< Exodus 12 >

1 Then the Lord spake to Moses and to Aaron in the land of Egypt, saying,
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 This moneth shalbe vnto you the beginning of moneths: it shalbe to you the first moneth of the yere.
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 Speake ye vnto all the congregation of Israel, saying, In the tenth of this moneth let euery man take vnto him a lambe, according to the house of the fathers, a lambe for an house.
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 And if the housholde be too litle for the lambe, he shall take his neighbour, which is next vnto his house, according to the nomber of the persons: euery one of you, according to his eating shall make your count for the lambes,
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 Your lambe shalbe without blemish, a male of a yeere olde: ye shall take it of the lambes, or of the kiddes.
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 And yee shall keepe it vntill the fourteenth day of this moneth: then al the multitude of the Congregation of Israel shall kill it at euen.
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 After, they shall take of the blood, and strike it on the two postes, and on the vpper doore post of the houses where they shall eate it.
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 And they shall eate the flesh the same night, roste with fire, and vnleauened bread: with sowre herbes they shall eate it.
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 Eate not thereof rawe, boyled nor sodden in water, but rost with fire, both his head, his feete, and his purtenance.
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 And ye shall reserue nothing of it vnto the morning: but that, which remaineth of it vnto the morowe, shall ye burne with fire.
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 And thus shall yee eate it, Your loynes girded, your shoes on your feete, and your staues in your handes, and yee shall eate it in haste: for it is the Lords Passeouer.
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 For I will passe through the lande of Egypt the same night, and will smite all the first borne in the land of Egypt, both man and beast, and I will execute iudgement vpon all the gods of Egypt. I am the Lord.
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 And the blood shalbe a token for you vpon the houses where ye are: so when I see the blood, I will passe ouer you, and the plague shall not be vpon you to destruction, when I smite the lande of Egypt.
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 And this day shalbe vnto you a remembrance: and ye shall keepe it an holie feast vnto the Lord, throughout your generations: yee shall keepe it holie by an ordinance for euer.
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 Seuen daies shall ye eat vnleauened bread, and in any case ye shall put away leauen the first day out of your houses: for whosoeuer eateth leauened bread from the first daie vntill the seuenth day, that person shalbe cut off from Israel.
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 And in the first day shalbe an holie assemblie: also in the seuenth day shalbe an holy assemblie vnto you: no worke shalbe done in them, saue about that which euery man must eate: that onely may ye do.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 Ye shall keepe also the feast of vnleauened bread: for that same daye I will bring your armies out of the lande of Egypt: therefore ye shall obserue this day, throughout your posteritie, by an ordinance for euer.
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 In the first moneth and the fourteenth day of the moneth at euen, yee shall eate vnleauened bread vnto the one and twentieth day of the moneth at euen.
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
19 Seuen daies shall no leauen be founde in your houses: for whosoeuer eateth leauened bread, that person shalbe cut off from the Congregation of Israel: whether he bee a stranger, or borne in the land.
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 Ye shall eate no leauened bread: but in all your habitations shall ye eate vnleauened bread.
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Then Moses called all the Elders of Israel, and saide vnto them, Choose out and take you for euerie of your housholdes a lambe, and kill the Passeouer.
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 And take a bunch of hyssop, and dip it in the blood that is in the basen, and strike the lintell, and the doore cheekes with the blood that is in the basen, and let none of you goe out at the doore of his house, vntill the morning.
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 For the Lord will passe by to smite the Egyptians: and when he seeth the blood vpon the lintel and on the two doore cheekes, the Lord wil passe ouer the doore, and wil not suffer the destroyer to come into your houses to plague you.
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 Therefore shall ye obserue this thing as an ordinance both for thee and thy sonnes for euer.
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 And when ye shall come into the land, which the Lord will giue you as hee hath promised, then ye shall keepe this seruice.
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 And when your children aske you, What seruice is this ye keepe?
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 Then ye shall saye, It is the sacrifice of the Lordes Passeouer, which passed ouer the houses of the children of Israel in Egypt, when he smote the Egyptians, and preserued our houses. Then the people bowed them selues, and worshipped.
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 So the children of Israel went, and did as the Lord had commanded Moses and Aaron: so did they.
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 Nowe at midnight, the Lord smote all the first borne in the lande of Egypt, from the first borne of Pharaoh that sate on his throne, vnto the first borne of the captiue that was in prison, and all the first borne of beastes.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 And Pharaoh rose vp in the night, he, and all his seruants and all the Egyptians: and there was a great crye in Egypt: for there was no house where there was not one dead.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 And hee called to Moses and to Aaron by night, and saide, Rise vp, get you out from among my people, both yee, and the children of Israel, and goe serue the Lord as ye haue sayde.
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 Take also your sheepe and your cattell as yee haue sayde, and depart, and blesse me also.
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 And the Egyptians did force the people, because they would send them out of the land in haste: for they said, We die all.
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 Therfore the people tooke their dough before it was leauened, euen their dough bound in clothes vpon their shoulders.
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 And the children of Israel did according to the saying of Moses, and they asked of ye Egyptians iewels of siluer and iewels of gold, and raiment.
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 And the Lord gaue the people fauour in the sight of the Egyptians: and they graunted their request: so they spoyled the Egyptians.
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 Then the children of Israel tooke their iourney from Rameses to Succoth about sixe hundreth thousand men of foote, beside children.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 And a great multitude of sundrie sortes of people went out with them, and sheepe, and beeues, and cattel in great abundance.
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 And they baked the dough which they brought out of Egypt, and made vnleauened cakes: for it was not leauened, because they were thrust out of Egypt, neither coulde they tarie, nor yet prepare themselues vitailes.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 So the dwelling of the children of Israel, while they dwelled in Egypt, was foure hundreth and thirtie yeres.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 And when the foure hundreth and thirtie yeeres were expired, euen the selfe same day departed all the hostes of the Lord out of the land of Egypt.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 It is a night to be kept holie to the Lord, because he brought them out of the lande of Egypt: this is that night of the Lord, which all the children of Israel must keepe throughout their generations.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 Also the Lord said vnto Moses and Aaron, This is the Lawe of the Passeouer: no stranger shall eate thereof.
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44 But euerie seruant that is bought for money, when thou hast circumcised him, then shall he eat thereof.
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 A stranger or an hyred seruant shall not eat thereof.
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 In one house shall it bee eaten: thou shalt carie none of ye flesh out of the house, neither shall ye breake a bone thereof.
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 All the Congregation of Israel shall obserue it.
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 But if a stranger dwell with thee, and will obserue the Passeouer of the Lord, let him circumcise all the males, that belong vnto him, and then let him come and obserue it, and he shall be as one that is borne in the land: for none vncircumcised person shall eate thereof.
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 One lawe shalbe to him that is borne in the land, and to the stranger that dwelleth among you.
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 Then all the children of Israel did as the Lord commanded Moses and Aaron: so did they.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 And the selfe same day did the Lord bring the children of Israel out of the land of Egypt by their armies.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

< Exodus 12 >