< Ezekiel 14 >

1 Then came certaine of the Elders of Israel vnto me, and sate before me.
Baadhi ya viongozi wa Israeli wakaja kwangu na kuketi mbele yangu.
2 And the worde of the Lord came vnto me, saying,
Ndipo neno la Yahwe likanijia, likisema,
3 Sonne of man, these men haue set vp their idoles in their heart, and put the stumbling blocke of their iniquitie before their face: should I, being required, answere them?
“Mwanadamu, hawa watu wamchukua sanamu zao kwenye mioyo yao na kuweka pingamizi la uovu wao mbele ya nyuso zao wenyewe. Je naweza kuulizwa yote na wao?
4 Therefore speake vnto them, and say vnto them, Thus saith the Lord God, Euery man of the house of Israel that setteth vp his idols in his heart, and putteth the stumbling blocke of his iniquitie before his face, and commeth to the Prophet, I the Lord will answere him that commeth, according to the multitude of his idoles:
Kwa hiyo watangazie hivi na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kila mtu wa nyumba ya Israeli achukuaye sanamu moyoni mwake, au awekeye pingamizi la uovu mbele ya uso wake, na kisha yule ajaye kwa nabii-Mimi, Yahwe, nitamjibu kulingana na sanamu zake.
5 That I may take the house of Israel in their owne heart, because they are all departed from me through their idoles.
Nitafanya hivi ili kwamba niweze kuirudisha nyumba ya Israeli katika mioyo yao ambayo ilikuwa mbali nami kwa ajili ya sanamu zao.'
6 Therfore say vnto the house of Israel, Thus sayth the Lord God, Returne, and withdraw your selues, and turne your faces from your idoles, and turne your faces from all your abominations.
Kwa hiyo sema kwa nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tubuni na rudini kutoka kwenye sanamu zenu! Rudisheni nyuma nyuso zenu kutoka kwenye kachukizo yenu yote.
7 For euery one of the house of Israel, or of the stranger that soiourneth in Israel, which departeth from mee, and setteth vp his idoles in his heart, and putteth the stumbling blocke of his iniquitie before his face, and commeth to a Prophet, for to inquire of him for me, I the Lord will answere him for my selfe,
Kwa kuwa kila mmoja kutoka kwenye nyumba ya Israeli na kila mmoja wa wageni wanaoishi katika Israeli ajitengaye nami, achukuaye sanamu zake kwenye moyo wake na kuweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake mwenyewe, na kisha yule ajaye kwa nabii kunitafuta-mimi, Yahwe, nitamjibu mimi mwenyewe.
8 And I will set my face against that man, and will make him an example and prouerbe, and I will cut him off from the middes of my people, and ye shall knowe that I am the Lord.
Hivyo nitauweka uso wangu juu ya huyo mtu na kumfanya ishara na mithali, kwa kuwa nitamkata kutoka kati ya watu wangu, na mtajua kuwa mimi ni Yahwe.
9 And if the Prophet be deceiued, when hee hath spoken a thing, I the Lord haue deceiued that Prophet, and I will stretch out mine hande vpon him, and will destroy him from the middes of my people of Israel.
Kama nabii atadanganywa na kuongea ujumbe, kisha Mimi Yahwe, nitamdanganya huyo nabii; Nitanyoosha mkono wangu na kumwangamizaku toka kati watu wangu Israeli.
10 And they shall beare their punishment: the punishment of the Prophet shall bee euen as the punishment of him that asketh,
Watabeba uovu wao wenyewe; uwovu wa nabii utakua uleule kama uovu wa yule aulizaye kutoka kwake.
11 That the house of Israel may go no more astray from mee, neither bee polluted any more with all their transgressions, but that they may be my people, and I may be their God, sayth the Lord God.
Kwa sababu hiyo basi, nyumba ya Israeli haitaenda mbali kutoka kunifuata mimi wala kujinajisi wenyewe kupitia dhambi zao zote. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao-hivi ndivyo Yahwe asemavyo.”'
