kikahaba.
34 And the contrary is in thee from other women in thy fornications, neither the like fornication shall be after thee: for in that thou giuest a rewarde, and no reward is giuen vnto thee, therefore thou art contrary.
Hivyo kuna tofauti kati yako na hao wanawake wengine, kwa kuwa hakuna hata mmoja ajaye kwako kukuuliza kulala pamoja nao. Badala yake, unawalipa. Hakuna akulipaye.
35 Wherefore, O harlot, heare the worde of the Lord.
Kwa hiyo, wewe kahaba, lisikilize neno la Yahwe.
36 Thus sayeth the Lord God, Because thy shame was powred out, and thy filthinesse discouered through thy fornications with thy louers, and with all the idoles of thine abominations, and by the blood of thy children, which thou didest offer vnto them,
Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umemwaga tamaa yako na kuonyesha sehemu zako za siri kupitia matendo yako ya ukahaba pamoja na wapenzi wako wote pamoja na sanamu zako za chukizo, na kwa sababu ya damu ya watoto wako uliyowapatia sanamu zako,
37 Beholde, therefore I wil gather all thy louers, with whom thou hast taken pleasure, and all them that thou hast loued, with al them that thou hast hated: I will euen gather them round about against thee, and will discouer thy filthines vnto them, that they may see all thy filthines.
kwa hiyo, tazama! Nitawakusanya wapenzi wako wote uliokutana nao, wote ambao uliowapenda na wote uliowachukia, na nitawakusanya juu yako kila upande. Nitawaonyesha wazi sehemu zako za siri hivyo wanaweza kuona uchi wako wote.
38 And I wil iudge thee after ye maner of them that are harlots, and of them that shead blood, and I wil giue thee the blood of wrath and ielousie.
Kwa kuwa nitakuadhibu kwa uasherati na kumwaga damu, na nitaleta juu yako damu ya hasira yangu na hasira kali.
39 I will also giue thee into their handes, and they shall destroy thine hie place, and shall breake downe thine hie places. they shall strippe thee also out of thy clothes, and shall take thy faire iewels, and leaue thee naked and bare.
Nitakutia kwenye mikono yao hivyo watakutupa chini kwenye chumba cha chini kwa chini na kupavunja mahali pako pa juu na watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vyote. watakuacha uchi bila nguo.
40 They shall also bring vp a company against thee, and they shall stone thee with stones, and thrust thee through with their swordes.
Kisha wataleta kundi la watu juu yako na kukupiga kwa mawe, na kukukata kwa panga zao.
41 And they shall burne vp thine houses with fire, and execute iudgements vpon thee in the sight of many women: and I will cause thee to cease from playing the harlot, and thou shalt giue no reward any more.
Watachoma nyumba zako na kufanya matendo mengi ya adhabu juu yako kwenye uso wa wanawake wengi, kwa kuwa nitakusimamisha ukahaba wako, na hutawalipa tena wapenzi wako.
42 So will I make my wrath towarde thee to rest, and my ielousie shall depart from thee, and I will cease and be no more angrie.
Kisha nitatuliza ghadhabu yangu juu yako; hasira yangu itakuacha, kwa kuwa nitaridhika, na sitakuwa na hasira tena.
43 Because thou hast not remembred the dayes of thy youth, but hast prouoked me with all these things, behold, therefore I also haue brought thy way vpon thine head, sayeth the Lord God: yet hast not thou had consideration of all thine abominations.
Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako na kunifanya nitetemeke kwa hasira kwa sababu ya haya mambo yote, kwa hiyo, tazama! Mimi mwenyewe nitashusha kwa kichwa chako mwenyewe adhabu kwa kile ulichokifanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Hutaongeza ukahaba kwa matendo yako yote ya machukizo?
44 Beholde, all that vse prouerbes, shall vse this prouerbe against thee, saying, As is the mother, so is her daughter.
Tazama! Kila mtu azungumzaye Mithali kuhusu wewe atasema, “Kama alivyo, hivyo pia ni binti yake.”
45 Thou art thy mothers daughter, that hath cast off her husband and her children, and thou art the sister of thy sisters, which forsooke their husbands and their children: your mother is an Hittite, and your father an Amorite.
Wewe ni binti wa mama yako, amchukiaye mume wake na mtoto wake, na wewe ni dada wa dada zako aliyewachukia waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
46 And thine elder sister is Samaria, and her daughters, that dwell at thy left hand, and thy yong sister, that dwelleth at thy right hand, is Sodom, and her daughters.
Dada yako mkubwa alikuwa Samaria na binti zake walikuwa wale waliokuwa wakiishi kaskazini, wakati dada yako mdogo alikuwa ni yule aliyekuwa akiishi kusini mwako, ambaye ni, Sodoma na binti zake.
47 Yet hast thou not walked after their wayes, nor done after their abominations: but as it had bene a very little thing, thou wast corrupted more then they in all thy wayes.
Hukuenenda katika njia zao na kuchukua tabia zao na matendo yao, lakini katika njia zako zote ulikuwa mbaya zaidi kuliko walivyokuwa wao.
