< Daniel 3 >

1 Nebuchad-nezzar the King made an image of gold, whose height was three score cubits, and the breadth thereof sixe cubites: hee set it vp in the plaine of Dura, in the prouince of Babel.
Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
2 Then Nebuchad-nezzar ye King sent foorth to gather together the nobles, the princes and the dukes, the iudges, the receiuers, the counsellers, the officers, and all the gouernours of the prouinces, that they should come to the dedication of the image, which Nebuchad-nezzar the King had set vp.
Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
3 So the nobles, princes and dukes, the iudges, the receiuers, the counsellers, the officers, and all the gouernours of the prouinces were assembled vnto the dedicating of the image, that Nebuchad-nezzar the King had set vp: and they stood before the image, which Nebuchad-nezzar had set vp.
Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
4 Then an herald cried aloude, Be it knowen to you, O people, nations, and languages,
Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
5 That when ye heare the sound of the cornet, trumpet, harpe, sackebut, psalterie, dulcimer, and all instruments of musike, ye fall downe and worship the golden image, that Nebuchad-nezzar the King hath set vp,
Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
6 And whosoeuer falleth not downe and worshippeth, shall the same houre bee cast into the middes of an hote fierie fornace.
Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
7 Therefore assoone as all the people heard the sound of the cornet, trumpet, harpe, sackebut, psalterie, and all instruments of musike, all the people, nations, and languages fell downe, and worshipped the golden image, that Nebuchad-nezzar the King had set vp.
Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
8 By reason whereof at that same time came men of the Caldeans, and grieuously accused the Iewes.
Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
9 For they spake and said to the King Nebuchad-nezzar, O King, liue for euer.
Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
10 Thou, O King, hast made a decree, that euery man that shall heare the sounde of the cornet, trumpet, harpe, sackebut, psalterie, and dulcimer, and all instruments of musike, shall fall downe and worship the golden image,
Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
11 And whosoeuer falleth not downe, and worshippeth, that he should be cast into the mids of an hote fierie fornace.
na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
12 There are certeine Iewes whome thou hast set ouer the charge of ye prouince of Babel, Shadrach, Meshach, and Abednego: these men, O King, haue not regarded thy commandement, neither wil they serue thy gods, nor worship the golden image, that thou hast set vp.
Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
13 Then Nebuchad-nezzar in his anger and wrath commanded that they should bring Shadrach, Meshach, and Abednego: so these men were brought before the King.
Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
14 And Nebuchad-nezzar spake, and said vnto them, What disorder? will not you, Shadrach, Meshach, and Abednego serue my god, nor worship the golden image, that I haue set vp?
naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Now therefore are ye ready when ye heare the sound of the cornet, trumpet, harpe, sackebut, psalterie, and dulcimer, and all instruments of musike, to fall downe, and worship the image, which I haue made? for if ye worship it not, ye shall be cast immediatly into the middes of an hote fierie fornace: for who is that God, that can deliuer you out of mine handes?
Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
16 Shadrach, Meshach, and Abednego answered and said to the King, O Nebuchad-nezzar, we are not carefull to answere thee in this matter.
Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
17 Beholde, our God whom we serue, is able to deliuer vs from the hote fierie fornace, and hee will deliuer vs out of thine hand, O King.
Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
18 But if not, bee it knowen to thee, O King, that wee will not serue thy gods, nor worship the golden image, which thou hast set vp.
Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
19 Then was Nebuchad-nezzar full of rage, and the forme of his visage was changed against Shadrach, Meshach, and Abednego: therefore hee charged and commanded that they should heate the fornace at once seuen times more then it was wont to be heat.
Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
20 And hee charged the most valiant men of warre that were in his armie, to binde Shadrach, Meshach, and Abednego, and to cast them into the hote fierie fornace.
na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
21 So these men were bounde in their coates, their hosen, and their clokes, with their other garments, and cast into the middes of the hote fierie fornace.
Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
22 Therefore, because the Kings commandement was straite, that the fornace should be exceeding hote, the flame of the fire slew those men that brought foorth Shadrach, Meshach and Abednego.
Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
23 And these three men Shadrach, Meshach and Abednego fell downe bound into the middes of the hote fierie fornace.
Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
24 Then Nebuchad-nezzar the King was astonied and rose vp in haste, and spake, and saide vnto his counsellers, Did not wee cast three men bound into the middes of the fire? Who answered and said vnto the King, It is true, O King.
Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
25 And he answered, and said, Loe, I see foure men loose, walking in the middes of the fire, and they haue no hurt, and the forme of the fourth is like the sonne of God.
Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
26 Then the King Nebuchad-nezzar came neere to the mouth of the hote fierie fornace, and spake and said, Shadrach, Meshach and Abednego, the seruants of the hie God goe foorth and come hither: so Shadrach, Meshach and Abednego came foorth of the middes of the fire.
Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
27 Then the nobles, princes and dukes, and the Kings counsellers came together to see these men, because the fire had no power ouer their bodies: for not an heare of their head was burnt, neither was their coates changed, nor any smelll of fire came vpon them.
Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
28 Wherefore Nebuchad-nezzar spake and said, Blessed be the God of Shadrach, Meshach and Abednego, who hath sent his Angel, and deliuered his seruants, that put their trust in him, and haue changed the Kings commandement, and yeelded their bodies rather then they would serue or worship any god, saue their owne God.
Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
29 Therefore I make a decree, that euery people, nation, and language, which speake any blasphemie against the God of Shadrach, Meshach and Abednego, shalbe drawen in pieces, and their houses shall be made a iakes, because there is no god that can deliuer after this sort.
Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
30 Then the King promoted Shadrach, Meshach and Abednego in the prouince of Babel.
Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.

< Daniel 3 >