< Deuteronomy 27 >

1 Then Moses with the Elders of Israel commanded the people, saying, Keepe all the comandements, which I command you this day.
Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
2 And when ye shall passe ouer Iorden vnto the lande which the Lord thy God giueth thee, thou shalt set thee vp great stones, and playster them with plaister,
Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
3 And shalt write vpon them all the words of this Lawe, when thou shalt come ouer, that thou mayest go into the land which the Lord thy God giueth thee: a land that floweth with milke and hony, as the Lord God of thy fathers hath promised thee.
Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
4 Therefore when ye shall passe ouer Iorden, ye shall set vp these stones, which I command you this daye in mount Ebal, and thou shalt plaister them with plaister.
Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
5 And there shalt thou build vnto the Lord thy God an altar, euen an altar of stones: thou shalt lift none yron instrument vpon them.
Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
6 Thou shalt make the altar of the Lord thy God of whole stones, and offer burnt offerings thereon vnto the Lord thy God.
Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
7 And thou shalt offer peace offrings, and shalt eate there and reioyce before the Lord thy God:
Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
8 And thou shalt write vpon the stones al the words of this Law, well and plainely.
Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
9 And Moses and the Priestes of the Leuites spake vnto all Israel, saying, Take heede and heare, O Israel: this day thou art become the people of the Lord thy God.
Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
10 Thou shalt hearken therefore vnto the voyce of the Lord thy God, and do his commandements and his ordinances, which I commande thee this day.
Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
11 And Moses charged the people the same day, saying,
Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
12 These shall stand vpon mount Gerizzim, to blesse the people when ye shall passe ouer Iorden: Simeon, and Leui, and Iudah, and Issachar, and Ioseph, and Beniamin.
Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
13 And these shall stand vpon mount Ebal to curse: Reuben, Gad, and Asher, and Zebulun, Dan, and Naphtali.
Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
14 And the Leuites shall answere and say vnto all the men of Israel with a loude voyce,
Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 Cursed be the man that shall make any carued or molten image, which is an abomination vnto the Lord, the worke of the hands of the craftesman, and putteth it in a secrete place: And all the people shall answere, and say: So be it.
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16 Cursed be he that curseth his father and his mother: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17 Cursed be he that remoueth his neighbors marke: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18 Cursed be he that maketh ye blinde go out of the way: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19 Cursed be he that hindreth the right of the stranger, the fatherles, and the widow: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20 Cursed be hee that lyeth with his fathers wife: for he hath vncouered his fathers skirt: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21 Cursed be he that lieth with any beast: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22 Cursed be he that lyeth with his sister, the daughter of his father, or the daughter of his mother: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23 Cursed be he that lyeth with his mother in law: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24 Cursed be hee that smiteth his neyghbour secretly: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25 Cursed be he that taketh a reward to put to death innocent blood: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26 Cursed be he that confirmeth not all the wordes of this Law, to do them: And all the people shall say: So be it.
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

< Deuteronomy 27 >