< Exodus 3 >

1 When Moses kept the sheepe of Iethro his father in lawe, Priest of Midian, and droue the flocke to the backe side of the desert, and came to the Mountaine of God, Horeb,
Wakati huu Musa aliendelea kuchunga mifugo ya Yethro baba mkwe wake, kuhani wa Midiani. Musa aliliongoza kundi la mifugo kuelekea upande wa mbali wa jangwa mpaka kufika Horebu, mlima wa Mungu.
2 Then the Angel of the Lord appeared vnto him in a flame of fire, out of the middes of a bush: and he looked, and behold, the bush burned with fire, and the bush was not consumed.
Akiwa pale malaika wa Yahwe akamtokea kama mwali wa moto katika kichaka. Musa aliangalia, na tazama, kichaka kiliwaka moto lakini hakikuteketea.
3 Therefore Moses saide, I will turne aside nowe, and see this great sight, why the bush burneth not.
Musa akasema, “Nitageuka ili nione kitaku hiki cha ajabu, kwa nini kichaka hakiteketei.”
4 And when the Lord sawe that he turned aside to see, God called vnto him out of the middes of the bush, and said, Moses, Moses. And he answered, I am here.
Yahwe alipoona ya kuwa amegeuka upande ili aone, Mungu alimwita kutoka katika kile kichaka na kusema, “Musa, Musa.” Musa akasema, “Mimi hapa.”
5 Then he saide, Come not hither, put thy shooes off thy feete: for the place whereon thou standest is holy ground.
Mungu akasema, “Usinikaribie! Vua viatu katika miguu yako, kwa kuwa mahali uliposimama ni mahali palipowekwa wakfu kwa ajili yangu.”
6 Moreouer he saide, I am the God of thy father, the God of Abraham, the God of Izhak, and the God of Iaakob. Then Moses hid his face: for he was afraid to looke vpon God.
Aliongeza kusema, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Kisha Musa akaufunika uso wake, kwa kuwa aliogopa kumwangalia Mungu.
7 Then the Lord said, I haue surely seene the trouble of my people, which are in Egypt, and haue heard their crie, because of their taskemasters: for I knowe their sorowes.
Yahwe akasema, “Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri. Nimesikia kelele zao kwa sababu ya mabwana wao, kwa kuwa nayajua mateso yao.
8 Therefore I am come downe to deliuer them out of the hande of the Egyptians, and to bring them out of that lande into a good lande and a large, into a lande that floweth with milke and honie, euen into the place of the Canaanites, and the Hittites, and the Amorites, and the Perizzites, and the Hiuites, and the Iebusites.
Nimekuja chini kuwaokoa dhidi ya mamlaka ya Wamisri na kuwatoa katika nchi ile na kuwaleta katika nchi nzuri, pana, nchi ijaayo maziwa na asali; kwenye ukanda wa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
9 And now lo, the crie of the children of Israel is come vnto me, and I haue also seene ye oppression, wherewith the Egyptians oppresse them.
Sasa kilio cha watu wa Israeli kimenifikia mimi. Zaidi sana, Mimi nimeyaona mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
10 Come now therefore, and I will send thee vnto Pharaoh, that thou maiest bring my people the children of Israel out of Egypt.
Sasa basi, nitakutuma wewe kwa Farao ili upate kuwatoa watu wangu, wana wa Israeli, kutoka katika nchi ya Misri.”
11 But Moses said vnto God, Who am I, that I should go vnto Pharaoh, and that I should bring the children of Israel out of Egypt?
Lakini Musa akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao na kuwatoa Waisraeli kutoka Misri?”
12 And he answered, Certainely I will be with thee: and this shall be a token vnto thee, that I haue sent thee, After that thou hast brought the people out of Egypt, ye shall serue God vpon this Mountaine.
Mungu akamjibu, “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako ya kuwa nimekutuma. Utakapokuwa umewatoa watu kutoka Misri, mtaniabubu mimi katika mlima huu.”
