< Deuteronomy 33 >

1 Nowe this is the blessing wherewith Moses the man of God blessed the children of Israel before his death, and said,
Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
2 The Lord came from Sinai, and rose vp from Seir vnto them, and appeared clearely from mount Paran, and he came with ten thousands of Saints, and at his right hand a firie Lawe for them.
Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
3 Though hee loue the people, yet all thy Saints are in thine handes: and they are humbled at thy foete, to receiue thy words.
Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
4 Moses commanded vs a Lawe for an inheritance of the Congregation of Iaakob.
Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
5 Then he was among the righteous people, as King, when the heades of the people, and the tribes of Israel were assembled.
Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
6 Let Reuben liue, and not die, though his men be a small nomber.
Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
7 And thus he blessed Iudah, and said, Heare, O Lord, the voyce of Iudah, and bring him vnto his people: his hands shalbe sufficient for him, if thou helpe him against his enemies.
Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
8 And of Leui he said, Let thy Thummim and thine Vrim be with thine Holy one, whome thou diddest proue in Massah, and didst cause him to striue at the waters of Meribah.
Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
9 Who said vnto his father and to his mother, I haue not seene him, neither knewe he his brethren, nor knewe his owne children: for they obserued thy word, and kept thy couenant.
Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
10 They shall teach Iaakob thy iudgements, and Israel thy Lawe: they shall put incense before thy face, and the burnt offring vpon thine altar.
Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
11 Blesse, O Lord, his substance, and accept the worke of his handes: smite through ye loynes of them that rise against him, and of them that hate him, that they rise not againe.
Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
12 Of Beniamin he said, The beloued of the Lord shall dwell in safetie by him: the Lord shall couer him all the day long, and dwell betweene his shoulders.
Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
13 And of Ioseph hee sayde, Blessed of the Lord is his land for the sweetenesse of heauen, for the dewe, and for the depth lying beneath,
Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
14 And for the sweete increase of the sunne, and for the sweete increase of the moone,
Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
15 And for the sweetenes of the top of the ancient mountaines, and for the sweetenes of the olde hilles,
kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
16 And for the sweetenesse of the earth, and abundance thereof: and the good will of him that dwelt in the bushe, shall come vpon the head of Ioseph, and vpon the toppe of the head of him that was separated from his brethren.
Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
17 His beautie shalbe like his first borne bullock, and his hornes as the hornes of an vnicorne: with them hee shall smite the people together, euen the endes of the world: these are also the ten thousands of Ephraim, and these are the thousands of Manasseh.
Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
18 And of Zebulun he sayd, Reioice, Zebulun, in thy going out, and thou Isshachar in thy tents.
Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
19 They shall call ye people vnto the mountaine: there they shall offer the sacrifices of righteousnesse: for they shall sucke of the abundance of the sea, and of the treasures hid in the sand.
Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
20 Also of Gad he said, Blessed be hee that enlargeth Gad: he dwelleth as a lion, that catcheth for his praye the arme with the head.
Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
21 And hee looked to himselfe at the beginning, because there was a portion of the Lawe-giuer hid: yet hee shall come with the heades of the people, to execute the iustice of the Lord, and his iudgements with Israel.
Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
22 And of Dan he said, Dan is a lions whelp: he shall leape from Bashan.
Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
23 Also of Naphtali he sayd, O Naphtali, satisfied with fauour, and filled with the blessing of the Lord, possesse the West and the South.
Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
24 And of Asher he saide, Asher shalbe blessed with children: he shalbe acceptable vnto his brethren, and shall dippe his foote in oyle.
Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
25 Thy shooes shalbe yron and brasse, and thy strength shall continue as long as thou liuest.
Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
26 There is none like God, O righteous people, which rideth vpon the heauens for thine helpe, and on the cloudes in his glory.
Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
27 The eternall God is thy refuge, and vnder his armes thou art for euer: hee shall cast out the enemie before thee, and will say, Destroy them.
Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
28 Then Israel the fountaine of Iaakob shall dwell alone in safetie in a lande of wheat, and wine: also his heauens shall drop the dewe.
Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
29 Blessed art thou, O Israel: who is like vnto thee, O people saued by the Lord, the shielde of thine helpe, and which is the sword of thy glorie? therefore thine enemies shall bee in subiection to thee, and thou shalt tread vpon their hie places.
Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.

< Deuteronomy 33 >