12 The worde of the Lord came againe vnto me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
13 Sonne of man, when ye land sinneth against me by committing a trespasse, then will I stretch out mine hand vpon it, and will breake the staffe of the bread thereof, and will send famine vpon it, and I will destroy man and beast forth of it.
“Mwanadamu, wakati nchi itakapo asi dhidi yangu kwa kufanya dhambi ili kwamba ninyooshe mkono wangu dhidi yake na kuvunja tegemea la mkate wake, na kuleta njaa juu yake na kukata mnyama kutoka kwenye nchi;
14 Though these three men Noah, Daniel, and Iob were among them, they shoulde deliuer but their owne soules by their righteousnes, saith the Lord God.
kisha hata kama hawa watu watatu-Nuhu, Danieli, na Ayubu-walikuwa katikati ya nchi, wangeweza kuokoa maisha yao wenyewe kwa haki-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 If I bring noysome beastes into the lande and they spoyle it, so that it bee desolate, that no man may passe through, because of beastes,
Kama nikileta wanyama waovu kwenye nchi na kuwafanya wasizae hivyo basi itakuwa hakuna mtu asiweze kupita kwa sababu ya hao wanyama,
16 Though these three men were in the mids thereof, As I liue, sayth the Lord God, they shall saue neither sonnes nor daughters: they onely shalbe deliuered, but the land shall be waste.
kisha hata kama watu hawa hawa watatu ndani yake-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa hata watoto wao wala binti; isipokuwa maisha yao yataokoka, lakini nchi itakuwa ukiwa.
17 Or if I bring a sworde vpon this land, and say, Sword, go through the land, so that I destroy man and beast out of it,
Au nikileta upanga juu ya hiyo nchi na kusema, 'Upanga, nenda kwenye nchi na wakate wote mtu na mnyama kutoka huo',
18 Though these three men were in the mids thereof, As I liue, sayth the Lord God, they shall deliuer neither sonnes nor daughters, but they onely shall be deliuered themselues.
kisha hata kama hawa watu watatu watakuwa katikatai ya nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa japo watoto wao wala binti; ila tu maisha yao wenyewe yangeokolewa.
19 Or if I send a pestilence into this land, and powre out my wrath vpon it in blood, to destroy out of it man and beast,
Au kama nikipeleka tauni juu ya nchi na kumwaga dhahabu yangu juu yake kwa damu, ili kuwakata mtu na mnyama,
20 And though Noah, Daniel and Iob were in the middes of it, As I liue, sayth the Lord God, they shall deliuer neither sonne nor daughter: they shall but deliuer their owne soules by their righteousnes.
kisha hata kama Nuhu, Danieli, na Ayubu wangekuwa kwenye hiyo nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuokoa hata watoto wao au binti; maisha yao pekee yangeokoka kwa haki.
21 For thus saith the Lord God, Howe much more when I sende my foure sore iudgements vpon Ierusalem, euen the sworde, and famine, and the noysome beast and pestilence, to destroy man and beast out of it?
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: hakika nitafanya mambo makali sana kwa kuleta adhabu zangu nne-njaa, upanga, wanyama wa porini, na tauni-juu ya Yerusalemu kuwakata wote mtu na mnyama kutoka kwake.
22 Yet beholde, therein shalbe left a remnant of them that shalbe caryed away both sonnes and daughters: behold, they shall come forth vnto you, and ye shall see their way, and their enterprises: and ye shall be comforted, concerning the euill that I haue brought vpon Ierusalem, euen concerning al that I haue brought vpon it.
Kisha, tazama! mabaki yatasalia kwake, watakaokoka wataenda pamoja na wana na binti. Tazama! Watawatokea, na mtaona njia zao na matendo yao yakiwafariji kuhusu adhabu niliyoipeleka Yerusalemu, na kuhusu kila kitu kingine ambacho nilichopeleka juu ya nchi.
23 And they shall comfort you, when yee see their way and their enterprises: and ye shall know, that I haue not done without cause all that I haue done in it, saith the Lord God.
Waliokoka watawafariji ninyi mtakapoona njia zao na matendo yao, hivyo mtayajua haya mambo niliyoyafanya juu yake, kwamba sijayafanya bure! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 14 >