< Exodus 32 >

1 Bvt when the people sawe, that Moses taryed long or he came downe from the mountaine, the people gathered themselues together against Aaron, and sayde vnto him, Vp, make vs gods to goe before vs: for of this Moses (the man that brought vs out of the land of Egypt) we knowe not what is become of him.
Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Aruni, wakamwambia, “Njoo, katufanyizie sanamu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”
2 And Aaron said vnto them, Plucke off the golden earings, which are in the eares of your wiues, of your sonnes, and of your daughters, and bring them vnto me.
Hivyo Aruni akawaambia, “Zitoeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.”
3 Then all ye people pluckt from them selues the golden earings, which were in their eares, and they brought them vnto Aaron.
Watu wote wakavua pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, na wakamletea Aruni.
4 Who receiued them at their handes, and facioned it with the grauing toole, and made of it a molte calfe: then they said, These be thy gods, O Israel, which brought thee out of ye lad of Egypt
Akapoke mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha. Nao wakasema, “Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”
5 When Aaron sawe that, he made an Altar before it: and Aaron proclaimed, saying, To morow shalbe the holy day of the Lord.
Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Aruni akatangaza akasema,
6 So they rose vp the next day in the morning, and offred burnt offerings, and brought peace offrings: also the people sate them downe to eate and drinke, and rose vp to play.
“Kesho itakuwa sikukuu kwa Yahweh.” Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
7 Then the Lord said vnto Moses, Go, get thee downe: for thy people which thou hast brought out of the land of Egypt, hath corrupted their wayes.
Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Shuka upesi, kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao.
8 They are soone turned out of the way, which I commanded them: for they haue made them a molten calfe and haue worshipped it, and haue offered thereto, saying, These be thy gods, O Israel, which haue brought thee out of the lande of Egypt.
Wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu. Wakasema, 'Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
9 Againe the Lord said vnto Moses, I haue seene this people, and beholde, it is a stiffe necked people.
Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.
10 Nowe therefore let mee alone, that my wrath may waxe hote against them, for I wil consume the: but I wil make of thee a mighty people.
Basi sasa usinizuie. Ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize. Nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.”
11 But Moses praied vnto the Lord his God, and said, O Lord, why doeth thy wrath waxe hote against thy people, which thou hast brought out of the lande of Egypt, with great power and with a mightie hand?
Musa akamsihi sana Yahweh Mungu wake, na kusema,”Yahweh, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
12 Wherefore shall the Egyptians speake, and say, He hath brought them out maliciously for to slay them in the mountaines, and to consume them from the earth? turne from thy fearce wrath, and change thy minde from this euill towarde thy people.
Kwa nini Wamisri kusema, 'Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi?' Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
13 Remember Abraham, Izhak, and Israel thy seruants, to whom thou swarest by thine owne selfe, and saydest vnto them, I wil multiply your seede, as the starres of the heauen, and all this land, that I haue spoken of, wil I giue vnto your seede, and they shall inherit it for euer.
Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, 'Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.'”
14 Then the Lord changed his minde from the euil, which he threatned to do vnto his people.
Na Yahweh akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.
15 So Moses returned and went downe from the mountaine with the two Tables of the Testimonie in his hande: the Tables were written on both their sides, euen on the one side and on the other were they written.
Kisha Musa akageuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake. Mbao zilizoandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa.
16 And these Tables were the worke of God, and this writing was the writing of God grauen in the Tables.
Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
17 And when Ioshua heard the noyse of the people, as they shouted, he said vnto Moses, There is a noyse of warre in the hoste.
Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, “Kuna kelele ya vita kambini.
18 Who answered, It is not the noyse of them that haue the victorie, nor the noyse of them that are ouercome: but I do heare ye noyse of singing.
“Lakini Musa akasema, “Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao ndizo ninazozisikia mimi.”
19 Nowe, as soone as he came neere vnto the hoste, he sawe the calfe and the dancing: so Moses wrath waxed hote, and he cast the Tables out of his handes, and brake them in pieces beneath the mountaine.
Hata alipoyakaribia kambini akaiona ile ndama, na watu wakicheza. Hasira ya Musa ikawaka. Akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima.
20 After, he tooke the calfe, which they had made, and burned it in the fire, and ground it vnto powder, and strowed it vpon the water, and made the children of Israel drinke of it.
Akaitwaa ile ndama waliyoifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji. Akawanywesha wana wa Israeli.
21 Also Moses said vnto Aaron, What did this people vnto thee, that thou hast brought so great a sinne vpon them?
Musa akamwambia Aruni, “Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao?
22 Then Aaron answered, Let not the wrath of my Lord waxe fearce: Thou knowest this people, that they are euen set on mischiefe.
Aruni akasema, “Hasira yako isiwake, bwana wangu. Wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya.
23 And they sayde vnto me, Make vs gods to go before vs: for we knowe not what is become of this Moses (the man that brought vs out of the land of Egypt.)
Maana waliniambia, 'Katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu. Kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.'
24 Then I sayde to them, Ye that haue golde, plucke it off: and they brought it me, and I did cast it into the fire, and thereof came this calfe.
Nikawaambia, 'Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivue; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.”
25 Moses therefore sawe that the people were naked (for Aaron had made them naked vnto their shame among their enemies)
Basi Musa alipoona ya kuwa watu hawa wameasi (maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao)
26 And Moses stoode in ye gate of the campe, and sayde, Who pertaineth to the Lord? let him come to mee. And all the sonnes of Leui gathered themselues vnto him.
Ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, “Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh na aje kwangu.” Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia.
27 Then he said vnto them, Thus sayth ye Lord God of Israel, Put euery man his sworde by his side: go to and from, from gate to gate, through the hoste, and slay euery man his brother, and euery man his companion, and euery man his neighbour.
Akawaambia, Yahweh, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake.'”
28 So the children of Leui did as Moses had commanded: and there fel of the people the same day about three thousand men.
Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.
29 (For Moses had said, Cosecrate your hands vnto the Lord this day, euen euery man vpon his sonne, and vpon his brother, that there may be giuen you a blessing this day)
Musa akasema, Jiwekeni wakfu kwa Yahweh leo, kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake; ili Yahweh awape baraka leo.”
30 And when the morning came, Moses sayde vnto the people, Yee haue committed a grieuous crime: but now I wil goe vp to the Lord, if I may pacifie him for your sinne.
Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, “Mmetenda dhambi kuu. Sasa nitakwenda juu kwa Yahweh. Labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
31 Moses therefore went againe vnto ye Lord, and said, Oh, this people haue sinned a great sinne, and haue made them gods of golde.
Musa akarejea kwa Yahweh akasema,” Oh! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
32 Therefore now if thou pardon their sinne, thy mercy shall appeare: but if thou wilt not, I pray thee, rase me out of thy booke, which thou hast written.
Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.”
33 Then the Lord sayd to Moses, Whosoeuer hath sinned against me, I will put out of my booke.
Yahweh akamwambia Musa, “Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
34 Go nowe therefore, bring the people vnto the place which I commanded thee: behold, mine Angel shall goe before thee, but yet in the day of my visitation I wil visite their sinne vpon them.
Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake. Tazama, malaika wangu atakutangulia. Lakini pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.”
35 So the Lord plagued the people, because they caused Aaron to make ye calfe which he made.
Kisha Yahweh akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Aruni aliifanya.

< Exodus 32 >