48 As I liue, saith the Lord God, Sodom thy sister hath not done, neither shee nor her daughters, as thou hast done and thy daughters.
Kama niishivyo- hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-dada yako Sodoma na binti zake, hawajafanya uovu mwingi kama wewe ulivyofanya na binti zako walivyofanya.
49 Beholde, this was the iniquitie of thy sister Sodom, Pride, fulnesse of bread, and aboundance of idlenesse was in her, and in her daughters: neither did shee strengthen the hande of the poore and needie.
Tazama! Hii ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: Alikuwa na kiburi katika mafanikio yake, uzembe na kutojali kuhusu chochote. Hakuitia nguvu mikono ya maskini na watu wahitaji.
50 But they were hautie, and committed abomination before mee: therefore I tooke them away, as pleased me.
Alikuwa na kiburi na kufanya machukizo mbele yangu, hivyo niliwatoa kama nilivyoona.
51 Neither hath Samaria committed halfe of thy sinnes, but thou hast exceeded them in thine abominations, and hast iustified thy sisters in all thine abominations, which thou hast done.
Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi zako; badala yake, umefanya machukizo mengi kuliko walivyofanya, na umewonyesha hayo dada zako walikuwa bora kuliko wewe kwa sababu ya machukizo yako uyafanyayo!
52 Therefore thou which hast iustified thy sisters, beare thine owne shame for thy sinnes, that thou hast committed more abominable then they which are more righteous then thou art: be thou therefore confounded also, and beare thy shame, seeing that thou hast iustified thy sisters.
Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe; kwa njia hii umewaonyesha dada zako walikuwa bora kuliko wewe, kwa sababu ya dhambi ulizozifanya katika hayo machukizo yako yote. Dada zako sasa wanaonekana bora kuliko wewe. Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe, kwa njia hii umewaonyesha kwamba dada zako walikuwa bora kuliko wewe.
53 Therefore I will bring againe their captiuitie with the captiuitie of Sodom, and her daughters, and with the captiuitie of Samaria, and her daughters: euen the captiuitie of thy captiues in the middes of them,
Kwa kuwa nitarudisha masalia wao-masalia ya Sodoma na binti zake, na masalia ya Samaria na binti zake; lakini masalia yako yatakuwa miongoni mwao.
54 That thou mayest beare thine owne shame, and mayest bee confounded in all that thou hast done, in that thou hast comforted them.
Kwa kufikiria haya mambo utaonyesha aibu yako; utakuwa mnyenyekevu kwa sababu ya kila kitu ulichokifanya, na kwa njia hii utakuwa faraja kwao.
55 And thy sister Sodom and her daughters shall returne to their former state: Samaria also and her daughters shall returne to their former state, when thou and thy daughters shall returne to your former state.
Hivyo dada yako Sodoma na binti zake watarudishwa kwenye hali yao ya zamani, na Samaria na binti zake watarudishwa kwenye mashamba yao ya zamani. Kisha wewe na binti zako watarudishwa kwenye hali yako ya kawaida.
56 For thy sister Sodom was not heard of by thy report in the day of thy pride,
Sodoma dada yako hakutajwa hata kwa kinywa chako katika siku ulipojiinua,
57 Before thy wickednes was discouered, as in that same time of the reproch of the daughters of Aram, and of all the daughters of the Philistims round about her which despise thee on all sides.
kabla uovu wako haujafunuliwa. Lakini sasa wewe ni kitu cha dharau kwa binti za Edomu na binti wote wa Wafilisti waliomzunguka. Watu wote wanakudharau wewe.
58 Thou hast borne therefore thy wickednesse and thine abomination, saith the Lord.
Utaonyesha aibu yako na matendo yako ya machukizo! -hivi ndivyo Yahwe asemavyo!
59 For thus saith the Lord God, I might euen deale with thee, as thou hast done: when thou didest despise the othe, in breaking the couenant.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitashughulika na wewe kama unavyostahili, wewe uliyedharau kiapo chako kwa kulivunja agano.
60 Neuerthelesse, I wil remember my couenant made with thee in ye dayes of thy youth, and I wil confirme vnto thee an euerlasting couenant.
Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nitaliimarisha agano la milele pamoja na wewe.
61 Then thou shalt remember thy wayes, and be ashamed, when thou shalt receiue thy sisters, both thy elder and thy yonger, and I will giue them vnto thee for daughters, but not by thy couenat.
Kisha utazikumbuka njia zako na kuona aibu utakapo wapokea dada zako wakubwa na dada zako wadogo. Nitakupatia wao kama binti zako, lakini kwa sababu ya agano lako.
62 And I wil establish my couenant with thee, and thou shalt knowe that I am the Lord,
Mimi nitaweka imara agano lango pamoja nawe, nawe utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
63 That thou mayest remember, and be ashamed, and neuer open thy mouth any more: because of thy shame when I am pacified toward thee, for all that thou hast done, saith the Lord God.
Kwa sababu ya haya mambo, utakumbuka kila kitu na kuona aibu, hutafungua mdomo wako tena kuongea kwa sababu ya aibu yako, wakati nitakapokusamehe kwa yale yote uliyoyafanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'

< Ezekiel 16 >