< Exodus 35 >

1 Then Moses assembled all the Congregation of the children of Israel, and sayd vnto them, These are the wordes which the Lord hath commanded, that ye should do them:
Musa akawakusanya jamii yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndio mambo Yahweh aliyo waamuru mfanye.
2 Six dayes thou shalt work, but the seuenth day shall bee vnto you the holy Sabbath of rest vnto the Lord: whosoeuer doth any worke therein, shall die.
Kwa siku sita kazi ya weza fanywa, lakini kwako, siku ya saba lazima iwe siku takatifu, siku ya Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Yahweh. Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe.
3 Ye shall kindle no fire throughout all your habitations vpon the Sabbath day.
Haupaswi kuwasha moto kwenye nyumba zenu siku ya Sabato.”
4 Againe, Moses spake vnto all the Congregation of the children of Israel, saying, This is the thing which the Lord commandeth, saying,
Musa akasema na jamii yote ya Waisraeli, kwa kusema, “Hichi ndicho kitu Yahweh alicho amuru.
5 Take from among you an offering vnto the Lord: whosoeuer is of a willing heart, let him bring this offring to the Lord, namely golde, and siluer, and brasse:
Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh, wote wenye moyo mkunjufu. Leta sadaka kwa Yahweh - dhahabu, fedha, shaba,
6 Also blewe silke, and purple, and skarlet, and fine linen, and goates heare,
buluu, zambarau, sufu nyekundu na kitambaa kizuri; nywele za mbuzi;
7 And rams skins died red, and badgers skins with Shittim wood:
ngozi za kondoo zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo; na mbao za mshita;
8 Also oyle for light, and spices for the anointing oyle, and for the sweete incense,
mafuta ya taa kwa pahali patakatifu, viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa,
9 And onix stones, and stones to be set in the Ephod, and in the brest plate.
kwa uvumba mzuri na vito vya shohamu na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani.
10 And all the wise hearted among you, shall come and make all that the Lord hath commanded:
Kila mwanaume mwenye ustadi kati yenu aje na afanye kila kitu ambacho Yahweh aliyaamuru —
11 That is, the Tabernacle, that pauilion thereof, and his couering, and his taches and his boards, his barres, his pillars and his sockets,
hema la kuabudia, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, nguzo, na sakafu;
12 The Arke, and the barres thereof ye Merci-seate, and the vaile that couereth it,
pia sanduku na nguzo zake, kiti cha rehema, na pazia la kusitiri.
13 The Table, and the barres of it, and all the instruments thereof, and the shewe bread:
Walileta meza na miguu yake, vyombo vyake vyote, na mkate wa wonyesho;
14 Also the Candlesticke of light and his instruments, and his lampes with the oyle for the light:
kinara cha taa, vyombo vyake, taa, na mafuta ya zile taa;
15 Likewise the Altar of perfume and his barres, and the anoynting oyle, and the sweete incense, and the vaile of the doore at the entring in of the Tabernacle,
ile madhabahu ya uvumba na nguzo zake, mafuta ya upako na uvumba ulitiwa maukato; kishikizo cha mwingilio wa hema ya kuabudia;
16 The Altar of burnt offering with his brasen grate, his barres and all his instruments, the Lauer and his foote,
madhabahu ya sadaka ya kuteketeza na kitunzi cha shaba na nguzo na vyombo; na ile beseni kubwa na sakafu yake.
17 The hangings of the court, his pillars and his sockets, and the vaile of the gate of the court,
Walileta vishikizo kwa ajili ya nyuani na nguzo zake na sakafu yake, na pazia kwa ajili mwingilio wa nyauni;
18 The pinnes of the Tabernacle, and the pinnes of the court with their cordes,
na ile misumari ya hema la kuabudia na nyuani, pamoja na kamba zake.
19 The ministring garments to minister in the holy place, and the holy garments for Aaron the Priest, and the garmentes of his sonnes, that they may minister in the Priests office.
Walileta mavazi yaliyofumwa kutumikia sehemu takatifu, mavazi takatifu ya Aruni kuhani na wanae, kwa wao kutumika kama makuhani.”
20 Then all the Congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
Kisha makabila yote ya Israeli yakaondoka na kwenda kutoka uweponi mwa Musa.
21 And euery one, whose heart encouraged him, and euery one, whose spirit made him willing, came and brought an offring to the Lord, for the worke of the Tabernacle of the Congregation, and for all his vses, and for the holy garments.