13 Then Moses said vnto God, Behold, when I shall come vnto the children of Israel, and shall say vnto them, The God of your fathers hath sent me vnto you: if they say vnto me, What is his Name? what shall I say vnto them?
Musa akamwambia Mungu, “Nikienda kwa Waisraeli na kuwaambia, 'Mungu wa baba zenu amenituma mimi kwenu,' na kisha wakiniambia, 'jina lake nani?' nitawaambia nini?”
14 And God answered Moses, I Am That I Am. Also he said, Thus shalt thou say vnto the children of Israel, I Am hath sent me vnto you.
Mungu akamwambia Musa, “MIMI NIPO AMBAYE NIPO.” Mungu akasema, “Ni lazima uwaambie Waisraeli, “MIMI NIPO amenituma kwenu.”
15 And God spake further vnto Moses, Thus shalt thou say vnto the children of Israel, The Lord God of your fathers, the God of Abraham, the God of Izhak, and the God of Iaakob hath sent me vnto you: this is my Name for euer, and this is my memoriall vnto all ages.
Pia Mungu akamwambia Musa, “Lazima uwaambie Waisraeli, 'Yahwe, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amenituma mimi kwenu. Hili ndio jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa na vizazi vyote.'
16 Go and gather the Elders of Israel together, and thou shalt say vnto the, The Lord God of your fathers, the God of Abraham, Izhak, and Iaakob appeared vnto me, and said, I haue surely remembred you, and that which is done to you in Egypt.
Nenda ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja. Waambie, 'Yahwe, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, wa Isaka na Yakobo, amenitokea mimi na kusema, “Hakika nimewatazama na nimeona yale mliyotendewa huko Misri.
17 Therefore I did say, I wil bring you out of the affliction of Egypt vnto the land of the Canaanites, and the Hittites, and the Amorites, and the Perizzites, and the Hiuites, and the Iebusites, vnto a lande that floweth with milke and honie.
Nimeahidi kuwatoa ninyi katika mateso ya Misri na kuwaleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Wamwori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi. Nchi ijaayo maziwa na asali.”
18 Then shall they obey thy voyce, and thou and the Elders of Israel shall go vnto the King of Egypt, and say vnto him, The Lord God of the Ebrewes hath met with vs: we pray thee nowe therefore, let vs goe three dayes iourney in the wildernesse, that we may sacrifice vnto the Lord our God.
Watakusikiliza. Wewe pamoja na wazee wa Israeeli itawapasa kwenda kwa mfalme wa Misri, na imewapasa kumwambia, 'Yahwe, Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Hivyo tuache sisi twende safari ya siku tatu katika jangwa ili tupate kutoa sadaka kwa Yahwe Mungu wetu.'
19 But I know, that the King of Egypt wil not let you goe, but by strong hande.
Lakini nafahamu ya kuwa mfalme wa Misri hatawaacha ninyi mwende, isipokuwa kwa kulazimishwa.
20 Therefore will I stretch out mine hande and smite Egypt with all my wonders, which I will doe in the middes thereof: and after that shall he let you goe.
Nitainua mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa miujiza yote nitakayoifanya kati yao. Baada ya hayo, atawaacha mwende.
21 And I will make this people to be fauoured of the Egyptians: so that when ye go, ye shall not goe emptie.
Nitawapa watu hawa kufadhiliwa kutoka kwa Wamisri ili muondokapo msiende mikono mitupu.
22 For euery woman shall aske of her neighbour, and of her that soiourneth in her house, iewels of siluer and iewels of gold and raiment, and ye shall put them on your sonnes, and on your daughters, and shall spoyle the Egyptians.
Kila mwanamke ataomba kwa jirani yake Mmisri na kwa kila mwanamke akaaye kwenye nyumba ya jirani yake, vyombo vya fedha na vya dhahabu na nguo. Nanyi mtawavika watoto wenu wa kiume na binti zenu. Kwa njia hii mtawateka nyara Wamisri.”

< Exodus 3 >