< Daniel 2 >

1 And in the seconde yeere of the raygne of Nebuchad-nezzar, Nebuchad-nezzar dreamed dreames wherewith his spirite was troubled, and his sleepe was vpon him.
Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala.
2 Then the King commanded to call the inchanters, and the astrologians and the sorcerers, and the Caldeans for to shewe the King his dreames: so they came and stoode before the King.
Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme,
3 And the King sayde vnto them, I haue dreamed a dreame, and my spirite was troubled to knowe the dreame.
akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
4 Then spake the Caldeans to the King in the Aramites language, O King, liue for euer: shewe thy seruants thy dreame, and wee shall shewe the interpretation.
Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu, “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
5 And the King answered and sayd to the Caldeans, The thing is gone from me. If ye will not make me vnderstande the dreame with the interpretation thereof, ye shall be drawen in pieces, and your houses shall be made a iakes.
Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi.
6 But if yee declare the dreame and the interpretation thereof, ye shall receyue of me gifts and rewardes, and great honour: therefore shewe me the dreame and the interpretation of it.
Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
7 They answered againe, and sayde, Let the King shewe his seruantes the dreame, and wee will declare the interpretation thereof.
Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
8 Then the King answered, and sayd, I knowe certeinly that ye would gaine the time, because ye see the thing is gone from me.
Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti:
9 But if ye will not declare mee the dreame, there is but one iudgement for you: for ye haue prepared lying and corrupt wordes, to speake before me till the time bee changed: therefore tell me the dreame, that I may knowe, if yee can declare me the interpretation thereof.
Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
10 Then the Caldeans answered before the King, and sayde, There is no man vpon earth that can declare the Kings matter: yea, there is neither king nor prince nor lorde that asked such things at an inchanter or astrologian or Caldean.
Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote.
11 For it is a rare thing that the King requireth, and there is none other that can declare it before the King, except the gods whose dwelling is not with flesh.
Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
12 For this cause the king was angrie and in great furie, and commanded to destroy all the wise men of Babel.
Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli.
13 And when sentence was giuen, the wise men were slayne: and they sought Daniel and his fellowes to be put to death.
Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
14 Then Daniel answered with counsel and wisedome to Arioch the Kings chiefe stewarde, which was gone foorth to put to death the wise men of Babel.
Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara.
15 Yea, he answered and sayde vnto Arioch the kings captaine, Why is the sentence so hastie from the king? Then Arioch declared the thing to Daniel.
Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo.
16 So Daniel went and desired the king that he woulde giue him leasure and that he woulde shewe the king the interpretation thereof.
Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
17 The Daniel went to his house and shewed the matter to Hananiah, Mishael, and Azariah his companions,
Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.
18 That they should beseech the God of heauen for grace in this secrete, that Daniel and his fellowes should not perish with the rest of ye wise men of Babel.
Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.
19 Then was the secret reueiled vnto Daniel in a vision by night: therefore Daniel praysed the God of heauen.
Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni,
20 And Daniel answered and sayde, The Name of God be praysed for euer and euer: for wisedome and strength are his,
na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
21 And hee changeth the times and seasons: he taketh away kings: he setteth vp kings: he giueth wisedome vnto the wise, and vnderstanding to those that vnderstand.
Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
22 Hee discouereth the deepe and secrete things: he knoweth what is in darkenes, and the light dwelleth with him.
Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.
23 I thanke thee and prayse thee, O thou God of my fathers, that thou hast giuen mee wisedome and strength, and hast shewed me nowe the thing that wee desired of thee: for thou hast declared vnto vs the kings matter.
Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu: Umenipa hekima na uwezo, umenijulisha kile tulichokuomba, umetujulisha ndoto ya mfalme.”
24 Therefore Daniel went vnto Arioch, whome the King had ordeyned to destroy the wise men of Babel: he went and sayde thus vnto him, Destroy not the wise men of Babel, but bring me before the King, and I will declare vnto the King the interpretation.
Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
25 Then Arioch brought Daniel before the King in all haste, and sayd thus vnto him, I haue found a man of the children of Iudah that were brought captiues, that will declare vnto the King the interpretation.
Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
26 Then answered the King, and sayde vnto Daniel, whose name was Belteshazzar, Art thou able to shew me the dreame, which I haue seene, and the interpretation thereof?
Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
27 Daniel answered in the presence of the King, and sayd, The secret which the King hath demanded, can neither the wise, the astrologians, the inchanters, nor the southsayers declare vnto the King.
Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza,
28 But there is a God in heauen that reueileth secrets, and sheweth the King Nebuchad-nezzar what shall bee in the latter dayes. Thy dreame, and the things which thou hast seene in thine heade vpon thy bed, is this.
lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
29 O King, when thou wast in thy bedde, thoughts came into thy mind, what should come to passe hereafter, and he that reueyleth secretes, telleth thee, what shall come.
“Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea.
30 As for me, this secret is not shewed mee for any wisedome that I haue, more then any other liuing, but onely to shewe the King the interpretation, and that thou mightest knowe the thoughts of thine heart.
Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
31 O King, thou sawest, and beholde, there was a great image: this great image whose glory was so excellent, stood before thee, and the forme thereof was terrible.
“Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake.
32 This images head was of fine golde, his breast and his armes of siluer, his bellie and his thighs of brasse,
Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba,
33 His legges of yron, and his feete were part of yron, and part of clay.
miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa.
34 Thou beheldest it til a stone was cut without hands, which smote the image vpon his feete, that were of yron and clay, and brake them to pieces.
Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja.
35 Then was the yron, the clay, the brasse, the siluer and the golde broken all together, and became like the chaffe of the sommer floures, and the winde caryed them away, that no place was founde for them: and the stone that smote the image, became a great mountaine, and filled the whole earth.
Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
36 This is the dreame, and we will declare before the King the interpretation thereof.
“Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme.
37 O King, thou art a king of Kings: for the God of heauen hath giuen thee a kingdome, power, and strength, and glorie.
Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu.
38 And in all places where the children of men dwell, the beasts of the fielde, and the foules of the heauen hath he giuen into thine hand, and hath made thee ruler ouer them al: thou art this heade of golde.
Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
39 And after thee shall rise another kingdome, inferiour to thee, of siluer, and another third kingdome shalbe of brasse, which shall beare rule ouer all the earth.
“Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote.
40 And the fourth kingdome shall be strong as yron: for as yron breaketh in pieces, and subdueth all things, and as yron bruiseth all these things, so shall it breake in pieces, and bruise all.
Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote.
41 Where as thou sawest the feete and toes, parte of potters clay, and part of yron: the kingdome shalbe deuided, but there shalbe in it of the strength of the yron, as thou sawest the yron mixt with the clay, and earth.
Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi.
42 And as the toes of the feete were parte of yron, and parte of clay, so shall the kingdome be partly strong, and partly broken.
Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu.
43 And where as thou sawest yron mixt with clay and earth, they shall mingle themselues with the seede of men: but they shall not ioyne one with another, as yron can not bee mixed with clay.
Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
44 And in the dayes of these Kings, shall the God of heauen set vp a kingdome, which shall neuer be destroyed: and this kingdome shall not be giuen to another people, but it shall breake, and destroy al these kingdomes, and it shall stand for euer.
“Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele.
45 Where as thou sawest, that the stone was cut of the mountaine without handes, and that it brake in pieces the yron, the brasse, the clay, the siluer, and the golde: so the great God hath shewed the King, what shall come to passe hereafter, and the dreame is true, and the interpretation thereof is sure.
Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande. “Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
46 Then the King Nebuchad-nezzar fell vpon his face, and bowed himselfe vnto Daniel, and commanded that they should offer meate offrings, and sweete odours vnto him.
Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba.
47 Also the King answered vnto Daniel, and said, I know of a trueth that your God is a God of gods, and the Lord of Kings, and the reueiler of secrets, seeing thou couldest open this secret.
Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
48 So the King made Daniel a great man, and gaue him many and great giftes. Hee made him gouernour ouer the whole prouince of Babel, and chiefe of the rulers, and aboue all the wise men of Babel.
Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote.
49 Then Daniel made request to the King, and hee set Shadrach, Meshach, and Abednego ouer the charge of the prouince of Babel: but Daniel sate in the gate of the King.
Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.

< Daniel 2 >