Kila mtu moyo wake ulimchochea na aliye andaliwa na roho yake alikuja na kuleta sadaka kwa Yahweh kwa matengenezo ya hema ya kuabudia, kwa vitu vyote kwajili ya huduma ndani yake, na kwa vazi takatifu.
22 Both men and women, as many as were free hearted, came and brought taches and earings, and rings, and bracelets, all were iewels of golde: and euery one that offered an offring of gold vnto the Lord:
Walikuja, wote wanaume kwa wanawake, wote waliokuwa na moyo wa utayari. Walileta madini, hereni, pete, na vitu vya thamani, vitu vyote tofauti vyenye madini ya dhahabu. Waliwasilisha sadaka za dhahabu kama sadaka ya kupunga kwa Yahweh.
23 Euery man also, which had blewe silke, and purple, and skarlet, and fine linen, and goates heare, and rammes skinnes died red, and badgers skins, brought them.
Kila mmoja alikuwa na sufu ya buluu, dhambarau, au nyekundu, nguo nzuri, singa za mbuzi, ngozi za kondoo zilizobadili kuwa nyekundu, na ngozi ya pomboo walivileta.
24 All that offered an oblation of siluer and of brasse, brought the offring vnto the Lord: and euery one, that had Shittim wood for any maner worke of the ministration, brought it.
kila mmoja alitengeneza sadaka ya fedha au shaba walizileta kama sadaka kwa Yahweh, na kila mmoja aliyekuwa na mti wa mshita kwa matumizi ya kazi aliuleta.
25 And all the women that were wise hearted, did spin with their hands, and brought ye spun worke, euen the blewe silke, and the purple, the skarlet, and the fine linen.
kila mwanamke mwenye ustadi walisokota sufu kwa mikono yao na walileta sufu walizosokota za buluu, dhambarau, au sufu nyekundu, au nguo nzuri.
26 Likewise al the women, whose hearts were moued with knowledge, spun goates heare.
Wanawake wote wenye mioyo iliyochochewa na walio na ustadi walisokota singa za mbuzi.
27 And ye rulers brought onix stones, and stones to be set in the Ephod, and in the brest plate:
Viongozi walileta mawe ya shohamu na mawe mengine kwaajili ya kuwekwa kwenye hiyo naivera na hicho kifuko cha kifuani;
28 Also spice, and oyle for light, and for the anoynting oyle, and for the sweete perfume.
walileta viungo na mafuta kwaajili ya taa, kwa mafuta ya upako, na kwa uvumba wa manukato.
29 Euery man and woman of the children of Israel, whose hearts moued the willingly to bring for all the worke which the Lord had commanded the to make by the hand of Moses, brought a free offring to the Lord.
Waisraeli walileta sadaka ya hiyari kwa Yahweh; kila mwanaume na mwanamke ambao mioyo yao ilikuwa tayari walileta vifaa kwaajili kazi zote ambazo Yahweh aliamuru kupitia Musa zifanyike.
30 Then Moses sayde vnto the children of Israel, Beholde, the Lord hath called by name Bezaleel the sonne of Vri, the sonne of Hur of the tribe of Iudah,
Musa alisema kwa waisraeli, “Tazama, Yahweh ameita kwa jina juu ya Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, kutoka kabila la Yuda.
31 And hath filled him with an excellent spirit of wisdome, of vnderstanding, and of knowledge, and in all maner worke,
Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake, kumpa hekima, uwelewa, na maarifa, kwa aina zote za ujenzi,
32 To finde out curious workes, to worke in golde, and in siluer, and in brasse,
kufanya sanaa ya ubunifu na kufanya kazi za dhahabu, shaba, na shaba;
33 And in grauing stones to set them, and in karuing of wood, euen to make any maner of fine worke.
pia kukata na kupanga mawe na mbao iliochongwa- kufanya kazi za aina zote kwa ubunifu na ujenzi.
34 And he hath put in his heart that hee may teach other: both hee, and Aholiab the sonne of Ahisamach of the tribe of Dan:
Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake, yeye pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani.
35 Them hath he filled with wisdome of heart to worke all maner of cunning and broidred, and needle worke: in blewe silke, and in purple, in skarlet, and in fine linnen and weauing, euen to do all maner of worke and subtill inuentions.
Aliwajaza kwa ustadi wa kufanya kazi za aina zote, kufanya kazi ya kama kuchora mawe, kama mwerevu, kama mtia taraza katika nyuzi za rangu ya buluu, dhambarau, na nyekundu na nguo nzuri, na kama washonaji. Walikuwa wachonga mawe wa kazi zote, na walikuwa wabunifu wa sanaa.

< Exodus 35 >